< Ezekiel 26 >
1 And it came to pass in the eleventh year, on the first of the month, [that] the word of Jehovah came unto me, saying,
Mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Son of man, because Tyre hath said against Jerusalem, Aha, she is broken, the gate of the peoples! she is turned unto me: I shall be replenished [now] she is laid waste;
“Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu, ‘Aha! Lango la kwenda kwa mataifa limevunjika, nayo milango yake iko wazi mbele yangu, sasa kwa kuwa amekuwa magofu nitastawi.’
3 therefore thus saith the Lord Jehovah: Behold, I am against thee, Tyre, and will cause many nations to come up against thee, as the sea causeth its waves to come up.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi niko kinyume na wewe, ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi dhidi yako, kama bahari inayovurumisha mawimbi yake.
4 And they shall destroy the walls of Tyre, and break down her towers. And I will scrape her dust from her, and make her a bare rock.
Watavunja kuta za Tiro na kuibomoa minara yake, nitakwangua udongo wake na kuufanya mwamba mtupu.
5 She shall be [a place] for the spreading of nets in the midst of the sea; for I have spoken [it], saith the Lord Jehovah; and she shall become a spoil for the nations.
Itakuwa huko katikati ya bahari patakuwa mahali pa kutandaza nyavu za kuvulia samaki, kwa maana nimenena, asema Bwana Mwenyezi. Atakuwa nyara kwa mataifa,
6 And her daughters that are in the field shall be slain by the sword; and they shall know that I [am] Jehovah.
nayo makao yake huko bara yataangamizwa kwa upanga. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.
7 For thus saith the Lord Jehovah: Behold, I will bring from the north, against Tyre, Nebuchadrezzar king of Babylon, the king of kings, with horses, and with chariots, and with horsemen, and an assemblage, and much people.
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kutoka kaskazini nitamleta dhidi ya Tiro Mfalme Nebukadneza wa Babeli, mfalme wa wafalme, akiwa na farasi na magari ya vita, wapanda farasi na jeshi kubwa.
8 He shall slay with the sword thy daughters in the field, and he shall make forts against thee, and cast up a mound against thee, and lift up the target against thee;
Atayaharibu makao yako huko bara kwa upanga, ataweka jeshi kukuzingira, atakuzingira mpaka kwenye kuta za ngome zako na kuinua ngao zake dhidi yako.
9 and he shall set his engines of attack against thy walls, and with his spikes he shall break down thy towers.
Ataelekeza mapigo ya vyombo vyake vya kubomolea dhidi ya kuta zako na kubomoa minara yako kwa silaha zake.
10 By reason of the abundance of his horses their dust shall cover thee; thy walls shall shake at the noise of the horsemen, and of the wheels, and of the chariots, when he shall enter through thy gates, as a city is entered into, wherein is made a breach.
Farasi zake zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba utafunikwa na mavumbi watakayotimua. Kuta zako zitatikisika kwa mshindo wa farasi wa vita, magari makubwa na magari ya vita wakati aingiapo malango yako kama watu waingiao mji ambao kuta zake zimebomolewa kote.
11 With the hoofs of his horses shall he tread down all thy streets; he shall slay thy people by the sword, and the pillars of thy strength shall go down to the ground.
“Kwato za farasi zake zitakanyaga barabara zako zote, atawaua watu wako kwa upanga na nguzo zako zilizo imara zitaanguka chini.
12 And they shall make a spoil of thy riches, and make a prey of thy wares; and they shall break down thy walls, and destroy thy pleasant houses; and they shall lay thy stones and thy timber and thy dust in the midst of the waters.
Watateka utajiri wako na kuchukua nyara bidhaa zako, watazivunja kuta zako na kuzibomoa nyumba zako nzuri, watatupa baharini mawe yako, mbao zako na kifusi chako.
13 And I will cause the noise of thy songs to cease; and the sound of thy harps shall be no more heard.
Nitakomesha kelele za nyimbo zako, na uimbaji wako wa kinubi kamwe hautasikika tena.
14 And I will make thee a bare rock; thou shalt be [a place] for the spreading of nets; thou shalt be built no more: for I Jehovah have spoken [it], saith the Lord Jehovah.
Nitakufanya mwamba mtupu, nawe utakuwa mahali pa kutandazia nyavu za kuvulia samaki. Kamwe hutajengwa tena, kwa maana Mimi Bwana nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
15 Thus saith the Lord Jehovah to Tyre: Shall not the isles shake at the sound of thy fall, when the wounded groan, when the slaughter is made in the midst of thee?
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa Tiro: ‘Je, nchi za pwani hazitatetemeka kwa kishindo cha anguko lako, wakati majeruhi wanapolia kwa maumivu makali na wakati mauaji yanaendelea ndani yako?
16 And all the princes of the sea shall come down from their thrones, and lay aside their robes, and put off their broidered garments: they shall clothe themselves with trembling, they shall sit upon the ground, and shall tremble [every] moment, and be astonied because of thee.
Ndipo wakuu wote wa mataifa ya pwani watashuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuweka kando majoho yao na kuvua nguo zao zilizotariziwa. Wakiwa wamevikwa hofu kuu, wataketi chini ardhini, wakiwa wanatetemeka kila dakika na wakikustajabia.
17 And they shall take up a lamentation for thee, and say to thee, How hast thou perished, that wast inhabited from the seas, O renowned city, which wast strong in the sea, — she and her inhabitants, who caused their terror to be on all them that dwell therein!
Ndipo wao watakuombolezea na kukuambia: “‘Tazama jinsi ulivyoharibiwa, ee mji uliokuwa na sifa, wewe uliyekaliwa na mabaharia! Ulikuwa na nguvu kwenye bahari, wewe na watu wako; wote walioishi huko, uliwatia hofu kuu.
18 Now shall the isles tremble in the day of thy fall; and the isles that are in the sea shall be troubled at thy departure.
Sasa nchi za pwani zinatetemeka katika siku ya anguko lako; visiwa vilivyomo baharini vinaogopa kwa kuporomoka kwako.’
19 For thus saith the Lord Jehovah: When I shall make thee a desolate city, like the cities that are not inhabited; when I bring up the deep upon thee, and the great waters cover thee:
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitakapokufanya uwe mji wa ukiwa, kama miji isiyokaliwa tena na watu, nitakapoleta vilindi vya bahari juu yako na maji yake makuu yatakapokufunika,
20 then will I bring thee down, with them that go down to the pit, to the people of old time, and will cause thee to dwell in the lower parts of the earth, in places desolate of old, with them that go down to the pit, that thou be not inhabited; and I will set glory in the land of the living.
ndipo nitakapokushusha chini pamoja na wale washukao shimoni, kwa watu wa kale, nami nitakufanya uishi katika pande za chini za nchi kama katika magofu ya kale, pamoja na wale washukao shimoni, nawe hutarudi au kurejea kwenye makao yako katika nchi ya walio hai.
21 And I will make thee a terror, and thou shalt be no [more]; and thou shalt be sought for, and shalt never be found again, for ever, saith the Lord Jehovah.
Nitakufikisha mwisho wa kutisha wala hutakuwepo tena. Watu watakutafuta, lakini kamwe hutaonekana tena, asema Bwana Mwenyezi.”