< Job 6 >
1 And Job answered and said,
Kisha Ayubu akajibu:
2 Oh that my grief were thoroughly weighed, and all my calamity laid in the balances!
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 For now it would be heavier than the sand of the seas; therefore my words are vehement.
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For the arrows of the Almighty are within me, their poison drinketh up my spirit: the terrors of God are arrayed against me.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 Doth the wild ass bray by the grass? loweth an ox over his fodder?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 Shall that which is insipid be eaten without salt? Is there any taste in the white of an egg?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 What my soul refuseth to touch, that is as my loathsome food.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 Oh that I might have my request, and that God would grant my desire!
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 And that it would please God to crush me, that he would let loose his hand and cut me off!
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 Then should I yet have comfort; and in the pain which spareth not I would rejoice that I have not denied the words of the Holy One.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 What is my strength, that I should hope? and what is mine end, that I should have patience?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 Is my strength the strength of stones? is my flesh of brass?
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Is it not that there is no help in me, and soundness is driven away from me?
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 For him that is fainting kindness [is meet] from his friend; or he forsaketh the fear of the Almighty.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 My brethren have dealt deceitfully as a stream, as the channel of streams which pass away,
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 Which are turbid by reason of the ice, in which the snow hideth itself:
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 At the time they diminish, they are dried up; when heat affecteth them, they vanish from their place:
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 They wind about in the paths of their course, they go off into the waste and perish.
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 The caravans of Tema looked, the companies of Sheba counted on them:
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 They are ashamed at their hope; they come thither, and are confounded.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 So now ye are nothing; ye see a terrible object and are afraid.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Did I say, Bring unto me, and make me a present from your substance?
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 Or, rescue me from the hand of the oppressor, and redeem me from the hand of the violent?
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Teach me, and I will hold my tongue; and cause me to understand wherein I have erred.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 How forcible are right words! but what doth your upbraiding reprove?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 Do ye imagine to reprove words? The speeches of one that is desperate are indeed for the wind.
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Yea, ye overwhelm the fatherless, and dig [a pit] for your friend.
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 Now therefore if ye will, look upon me; and it shall be to your face if I lie.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Return, I pray you, let there be no wrong; yea, return again, my righteousness shall be in it.
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 Is there wrong in my tongue? cannot my taste discern mischievous things?
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?