< Job 11 >
1 And Zophar the Naamathite answered and said,
Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
2 Should not the multitude of words be answered? and should a man of much talk be justified?
“Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
3 Should thy fictions make men hold their peace? and shouldest thou mock, and no one make [thee] ashamed?
Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
4 For thou sayest, My doctrine is pure, and I am clean in thine eyes.
Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
5 But oh that God would speak, and open his lips against thee;
Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
6 And that he would shew thee the secrets of wisdom, how that they are the double of what is realised; and know that God passeth by [much] of thine iniquity!
hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
7 Canst thou by searching find out God? canst thou find out the Almighty to perfection?
Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
8 [It is as] the heights of heaven; what wilt thou do? deeper than Sheol; what canst thou know? (Sheol )
Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol )
9 The measure thereof is longer than the earth, and broader than the sea.
Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
10 If he pass by, and shut up, and call to judgment, who can hinder him?
kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
11 For he knoweth vain men, and seeth wickedness when [man] doth not consider it;
Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
12 Yet a senseless man will make bold, though man be born [like] the foal of a wild ass.
Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
13 If thou prepare thy heart and stretch out thy hands toward him,
Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
14 If thou put far away the iniquity which is in thy hand, and let not wrong dwell in thy tents;
ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
15 Surely then shalt thou lift up thy face without spot, and thou shalt be stedfast and shalt not fear:
Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
16 For thou shalt forget misery; as waters that are passed away shalt thou remember it;
Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
17 And life shall arise brighter than noonday; though thou be enshrouded in darkness, thou shalt be as the morning,
Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
18 And thou shalt have confidence, because there shall be hope; and having searched about [thee], thou shalt take rest in safety.
Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
19 Yea, thou shalt lie down, and none shall make thee afraid; and many shall seek thy favour.
Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
20 But the eyes of the wicked shall fail, and [all] refuge shall vanish from them, and their hope [shall be] the breathing out of life.
Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.