< Hebrews 13 >
1 Let brotherly love abide.
Endeleeni kupendana kidugu.
2 Be not forgetful of hospitality; for by it some have unawares entertained angels.
Msisahau kuwakaribisha wageni; maana kwa kufanya hivyo watu wengine walipata kuwakaribisha malaika bila kujua.
3 Remember prisoners, as bound with [them]; those that are evil-treated, as being yourselves also in [the] body.
Wakumbukeni wale waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao. Wakumbukeni wale wanaoteseka kana kwamba nanyi mnateseka kama wao.
4 [Let] marriage [be held] every way in honour, and the bed [be] undefiled; for fornicators and adulterers will God judge.
Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, na haki zake zitekelezwe kwa uaminifu. Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.
5 [Let your] conversation [be] without love of money, satisfied with [your] present circumstances; for he has said, I will not leave thee, neither will I forsake thee.
Msiwe watu wa kupenda fedha; toshekeni na vile vitu mlivyo navyo. Mungu mwenyewe amesema: “Sitakuacha kamwe, wala sitakutupa.”
6 So that, taking courage, we may say, The Lord [is] my helper, and I will not be afraid: what will man do unto me?
Ndiyo maana tunathubutu kusema: “Bwana ndiye msaada wangu, sitaogopa. Binadamu atanifanya nini?”
7 Remember your leaders who have spoken to you the word of God; and considering the issue of their conversation, imitate their faith.
wakumbukeni viongozi wenu waliowatangazieni ujumbe wa Mungu. Fikirieni juu ya mwenendo wao, mkaige imani yao.
8 Jesus Christ [is] the same yesterday, and to-day, and to the ages [to come]. (aiōn )
Yesu Kristo ni yuleyule, jana, leo na milele. (aiōn )
9 Be not carried away with various and strange doctrines; for [it is] good that the heart be confirmed with grace, not meats; those who have walked in which have not been profited by [them].
Msipeperushwe huku na huku kwa mafundisho tofauti ya kigeni. Neema ya Mungu ndiyo inayoimarisha roho zetu na wala si masharti juu ya chakula; masharti hayo hayakumsaidia kamwe mtu yeyote aliyeyafuata.
10 We have an altar of which they have no right to eat who serve the tabernacle;
Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaotumikia bado katika hema la Wayahudi, hawana haki ya kula vitu vyake.
11 for of those beasts whose blood is carried [as sacrifices for sin] into the [holy of] holies by the high priest, of these the bodies are burned outside the camp.
Kuhani Mkuu wa Kiyahudi huleta damu ya wanyama katika Mahali Patakatifu na kuitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi; lakini nyama za hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
12 Wherefore also Jesus, that he might sanctify the people by his own blood, suffered without the gate:
Ndiyo maana Yesu pia, kusudi apate kuwatakasa watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa na kufa nje ya mji.
13 therefore let us go forth to him without the camp, bearing his reproach:
Basi, tumwendee huko nje ya kambi tukajitwike laana yake.
14 for we have not here an abiding city, but we seek the coming one.
Maana hapa duniani hatuna mji wa kudumu; lakini tunautafuta ule unaokuja.
15 By him therefore let us offer [the] sacrifice of praise continually to God, that is, [the] fruit of [the] lips confessing his name.
Basi, kwa njia ya Yesu, tumtolee Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani sifa zinazotolewa na midomo inayoliungama jina lake.
16 But of doing good and communicating [of your substance] be not forgetful, for with such sacrifices God is well pleased.
Msisahau kutenda mema na kusaidiana, maana hizi ndizo dhabihu zinazompendeza Mungu.
17 Obey your leaders, and be submissive; for they watch over your souls as those that shall give account; that they may do this with joy, and not groaning, for this [would be] unprofitable for you.
Watiini viongozi wenu na kushika amri zao; wao huchunga roho zenu usiku na mchana, na watatoa ripoti ya utumishi wao mbele ya Mungu. Kama mkiwatii watafanya kazi zao kwa furaha, la sivyo, watazifanya kwa huzuni, na hiyo haitakuwa na faida kwenu.
18 Pray for us: for we persuade ourselves that we have a good conscience, in all things desirous to walk rightly.
Tuombeeni na sisi. Tuna hakika kwamba tunayo dhamiri safi, maana twataka kufanya lililo sawa daima.
19 But I much more beseech [you] to do this, that I may the more quickly be restored to you.
Nawasihi sana mniombee ili Mungu anirudishe kwenu upesi iwezekanavyo.
20 But the God of peace, who brought again from among [the] dead our Lord Jesus, the great shepherd of the sheep, in [the power of the] blood of [the] eternal covenant, (aiōnios )
Mungu amemfufua Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ni Mchungaji Mkuu wa kondoo kwa sababu ya kumwaga damu yake iliyothibitisha agano la milele. (aiōnios )
21 perfect you in every good work to the doing of his will, doing in you what is pleasing before him through Jesus Christ; to whom [be] glory for the ages of ages. Amen. (aiōn )
Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze mapenzi yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina. (aiōn )
22 But I beseech you, brethren, bear the word of exhortation, for it is but in few words that I have written to you.
Basi, ndugu, nawasihi mpokee kwa utulivu ujumbe huu wa kuwatieni moyo. Hii ni barua fupi tu ambayo nimewaandikieni.
23 Know that our brother Timotheus is set at liberty; with whom, if he should come soon, I will see you.
Napenda kuwajulisheni kwamba ndugu yetu Timotheo amekwisha funguliwa gerezani. Kama akifika hapa mapema, nitakuja naye nitakapokuja kwenu.
24 Salute all your leaders, and all the saints. They from Italy salute you.
Wasalimieni viongozi wenu wote pamoja na watu wa Mungu! Ndugu wa Italia wanawasalimuni.
25 Grace [be] with you all. Amen.
Tunawatakieni nyote neema ya Mungu.