< Job 35 >
1 Moreover Elihu answered and said,
Aidha, Elihu aliendelea kusema,
2 Thinkest thou this to be right, that thou saidst, My righteousness is more than God's?
“Je unadhani hii ni sawa unaposema, 'Haki yangu mbele ya Mungu?
3 For thou hast asked of what profit it is unto thee: what do I gain more than if I had sinned?
Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?'
4 I will reply to thee in words, and to thy companions with thee.
Nitakujibu, wewe pamoja na marafiki zako.
5 Look unto the heavens and see; and survey the skies: they are higher than thou.
Tazama juu angani, na ulione; angalia anga, ambalo liko juu sana kuliko wewe.
6 If thou sinnest, what doest thou against him? If thy transgressions be multiplied, what doest thou unto him?
Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu? Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?
7 If thou be righteous, what givest thou to him? or what doth he receive of thy hand?
Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?
8 Thy wickedness [may affect] a man as thou [art], and thy righteousness a son of man.
Uovu wako waweza kuwaumiza mtu, kama ulivyo wewe ni mtu, na haki yako yaweza kumnufaisha mwana mwingine wa mtu.
9 By reason of the multitude of oppressions they cry; they cry out by reason of the arm of the mighty:
Watu wanalia kwasababu ya matendo mengi ya unyanyasaji; wanaomba msaada katika mikono ya watu wenye nguvu.
10 But none saith, Where is God my Maker, who giveth songs in the night,
Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi, ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,
11 Who teacheth us more than the beasts of the earth, and maketh us wiser than the fowl of the heavens?
ambaye hutufundisha sisi zaidi anavyowafundisha wanyama wa dunia, na ambaye hutufanya sisi kuwa wenye hekima kuliko ndege wa angani?
12 There they cry, and he answereth not, because of the pride of evil men.
Huko wanalia, lakini Mungu hawajibu kwasababu ya kibriu ya watu waovu.
13 Surely God will not hear vanity, neither will the Almighty regard it.
Kwa hakika Mungu hatasikia kilio cha kipumbavu; Mwenye nguvu wala hatajali.
14 Although thou sayest thou dost not see him, judgment is before him, therefore wait for him.
Ni kwa namna gani atakujibu ikiwa unasema haumwoni, na ya kwamba hoja yako iko mbele yake, na ya kuwa unamngojea yeye!
15 But now, because he hath not visited in his anger, doth not [Job] know [his] great arrogancy?
Ni kwa jinsi gani atakujibu kama unasema kwamba hamwadhibu yeyote kwa hasira, na ya kwamba hajishughulishi na kiburi cha watu.
16 For Job hath opened his mouth in vanity, and made words abundant without knowledge.
Basi Ayubu hufumbua kinywa chake tu ili kusema upumbavu; huongeza maneno bila maarifa.”