< Exodus 36 >

1 Then wrought Bezaleel and Aholiab, and every man that was wise-hearted, in whom Jehovah had put wisdom and understanding to know how to work all manner of work of the service of the sanctuary — according to all that Jehovah had commanded.
Hivyo Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Yahweh aliye mpa ustadi na uwezo kujua jinsi ya kufanya kazi katika ujenzi wa sehemu takatifu wafanye kazi kadiri ya yote Yahweh aliyo amuru.”
2 And Moses called Bezaleel and Aholiab, and every man that was wise-hearted, in whose heart God had put wisdom, every one whose heart moved him to come to the work to do it.
Musa akamuita Bezaleli, Oholiabu, na kila mtu mwenye ujuzi ambaye Yahweh kampa ujuzi, na ambaye moyoni mwake ulichochewa kuja na kufanya kazi.
3 And they took from Moses every heave-offering that the children of Israel had brought for the work of the service of the sanctuary, to make it. And they still brought him voluntary offerings morning by morning.
Walipokea kutoka kwa Musa sadaka zote ambazo Waisraeli walizo leta kwa ujenzi ya sehemu takatifu. Watu walikuwa bado wanaleta sadaka za hiari kila asubui kwa Musa.
4 And all the wise men that wrought all the work of the sanctuary came, every man from his work which they wrought,
Hivyo watu wote walikuwa na ujuzi walikuwa wakifanya kazi sehemu takatifu walikuja kutoka kwenye kazi walikuwa wakifanya.
5 and spoke to Moses, saying, The people bring much more than enough for the service of the work that Jehovah commanded to be done.
Wachonga mawe walimwabia Musa, “Watu wanaleta zaidi sana ya yanayo itajika kufanya kazi Yahweh aliyo tuamuru.”
6 Then Moses gave commandment, and they caused it to be proclaimed through the camp, saying, Let neither man nor woman make any more work for the heave-offering of the sanctuary! So the people were restrained from bringing;
Hivyo Musa akaamuru mtu yeyote asilete tena kwa ujenzi wa sehemu takatifu. Kisha watu wakaacha kuleta hivi vitu.
7 for the work they had was sufficient for all the work to do it, and it was too much.
Walikuwa na zaidi ya vitu vya ujenzi.
8 And every wise-hearted man among those that wrought the work of the tabernacle made ten curtains of twined byssus, and blue, and purple, and scarlet: [with] cherubim of artistic work did he make them.
Hivyo wachonga mawe miongoni mwao wakajenga lile hema la kuabudia kwa mapazia kumi yaliyo jengwa kitamba kizuri na buluu, zambarau, na sufu nyekundu kwa aina ya kerubi. Hii ni kazi ya Bezaleli, mjenzi mwenye ujuzi sana.
9 The length of one curtain was twenty-eight cubits, and the breadth of one curtain four cubits — one measure for all the curtains.
Urefu wa kila pazia ulikuwa mikono ishirini na nane, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa vyote hivyo vilikuwa na kipimo kimoja.
10 And he coupled five of the curtains one to another, and [the other] five curtains coupled he one to another.
Bezaleli akaunganisha vitambaa vitano pamoja, na vile vitambaa vingine vitano akaviunganisha pamoja.
11 And he made loops of blue on the edge of one curtain at the edge of the coupling; he did likewise in the edge of the outermost curtain in the other coupling.
Kisha akafanya vitanzi vya uzi wa bluu kwenye upindo wa kitambaa kilicho mahali pa kuungania. Akafanya vivyo hivyo kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pale pengine pa kuungania.
12 He made fifty loops in one curtain, and he made fifty loops at the end of the curtain that was in the other coupling: the loops were opposite to one another.
Akafanya vitanzi hamsini kwenye kitambaa kimoja, akafanya vitanzi hamsini kwenye mwisho wa kitambaa kilichokuwa mahali pale pengine pa kuungania, vitanzi hivyo vikiwa vinaelekeana.
13 And he made fifty clasps of gold, and coupled the curtains together with the clasps, so that the tabernacle became one.
Mwishowe akafanya kulabu hamsini za dhahabu na kuviunganisha vitambaa hivyo pamoja kwa kulabu hizo, hivi kwamba hiyo ikawa maskani moja.
14 And he made curtains of goats' [hair] for the tent over the tabernacle: eleven curtains did he make them.
Bezaleli akafanya vitambaa vya mahema vya manyoya ya mbuzi kwa ajili ya hema lililo juu ya maskani. Vitambaa kumi na moja ndivyo alivyofanyiza.
15 The length of one curtain was thirty cubits, and four cubits the breadth of one curtain — one measure for the eleven curtains.
Urefu wa kila kitambaa ulikuwa mikono thelathini, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa hivyo kumi na moja vilikuwa na kipimo kimoja.
16 And he coupled five of the curtains by themselves, and six of the curtains by themselves.
Kisha akaunganisha vitambaa vitano pamoja na vile vitambaa vingine sita pamoja.
17 And he made fifty loops on the edge of the outermost curtain in the coupling, and fifty loops made he on the edge of the curtain in the other coupling.
