< John 4 >

1 When therefore the Lord knew that the Pharisees had heard that Jesus makes and baptises more disciples than John
Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2 (however, Jesus himself did not baptise, but his disciples),
(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3 he left Judaea and went away again unto Galilee.
Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4 And he must needs pass through Samaria.
na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5 He comes therefore to a city of Samaria called Sychar, near to the land which Jacob gave to his son Joseph.
Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6 Now a fountain of Jacob's was there; Jesus therefore, being wearied with the way he had come, sat just as he was at the fountain. It was about the sixth hour.
Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7 A woman comes out of Samaria to draw water. Jesus says to her, Give me to drink
Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, “Nipatie maji ninywe.”
8 (for his disciples had gone away into the city that they might buy provisions).
(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9 The Samaritan woman therefore says to him, How dost thou, being a Jew, ask to drink of me who am a Samaritan woman? for Jews have no intercourse with Samaritans.
Lakini huyo mwanamke akamwambia, “Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?” (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10 Jesus answered and said to her, If thou knewest the gift of God, and who it is that says to thee, Give me to drink, thou wouldest have asked of him, and he would have given thee living water.
Yesu akamjibu, “Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai.”
11 The woman says to him, Sir, thou hast nothing to draw with, and the well is deep: whence then hast thou the living water?
Huyo mama akasema, “Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12 Art thou greater than our father Jacob, who gave us the well, and drank of it himself, and his sons, and his cattle?
Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki.”
13 Jesus answered and said to her, Every one who drinks of this water shall thirst again;
Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14 but whosoever drinks of the water which I shall give him shall never thirst for ever, but the water which I shall give him shall become in him a fountain of water, springing up into eternal life. (aiōn g165, aiōnios g166)
Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 The woman says to him, Sir, give me this water, that I may not thirst nor come here to draw.
Huyo mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji.”
16 Jesus says to her, Go, call thy husband, and come here.
Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa.”
17 The woman answered and said, I have not a husband. Jesus says to her, Thou hast well said, I have not a husband;
Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume.
18 for thou hast had five husbands, and he whom now thou hast is not thy husband: this thou hast spoken truly.
Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.”
19 The woman says to him, Sir, I see that thou art a prophet.
Huyo Mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20 Our fathers worshipped in this mountain, and ye say that in Jerusalem is the place where one must worship.
Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu.”
21 Jesus says to her, Woman, believe me, [the] hour is coming when ye shall neither in this mountain nor in Jerusalem worship the Father.
Yesu akamwambia, “Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22 Ye worship ye know not what; we worship what we know, for salvation is of the Jews.
Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23 But [the] hour is coming and now is, when the true worshippers shall worship the Father in spirit and truth; for also the Father seeks such as his worshippers.
Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24 God [is] a spirit; and they who worship him must worship [him] in spirit and truth.
Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake.”
25 The woman says to him, I know that Messias is coming, who is called Christ; when he comes he will tell us all things.
Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.”
26 Jesus says to her, I who speak to thee am [he].
Yesu akamwambia, “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”
27 And upon this came his disciples, and wondered that he spoke with a woman; yet no one said, What seekest thou? or, Why speakest thou with her?
Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?”
28 The woman then left her waterpot and went away into the city, and says to the men,
Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29 Come, see a man who told me all things I had ever done: is not he the Christ?
“Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?”
30 They went out of the city and came to him.
Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31 But meanwhile the disciples asked him saying, Rabbi, eat.
Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, ule chakula.”
32 But he said to them, I have food to eat which ye do not know.
Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
33 The disciples therefore said to one another, Has any one brought him [anything] to eat?
Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?”
34 Jesus says to them, My food is that I should do the will of him that has sent me, and that I should finish his work.
Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35 Do not ye say, that there are yet four months and the harvest comes? Behold, I say to you, Lift up your eyes and behold the fields, for they are already white to harvest.
Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36 He that reaps receives wages and gathers fruit unto life eternal, that both he that sows and he that reaps may rejoice together. (aiōnios g166)
Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja. (aiōnios g166)
37 For in this is [verified] the true saying, It is one who sows and another who reaps.
Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38 I have sent you to reap that on which ye have not laboured; others have laboured, and ye have entered into their labours.
Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao.”
39 But many of the Samaritans of that city believed on him because of the word of the woman who bore witness, He told me all things that I had ever done.
Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: “Ameniambia mambo yote niliyofanya.”
40 When therefore the Samaritans came to him they asked him to abide with them, and he abode there two days.
Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41 And more a great deal believed on account of his word;
Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42 and they said to the woman, [It is] no longer on account of thy saying that we believe, for we have heard him ourselves, and we know that this is indeed the Saviour of the world.
Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”
43 But after the two days he went forth thence and went away into Galilee,
Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44 for Jesus himself bore witness that a prophet has no honour in his own country.
Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, “Nabii hapati heshima katika nchi yake.”
45 When therefore he came into Galilee, the Galileans received him, having seen all that he had done in Jerusalem during the feast, for they also went to the feast.
Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46 He came therefore again to Cana of Galilee, where he made the water wine. And there was a certain courtier in Capernaum whose son was sick.
Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47 He, having heard that Jesus had come out of Judaea into Galilee, went to him and asked [him] that he would come down and heal his son, for he was about to die.
Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48 Jesus therefore said to him, Unless ye see signs and wonders ye will not believe.
Yesu akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!”
49 The courtier says to him, Sir, come down ere my child die.
Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa.”
50 Jesus says to him, Go, thy son lives. And the man believed the word which Jesus said to him, and went his way.
Yesu akamwambia, “Nenda tu, mwanao yu mzima.” Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51 But already, as he was going down, his servants met him and brought [him] word saying, Thy child lives.
Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52 He inquired therefore from them the hour at which he got better. And they said to him, Yesterday at the seventh hour the fever left him.
Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, “Jana saa saba mchana, homa ilimwacha.”
53 The father therefore knew that [it was] in that hour in which Jesus said to him, Thy son lives; and he believed, himself and his whole house.
Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: “Mwanao yu mzima.” Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54 This second sign again did Jesus, being come out of Judaea into Galilee.
Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.

< John 4 >