< Job 40 >
1 And Jehovah answered Job and said,
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Shall he that will contend with the Almighty instruct [him]? he that reproveth God, let him answer it.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 And Job answered Jehovah and said,
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Behold, I am nought: what shall I answer thee? I will lay my hand upon my mouth.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Once have I spoken, and I will not answer; yea twice, but I will proceed no further.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 And Jehovah answered Job out of the whirlwind and said,
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Gird up now thy loins like a man: I will demand of thee, and inform thou me.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Wilt thou also annul my judgment? wilt thou condemn me that thou mayest be righteous?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Hast thou an arm like God? or canst thou thunder with a voice like him?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Deck thyself now with glory and excellency, and clothe thyself with majesty and splendour.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Cast abroad the ragings of thine anger, and look on every one that is proud, and abase him:
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Look on every one that is proud, bring him low, and tread down the wicked in their place:
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Hide them in the dust together; bind their faces in secret.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Then will I also praise thee, because thy right hand saveth thee.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 See now the behemoth, which I made with thee: he eateth grass as an ox.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Behold now, his strength is in his loins, and his force is in the muscles of his belly.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 He bendeth his tail like a cedar; the sinews of his thighs are woven together.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 His bones are tubes of bronze, his members are like bars of iron.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 He is the chief of God's ways: he that made him gave him his sword.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 For the mountains bring him forth food, where all the beasts of the field play.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 He lieth under lotus-bushes, in the covert of the reed and fen:
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Lotus-bushes cover him with their shade; the willows of the brook surround him.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Lo, the river overfloweth — he startleth not: he is confident though a Jordan break forth against his mouth.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 Shall he be taken in front? will they pierce through [his] nose in the trap?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?