< Job 30 >
1 But now they that are younger than I have me in derision, whose fathers I would have disdained to set with the dogs of my flock.
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 Yea, whereto [should] the strength of their hands [profit] me, [men] in whom vigour hath perished?
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 Withered up through want and hunger, they flee into waste places long since desolate and desert:
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 They gather the salt-wort among the bushes, and the roots of the broom for their food.
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 They are driven forth from among [men] — they cry after them as after a thief —
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 To dwell in gloomy gorges, in caves of the earth and the rocks:
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 They bray among the bushes; under the brambles they are gathered together:
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 Sons of fools, and sons of nameless sires, they are driven out of the land.
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 And now I am their song, yea, I am their byword.
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 They abhor me, they stand aloof from me, yea, they spare not to spit in my face.
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 For he hath loosed my cord and afflicted me; so they cast off the bridle before me.
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 At [my] right hand rise the young brood; they push away my feet, and raise up against me their pernicious ways;
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 They mar my path, they set forward my calamity, without any to help them;
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 They come in as through a wide breach: amid the confusion they roll themselves onward.
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 Terrors are turned against me; they pursue mine honour as the wind; and my welfare is passed away like a cloud.
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 And now my soul is poured out in me; days of affliction have taken hold upon me.
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 The night pierceth through my bones [and detacheth them] from me, and my gnawing pains take no rest:
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 By their great force they have become my raiment; they bind me about as the collar of my coat.
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 He hath cast me into the mire, and I have become like dust and ashes.
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 I cry unto thee, and thou answerest me not; I stand up, and thou lookest at me.
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 Thou art changed to a cruel one to me; with the strength of thy hand thou pursuest me.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 Thou liftest me up to the wind; thou causest me to be borne away, and dissolvest my substance.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 For I know that thou wilt bring me to death, and into the house of assemblage for all living.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 Indeed, no prayer [availeth] when he stretcheth out [his] hand: though they cry when he destroyeth.
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 Did not I weep for him whose days were hard? was not my soul grieved for the needy?
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 For I expected good, and there came evil; and I waited for light, but there came darkness.
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 My bowels well up, and rest not; days of affliction have confronted me.
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 I go about blackened, but not by the sun; I stand up, I cry in the congregation.
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 I am become a brother to jackals, and a companion of ostriches.
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 My skin is become black [and falleth] off me, and my bones are parched with heat.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 My harp also is [turned] to mourning, and my pipe into the voice of weepers.
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.