< Jeremiah 28 >
1 And it came to pass the same year, in the beginning of the reign of Zedekiah king of Judah, in the fourth year, in the fifth month, [that] Hananiah the son of Azzur, the prophet, who was of Gibeon, spoke to me in the house of Jehovah, in the presence of the priests and of all the people, saying,
Ilitokea katika mwaka ule, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne na mwezi wa tano, Hanania mwana wa Azuri nabii, alikuwa wa Gibeoni, alisema kwangu katika nyumba ya Yahwe mbele za makuhani na watu wote. Alisema,
2 Thus speaketh Jehovah of hosts, the God of Israel, saying, I have broken the yoke of the king of Babylon.
“Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeivunja nira iliyowekwa na mfalme wa Babeli.
3 Within two full years will I bring again into this place all the vessels of Jehovah's house, that Nebuchadnezzar king of Babylon took away from this place, and carried to Babylon;
Ndani ya miaka miwili nitavirudisha katika sehemu hii vyombo vyote vya nyumba ya Yahwe ambavyo Nebukadreza mfalme wa Babeli livichukua kutoka sehemu hii na kuvisafirisha hadi Babeli.
4 and I will bring again to this place Jeconiah the son of Jehoiakim, the king of Judah, with all the captives of Judah that went to Babylon, saith Jehovah: for I will break the yoke of the king of Babylon.
Kisha nitawarudisha katika sehemu hii Yekonia mwana wa Yehotakimu, mfalme wa Yuda, na mateka wote wa Yuda ambao walipelekwa Babeli—hili ni tangazo la Yahwe—kwa maana nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.”
5 And the prophet Jeremiah spoke unto the prophet Hananiah in the presence of the priests, and in the presence of all the people that stood in the house of Jehovah.
Kwa hiyo Yeremia nabii akasema kwa Hanania nabii mbele ya makuhani na kwa watu wote waliosimama katika nyumba ya Yahwe.
6 And the prophet Jeremiah said, Amen, may Jehovah do so! may Jehovah perform thy words which thou hast prophesied, to bring again from Babylon, into this place, the vessels of Jehovah's house, and all them of the captivity!
Yeremia nabii akasema, “Yahwe afanye hivi! Yahwe ayathibitishe maneno ambayao ulitabiri na kuvirudisha katika sehemsu hii vyombo vya nyumb a ya Yahwe, na mateka wote kutoka Babeli.
7 Nevertheless, hear, I pray thee, this word which I speak in thine ears, and in the ears of all the people:
Vile vile, sikilizeni neno ambaloo ninalitangaza katika masikio yenu na katika masikio ya watu wote.
8 The prophets that have been before me and before thee of old, prophesied also concerning many countries and concerning great kingdoms, of war, and of evil, and of pestilence.
Manabii ambao walikuwepo mbele yangu na na mbele yenu muda mrefu uliopita pia walitabiri kuhusu mataifa mengi na juu ya falme kuu, kuhusu vita, njaa, na mapigo.
9 The prophet that prophesieth of peace, when the word of the prophet shall come to pass, shall be known as the prophet whom Jehovah hath really sent.
Kwa hiyo nabii anayetabiri kwamba kutakuwa na amani—kama neno lake litatimia, basi itajulikana kwamba yeye ni nabii kweli aliyetumwa na Yahwe.”
10 And the prophet Hananiah took the yoke from off the prophet Jeremiah's neck, and broke it.
Lakini Hanania nabii akaichukua nira kutoka kwenye shingo ya Yeremia na kuivunja.
11 And Hananiah spoke in the presence of all the people, saying, Thus saith Jehovah: So will I break the yoke of Nebuchadnezzar the king of Babylon within two full years from off the neck of all the nations. And the prophet Jeremiah went his way.
Kisha Hanania akanena mbele ya watu wote na kusema, “Yahwe anasema hivi: Kama hivi tu, ndani ya miaka miwili nitaivunja nira iliyowekwa na Nebukadreza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo ya kila taifa.” Kisha Yeremia nabii akaenda njia yake.
12 And the word of Jehovah came unto Jeremiah, after that the prophet Hananiah had broken the yoke from off the neck of the prophet Jeremiah, saying,
Baada ya Hanania nabii kuivunja nira kutoka kwenye shingo ya Yeremia nabii, neno la Yahwe likamjia Yeremia. likisema,
13 Go and tell Hananiah, saying, Thus saith Jehovah: Thou hast broken the yokes of wood, and thou hast made in their place yokes of iron.
Nenda na ukaseme kwa Hanania na useme, Yahwe anasema hivi: Uliivunja nira ya mbao, lakini badala yake nitafanya nira ya chuma.'
14 For thus saith Jehovah of hosts, the God of Israel: I have put a yoke of iron upon the neck of all these nations, that they may serve Nebuchadnezzar king of Babylon; and they shall serve him: and I have given him the beasts of the field also.
Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeweka nira ya chuma shingoni mwa mataifa haya yote ili wamtumikea Nebukadreza mfalme wa Babeli, na watamtumikia. Pia nimempa wanyama wa mashambani awatawale.”
15 And the prophet Jeremiah said unto the prophet Hananiah, Hear now, Hananiah: Jehovah hath not sent thee; and thou makest this people to trust in falsehood.
Kisha nabii Yeremia akamwambia Hanania nabii, “Sikiliza Hanania! Yahwe hajakutuma, bali wewe mwenyewe umewasababisha watu hawa kuamini katika uongo.
16 Therefore thus saith Jehovah: Behold, I will cast thee from off the face of the earth: this year thou shalt die, for thou hast spoken revolt against Jehovah.
Kwa hiyo Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kukutuma nje ya dunia. Mwaka huu utakufa.”
17 And the prophet Hananiah died in the same year in the seventh month.
Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, Hanania nabii akafa.