Kisha akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pa kuungania, naye akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kile kitambaa kingine kilichoungana nacho.
18 And he made fifty clasps of copper to couple the tent, that it might be one.
Bezaleli akafanya kulabu hamsini za shaba kwa ajili ya kuliunganisha hilo hema pamoja liwe kipande kimoja.
19 And he made a covering for the tent [of] rams' skins dyed red, and a covering of badgers' skins above [that].
Naye akafanya kifuniko cha hema kutokana na ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko kutokana na ngozi za sili, upande wa juu.
20 And he made the boards for the tabernacle of acacia-wood, standing up;
Bezaleli akafanya viunzi vya mbao vya hema ya kukutani kutokana na mbao za mshita.
21 ten cubits the length of the boards, and one cubit and a half the breadth of one board;
Urefu wa kiunzi ulikuwa mikono kumi, nao upana wa kila kiunzi ulikuwa mkono mmoja na nusu.
22 two tenons in one board, connected one with the other: thus did he make for all the boards of the tabernacle.
Kila kiunzi kilikuwa na ndimi mbili zilizounganishwa. Hivyo ndivyo alivyofanya viunzi vyote vya maskani.
23 And he made the boards for the tabernacle: twenty boards for the south side southward;
Basi akafanya viunzi vya maskani, viunzi ishirini kwa ajili ya upande kuelekea kusini.
24 and he made forty bases of silver under the twenty boards, two bases under one board, for its two tenons, and two bases under another board for its two tenons.
Bezaleli akafanya vikalio arobaini vya fedha viwe chini ya vile viunzi ishirini, vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja pamoja na ndimi zake mbili na vikalio vingine viwili chini ya kiunzi kingine pamoja na ndimi zake mbili.
25 And for the other side of the tabernacle, on the side toward the north, he made twenty boards,
Na kwa ajili ya ule upande mwingine wa maskani, upande wa kaskazini, akafanya viunzi ishirini
26 and their forty bases of silver, two bases under one board, and two bases under another board.
na vikalio vyake arobaini vya fedha. Vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja na vikalio viwili chini ya kiunzi kingine
27 And at the rear of the tabernacle, westward, he made six boards;
Na kwa ajili ya zile pande za nyuma za maskani kuelekea magharibi akafanya viunzi sita.
28 and he made two boards for the corners of the tabernacle at the rear;
Naye akafanya viunzi viwili vya pembeni ya maskani kwenye pande zake mbili za nyuma
29 and they were joined beneath, and were coupled together at the top thereof into one ring: thus he did to both of them in both the corners;
Hizi zilikuwa pacha upande wa chini, lakini juu ya kila moja kwenye pete ya kwanza. Hivyo ndivyo alivyoifanya yote miwili, ile miimo ya pembeni.
30 and there were eight boards, and their silver bases: sixteen bases, under every board two bases.
Basi vikajumlika kuwa viunzi vinane na vikalio vyake kumi na sita vya fedha, vikalio viwili kando ya vikalio viwili chini ya kila kiunzi.
31 — And he made bars of acacia-wood: five for the boards of the one side of the tabernacle,
Bezaleli akafanya miti ya mshita, mitano kwa ajili ya viunzi vya upande mmoja wa maskani,
32 and five bars for the boards of the other side of the tabernacle, and five bars for the boards of the tabernacle at the rear, westward.
na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya upande ule mwingine wa maskani na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya maskani kwa ajili ya zile pande mbili za nyuma za magharibi.
33 And he made the middle bar in the midst of the boards reach from one end to the other.
Kisha akafanya mti wa katikati upitie katikati ya vile viunzi toka mwisho mmoja mpaka ule mwingine.
34 And he overlaid the boards with gold; and made their rings of gold [as] receptacles for the bars; and overlaid the bars with gold.
Naye akavifunika vile viunzi kwa dhahabu, akafanyiza pete zake za dhahabu ziwe vitegemezo kwa ajili ya ile miti, akaifunika ile miti kwa dhahabu.
35 And he made the veil of blue, and purple, and scarlet, and twined byssus: of artistic work he made it [with] cherubim.
Bezaleli akafanya pazia, la uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kalitia makerubi kwa kazi ya mjenzi.
36 And he made four pillars of acacia[-wood] for it, and overlaid them with gold; their hooks were of gold; and he cast for them four bases of silver.
Kisha akalifanyia nguzo nne za mshita na kuzifunika kwa dhahabu, vibanio vyake vikiwa vya dhahabu, na kutengeneza vikalio vinne vya fedha kwa ajili yake.
37 And he made a curtain for the entrance of the tent of blue, and purple, and scarlet, and twined byssus, of embroidery;
Naye akafanya kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema kutokana na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kazi ya mfumaji.
38 and its five pillars with their hooks; and he overlaid their capitals and their connecting-rods with gold; and their five bases were of copper.
Pia akafanya na nguzo zake tano na vibanio vyake. Naye akavifunika vilele vyake na viungo vyake kwa dhahabu, lakini vile vikalio vyake vitano vilikuwa vya shaba.

< Exodus 36 >