< John 16 >

1 These things I have spoken unto you that ye may not be offended.
“Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu.
2 They shall put you out of the synagogues; but the hour is coming that every one who kills you will think to render service to God;
Watu watawatenga ninyi na masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua ninyi atadhani anamhudumia Mungu.
3 and these things they will do because they have not known the Father nor me.
Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi.
4 But I have spoken these things to you, that when their hour shall have come, ye may remember them, that I have said [them] unto you. But I did not say these things unto you from [the] beginning, because I was with you.
Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni. “Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 But now I go to him that has sent me, and none of you demands of me, Where goest thou?
Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: Unakwenda wapi?
6 But because I have spoken these things to you, sorrow has filled your heart.
Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu.
7 But I say the truth to you, It is profitable for you that I go away; for if I do not go away, the Comforter will not come to you; but if I go I will send him to you.
Lakini, nawaambieni ukweli: afadhali kwenu mimi niende zangu, maana nisipokwenda Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, basi, nitamtuma kwenu.
8 And having come, he will bring demonstration to the world, of sin, and of righteousness, and of judgment:
Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu.
9 of sin, because they do not believe on me;
Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini;
10 of righteousness, because I go away to [my] Father, and ye behold me no longer;
kuhusu uadilifu, kwa sababu naenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena;
11 of judgment, because the ruler of this world is judged.
kuhusu hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa.
12 I have yet many things to say to you, but ye cannot bear them now.
“Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili.
13 But when he is come, the Spirit of truth, he shall guide you into all the truth: for he shall not speak from himself; but whatsoever he shall hear he shall speak; and he will announce to you what is coming.
Lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atawaambieni yote atakayosikia, na atasema mambo yatakayokuwa yanakuja.
14 He shall glorify me, for he shall receive of mine and shall announce [it] to you.
Yeye atanitukuza mimi kwa kuwa atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
15 All things that the Father has are mine; on account of this I have said that he receives of mine and shall announce [it] to you.
Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu; ndiyo maana nimesema kwamba huyo Roho Mtakatifu atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
16 A little while and ye do not behold me; and again a little while and ye shall see me, [because I go away to the Father].
“Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona!”
17 [Some] of his disciples therefore said to one another, What is this he says to us, A little while and ye do not behold me; and again a little while and ye shall see me, and, Because I go away to the Father?
Hapo baadhi ya wanafunzi wake wakaulizana, “Ana maana gani anapotwambia: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona? Tena anasema: Kwa kuwa ninakwenda kwa Baba!”
18 They said therefore, What is this which he says [of] the little while? We do not know [of] what he speaks.
Basi, wakawa wanaulizana, “Ana maana gani anaposema: Bado kitambo kidogo? Hatuelewi anaongelea nini.”
19 Jesus knew therefore that they desired to demand of him, and said to them, Do ye inquire of this among yourselves that I said, A little while and ye do not behold me; and again a little while and ye shall see me?
Yesu alijua kwamba walitaka kumwuliza, basi akawaambia, “Je, mnaulizana juu ya yale niliyosema: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona?
20 Verily, verily, I say to you, that ye shall weep and lament, ye, but the world shall rejoice; and ye will be grieved, but your grief shall be turned to joy.
Nawaambieni kweli, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi: mtaona huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 A woman, when she gives birth to a child, has grief because her hour has come; but when the child is born, she no longer remembers the trouble, on account of the joy that a man has been born into the world.
Wakati mama anapojifungua huona huzuni kwa sababu saa ya maumivu imefika; lakini akisha jifungua hayakumbuki tena maumivu hayo kwa sababu ya furaha kwamba mtu amezaliwa duniani.
22 And ye now therefore have grief; but I will see you again, and your heart shall rejoice, and your joy no one takes from you.
Ninyi pia mna huzuni sasa; lakini nitawajieni tena, nanyi mtajaa furaha mioyoni mwenu, na furaha hiyo hakuna mtu atakayeiondoa kwenu.
23 And in that day ye shall demand nothing of me: verily, verily, I say to you, Whatsoever ye shall ask the Father in my name, he will give you.
Siku hiyo hamtaniomba chochote. Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu, atawapeni.
24 Hitherto ye have asked nothing in my name: ask, and ye shall receive, that your joy may be full.
Mpaka sasa hamjaomba chochote kwa jina langu. Ombeni nanyi mtapata ili furaha yenu ikamilike.
25 These things I have spoken to you in allegories; the hour is coming that I will no longer speak to you in allegories, but will declare to you openly concerning the Father.
“Nimewaambieni mambo hayo kwa mafumbo. Lakini wakati utakuja ambapo sitasema tena nanyi kwa mafumbo, bali nitawaambieni waziwazi juu ya Baba.
26 In that day ye shall ask in my name; and I say not to you that I will demand of the Father for you,
Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitamwomba Baba kwa niaba yenu;
27 for the Father himself has affection for you, because ye have had affection for me, and have believed that I came out from God.
maana yeye mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
28 I came out from the Father and have come into the world; again, I leave the world and go to the Father.
Mimi nilitoka kwa Baba, nikaja ulimwenguni; na sasa nauacha ulimwengu na kurudi kwa Baba.”
29 His disciples say to him, Lo, now thou speakest openly and utterest no allegory.
Basi, wanafunzi wake wakamwambia, “Ahaa! Sasa unasema waziwazi kabisa bila kutumia mafumbo.
30 Now we know that thou knowest all things, and hast not need that any one should demand of thee. By this we believe that thou art come from God.
Sasa tunajua kwamba wewe unajua kila kitu, na huna haja ya kuulizwa maswali na mtu yeyote; kwa hiyo tunaamini kwamba umetoka kwa Mungu.”
31 Jesus answered them, Do ye now believe?
Yesu akawajibu, “Je, mnaamini sasa?
32 Behold, [the] hour is coming, and has come, that ye shall be scattered, each to his own, and shall leave me alone; and [yet] I am not alone, for the Father is with me.
Wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo ninyi nyote mtatawanyika kila mtu kwake, nami nitaachwa peke yangu. Kumbe, lakini mimi siko peke yangu, maana Baba yu pamoja nami.
33 These things have I spoken to you that in me ye might have peace. In the world ye have tribulation; but be of good courage: I have overcome the world.
Nimewaambieni mambo haya ili mpate kuwa na amani katika kuungana nami. Ulimwenguni mtapata masumbuko; lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu!”

< John 16 >