< Job 36 >

1 And Elihu proceeded and said,
Elihu aliendelea na kusema,
2 Suffer me a little, and I will shew thee that I have yet words for God.
“Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
3 I will fetch my knowledge from afar, and will ascribe righteousness to my Creator.
Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
4 For truly my words shall be no falsehood: one perfect in knowledge is with thee.
Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
5 Lo, God is mighty, but despiseth not [any]; mighty in strength of understanding:
Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
6 He saveth not the wicked alive; but he doeth justice to the afflicted.
Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
7 He withdraweth not his eyes from the righteous, but with kings on the throne doth he even set them for ever; and they are exalted.
Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
8 And if, bound in fetters, they be held in cords of affliction,
Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
9 Then he sheweth them their work, and their transgressions, because they have increased.
kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
10 And he openeth their ear to discipline, and commandeth that they return from iniquity.
Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
11 If they hearken and serve [him], they shall accomplish their days in prosperity, and their years in pleasures.
Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
12 But if they hearken not, they shall pass away by the sword, and expire without knowledge.
Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
13 But the godless in heart heap up anger; they cry not when he bindeth them:
Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
14 Their soul dieth in youth, and their life is among the unclean.
Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
15 But he delivereth the afflicted in his affliction, and openeth their ear in [their] oppression.
Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
16 Even so would he have allured thee out of the jaws of distress into a broad place, where there is no straitness; and the supply of thy table [would be] full of fatness.
Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
17 But thou art full of the judgments of the wicked: judgment and justice take hold [on thee].
Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
18 Because there is wrath, [beware] lest it take thee away through chastisement: then a great ransom could not avail thee.
Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
19 Will he esteem thy riches? Not gold, nor all the resources of strength!
Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
20 Desire not the night, when peoples are cut off from their place.
Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
21 Take heed, turn not to iniquity; for this hast thou chosen rather than affliction.
Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
22 Lo, God is exalted in his power: who teacheth as he?
Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Who hath appointed him his way? or who hath said, Thou hast wrought unrighteousness?
Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
24 Remember that thou magnify his work, which men celebrate.
Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
25 All men look at it; man beholdeth [it] afar off.
Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
26 Lo, God is great, and we comprehend [him] not, neither can the number of his years be searched out.
Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
27 For he draweth up the drops of water: they distil in rain from the vapour which he formeth,
Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
28 Which the skies pour down [and] drop upon man abundantly.
ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
29 But can any understand the spreadings of the clouds, [or] the crashing of his pavilion?
Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
30 Lo, he spreadeth his light around him, and covereth the bottom of the sea.
Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
31 For with them he judgeth the peoples; he giveth food in abundance.
Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
32 [His] hands he covereth with lightning, and commandeth it where it is to strike.
Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
33 His thundering declareth concerning him; the cattle even, concerning its coming.
Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.

< Job 36 >