< Exodus 17 >
1 And all the assembly of the children of Israel journeyed from the wilderness of Sin, according to their journeys, at the command of Jehovah; and they encamped in Rephidim; and there was no water for the people to drink.
Jamii yote ya Israeli ili safiri kutoka nyikani ya Sinu, wakifuata maelekezo ya Yahweh. Walieka kambi Refidimu, lakini hapakuwa na maji ya watu kunywa.
2 And the people contended with Moses, and said, Give us water, that we may drink! And Moses said to them, Why do ye dispute with me? Why do ye tempt Jehovah?
Hivyo watu wakamlaumu Musa kwa hali yao na kusema, “Tupe maji ya kunywa.” Musa akasema, “Kwanini mnagombana na mimi? Kwanini mnajaribu Yahweh?”
3 And the people thirsted there for water; and the people murmured against Moses, and said, Why is it that thou hast brought us up out of Egypt, to kill us and our children and our cattle with thirst?
Watu walikuwa na kiu sana, na waka mlalamikia Musa. Wakasema, “Kwanini umetutoa Misri? Ili utuue sisi na watoto wetu na mifugo yetu kwa kiu?”
4 And Moses cried to Jehovah, saying, What shall I do with this people? Yet a little, and they will stone me!
Kisha Musa akamlilia Yahweh, “Nini ni fanya kwa hawa watu? Wako tayari ata kunipiga mawe.”
5 And Jehovah said to Moses, Go on before the people, and take with thee of the elders of Israel, and thy staff with which thou didst smite the river, take in thy hand, and go.
Yahweh akamwambia Musa, “Nenda mbele yao, na uchukuwe baadhi ya wazee wa Israeli. Chukuwa gongo ulilo piga nalo mto, na uende.
6 Behold, I will stand before thee there upon the rock on Horeb; and thou shalt strike the rock, and there shall come water out of it, that the people may drink. And Moses did so before the eyes of the elders of Israel.
Nitasimama mbele yako pale kwenye mwamba wa Horebu, na utaupiga mwamba. Maji yatatoka ya watu kunywa.” Kisha Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Israeli.
7 And he called the name of the place Massah, and Meribah, because of the contention of the children of Israel, and because they had tempted Jehovah, saying, Is Jehovah among us, or not?
Aliita ile sehemu Massa na Meriba kwasababu ya malalamishi ya Waisraeli, na kwasababu walimjaribu Bwana kwa kusema, “Je Yahweh yupo miongoni mwetu au hapana?”
8 And Amalek came and fought with Israel in Rephidim.
Kisha jeshi la watu wa Ameleki wakaja na kushambulia Israeli huko Refidimu.
9 And Moses said to Joshua, Choose us men, and go out, fight with Amalek; to-morrow I will stand on the top of the hill with the staff of God in my hand.
Hivyo Musa akamwambia Yoshua, “Chagau wanaume kadha na uende nje. Pigana na Ameleki. Kesho nitasimama juu ya kilima na gongo la Mungu mkononi mwangu.”
10 And Joshua did as Moses had said to him, to fight with Amalek; and Moses, Aaron and Hur went up to the top of the hill.
Hivyo Yoshua akapigana na Ameleki kama Musa alivyo elekeza, wakati Musa, Aruni, na Huri walienda juu ya kilima.
11 And it came to pass when Moses raised his hand, that Israel prevailed; and when he let down his hand, Amalek prevailed.
Wakati Musa alipo kuwa ameshikilia mikono yake juu, Israeli ilikuwa yashinda; alipo acha mikono yake ipumzike, Ameleki alianza kushinda.
12 And Moses' hands were heavy; then they took a stone, and put [it] under him, and he sat on it; and Aaron and Hur supported his hands, one on this side, and one on that side; and his hands were steady until the going down of the sun.
Mikono ya Musa alipo kuwa mizito, Aruni na Huri walichukuwa jiwe na kuweka chini yake alikalie. Muda huo huo, Aruni na Huri walinyanyua mikono yake juu, mtu mmoja upande mmoja, na mtu mmoja upande mwingine. Hivyo mikono ya Musa ilishikiliwa tuli mpaka jua lilipo zama.
13 And Joshua broke the power of Amalek and his people with the edge of the sword.
Hivyo Yoshua akawashinda watu wa Ameleki kwa upanga.
14 And Jehovah said to Moses, Write this [for] a memorial in the book, and rehearse [it] in the ears of Joshua, that I will utterly blot out the remembrance of Amalek from under the heavens.
Yahweh akamwambia Musa, “Andika haya kwenye kitabu na umsomee Yoshua, kwasababu nitaondoa kumbukumbu ya Ameleki kutoka chini ya mbingu.”
15 And Moses built an altar, and called the name of it Jehovah-nissi.
Kisha Musa akajenga madhabahu na kuiita “Yahweh ni bendera yangu.”
16 And he said, For the hand is on the throne of Jah; Jehovah will have war with Amalek from generation to generation!
Alisema, “Kwa kuwa mkono ulinyanyuliwa juu kuelekea kiti cha enzi cha Yahweh - kwamba Yahweh ata fanya vita na Ameleki vizazi na vizazi.”