< Job 33 >

1 Howbeit, Job, I pray thee, hear mine utterances, and hearken to all my words.
Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
2 Behold now, I have opened my mouth, my tongue speaketh in my palate,
Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
3 My words shall be of the uprightness of my heart, and my lips shall utter knowledge purely.
Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
4 The Spirit of God hath made me, and the breath of the Almighty hath given me life.
Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
5 If thou canst, answer me; array [thy words] before me: take thy stand.
Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
6 Behold, before God I am as thou; I also am formed out of the clay.
Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
7 Behold, my terror shall not make thee afraid, nor my burden be heavy upon thee.
Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
8 Surely thou hast spoken in my hearing, and I have heard the voice of [thy] words: —
Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
9 I am clean without transgression; I am pure, and there is no iniquity in me;
'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
10 Lo, he findeth occasions of hostility against me, he counteth me for his enemy;
Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
11 He putteth my feet in the stocks, he marketh all my paths.
Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
12 Behold, I will answer thee in this, thou art not right; for God is greater than man.
Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
13 Why dost thou strive against him? for he giveth not account of any of his matters.
Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
14 For God speaketh once, and twice, — [and man] perceiveth it not —
Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
15 In a dream, in a vision of the night, when deep sleep falleth upon men, in slumberings upon the bed;
Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
16 Then he openeth men's ears, and sealeth their instruction,
basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
17 That he may withdraw man [from his] work, and hide pride from man.
kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
18 He keepeth back his soul from the pit, and his life from passing away by the sword.
Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
19 He is chastened also with pain upon his bed, and with constant strife in his bones;
Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
20 And his life abhorreth bread, and his soul dainty food;
ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
21 His flesh is consumed away from view, and his bones that were not seen stick out;
Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
22 And his soul draweth near to the pit, and his life to the destroyers.
Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
23 If there be a messenger with him, an interpreter, one among a thousand, to shew unto man his duty;
Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
24 Then he will be gracious unto him, and say, Deliver him from going down to the pit: I have found a ransom.
na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
25 His flesh shall be fresher than in childhood; he shall return to the days of his youth.
kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
26 He shall pray unto God, and he will receive him with favour; and he shall see his face with shoutings, and he will render unto man his righteousness.
Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
27 He will sing before men, and say, I have sinned, and perverted what was right, and it hath not been requited to me;
Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
28 He hath delivered my soul from going into the pit, and my life shall see the light.
Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
29 Lo, all these [things] worketh God twice, thrice, with man,
Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
30 To bring back his soul from the pit, that he may be enlightened with the light of the living.
kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
31 Mark well, Job, hearken unto me; be silent, and I will speak.
Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
32 If thou hast anything to say, answer me; speak, for I desire to justify thee.
Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
33 If not, hearken thou unto me; be silent, and I will teach thee wisdom.
Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”

< Job 33 >