< 2 Samuel 11 >
1 And it came to pass, at the return of the year, at the time when kings go forth, that David sent Joab, and his servants with him, and all Israel; and they laid waste the [land of the] children of Ammon, and besieged Rabbah. But David abode at Jerusalem.
Ikawa wakati wa majira ya kipupwe, wakati ambapo kwa kawaida wafalme huenda vitani, Daudi akamtuma Yoabu, mtumishi wake, na jeshi lote la Israeli. Wakaliaribu jeshi la Amoni na kuuhusuru Raba. Lakini Daudi akakaa Yerusalemu.
2 And it came to pass at evening time that David arose from off his couch, and walked upon the roof of the king's house; and from the roof he saw a woman bathing, and the woman was very beautiful;
Hivyo ikawa siku moja wakati wa jioni Daudi akaamka kutoka kitandani na akatembea katika dari la kasri. Akiwa pale akamwona mwanamke aliyekuwa akioga, mwanamke yule alikuwa mzuri sana kwa mwonekano.
3 and David sent and inquired after the woman. And one said, Is not this Bathsheba, the daughter of Eliam, the wife of Urijah the Hittite?
Hivyo Daudi akatuma na kuuliza watu waliomfahamu yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, “Je huyu siye Bathsheba, binti Eliamu, naye si mke wa Uria mhiti?
4 And David sent messengers, and took her; and she came in to him, and he lay with her; and she had purified herself from her uncleanness; and she returned to her house.
Daudi akatuma wajumbe nao wakamchukua; akaja kwake, na akalala naye(kwani ndo alikuwa amejitakasa kutoka siku zake). Kisha akarudi nyumbani kwake.
5 And the woman conceived, and sent and told David, and said, I am with child.
Mwanamke akawa mjamzito, naye akatuma na kumwambia Daudi; akasema, “mimi ni mjamzito.”
6 And David sent to Joab [saying], Send me Urijah the Hittite. And Joab sent Urijah to David.
Kisha Daudi akatuma watu kwa Yoabu kusema, “Umtume kwangu Uria mhiti.” Hivyo Yoabu akamtuma Uria kwa Daudi.
7 And when Urijah had come to him, David asked how Joab prospered, and how the people prospered, and how the war prospered.
Uria alipofika, Daudi akamuuliza hali ya Yoabu. Jinsi jeshi lilivyokuwa likiendelea, na jinsi vita vilivyokuwa vinaendelea.
8 And David said to Urijah, Go down to thy house and wash thy feet. And Urijah departed out of the king's house, and there followed him presents from the king.
Daudi akamwambia Uria, “Shuka nyumbani kwako, unawe miguu yako. “Hivyo Uria akaondoka katika kasri la mfalme, mfalme akamtumia zawadi kwa Uria.
9 And Urijah slept at the entrance of the king's house with all the servants of his lord, and went not down to his house.
Lakini Uria akalala pamoja na watumishi wa bwana wake katika lango la kasri, wala hakushuka nyumbani kwake.
10 And they had told David saying, Urijah did not go down to his house; and David said to Urijah, Art thou not come from a journey? why didst thou not go down to thy house?
Daudi alipoambiwa, “Uria hakushuka nyumbani kwake,” akamwambia Uria, Je haukutoka safarini? Kwa nini haukushuka nyumbani kwako?”
11 And Urijah said to David, The ark, and Israel, and Judah abide in booths; and my lord Joab, and the servants of my lord, are encamped in the open fields: shall I then go into my house, to eat and to drink, and to lie with my wife? [As] thou livest, and [as] thy soul liveth, I will not do this thing.
Uria akamjibu Daudi, “Sanduku, na Israeli na Yuda wamo kwenye mahema, na Yoabu na watumishi wa bwana wangu wamepiga hema uwandani. Jinsi gani basi mimi naweza kwenda nyumbani kwangu kula kunywa na kulala na mke wangu? kwa hakika kama uishivyo, sitafanya hivyo.
12 And David said to Urijah, Abide here to-day also, and to-morrow I will let thee depart. And Urijah abode in Jerusalem that day and the morrow.
Hivyo Daudi akamwambia Uria, “Ukae leo pia, kesho nitakuacha uende.” Kwa hiyo uria akakaa Yerusalemu siku hiyo na iliyofuata.
13 And David invited him, and he ate and drank before him; and he made him drunk. And in the evening he went out to lie on his couch with the servants of his lord, but did not go down to his house.
Daudi alipomwita, alikula na kunywa pamoja naye, Daudi akamfanya alewe. Wakati wa jioni Uria akaenda kulala kitandani pake pamoja na watumish wa bwana wake; hakushuka nyumbani kwake.
14 And it came to pass in the morning, that David wrote a letter to Joab, and sent it by Urijah.
Hivyo asubuhi Daudi akamwandikia Yoabu barua, naye akaituma kwa mkono wa Uria.
15 And he wrote in the letter saying, Set Urijah in the front of the thickest fight, and withdraw from him, that he may be smitten and die.
Ndani ya barua Daudi aliandika hivi, “Mweke Uria mbele ya vita vikali sana, na kisha, mmwache, ili apigwe na afe.
16 And it came to pass as Joab watched the city, that he assigned Urijah to a place where he knew that the valiant men were.
Hivyo Yoabu alipoona mji ukizingirwa, alimweka Uria katika sehemu aliyojua askari adui wenye nguvu wangekuwa wakipigana.
17 And the men of the city went out and fought with Joab; and there fell some of the people, of the servants of David; and Urijah the Hittite died also.
Wakati watu wa mji walipotoka na kupigana dhidi ya jeshi la Yoabu, baadhi ya askari wa Daudi wakaanguka, na Uria Mhiti pia akauwawa.
18 Then Joab sent and told David all the matters of the war;
Wakati Yoabu alipotuma neno kwa mfalme kuhusu hali ya vita,
19 and charged the messenger, saying, When thou hast ended telling the matters of the war to the king,
alimwagiza mjumbe, kusema, “Utakapomaliza kumwambia mfalme kuhusu hali ya vita,
20 and if so be that the king's wrath arise, and he say to thee, Why did ye go so near to the city to fight? did ye not know that they would shoot from the wall?
yawezekana mfalme akakasirika, naye akakwambia, 'Kwa nini mlipigana na mji kwa karibu hivyo, hamkujua kwamba wangeweza kushambulia kutokea ukutani?
21 Who smote Abimelech the son of Jerubbesheth? did not a woman cast the upper stone of a handmill from the wall, that he died in Thebez? why did ye go near the wall? — then say thou, Thy servant Urijah the Hittite is dead also.
Ni nani aliyemwua Abimeleki mwana wa Yerubeshethi? Siye mwanamke aliyerusha jiwe la kusagia juu yake kutoka ukutani, hata akafa huko Thebesi? Kwanini basi mliukaribia ukuta jinsi hiyo? Nawe umjibu, 'Uria mtumishi wako amekufa pia.”
22 And the messenger went; and he came and told David all that Joab had sent him for.
Hivyo mjumbe akaondoka na kwenda kwa Daudi akamwambia kila jambo ambalo Yoabu alimtuma kusema.
23 And the messenger said to David, The men prevailed against us, and came out against us into the field, and we were upon them as far as the entrance of the gate.
Na mjumbe akamwambia Daudi, “Mwanzoni adui walikuwa na nguvu kuliko sisi; walitukabili uwandani, lakini tukawarudisha nyuma kwenye maingilio ya lango.
24 And the shooters shot from upon the wall against thy servants; and some of the king's servants are dead, and thy servant Urijah the Hittite is dead also.
Na wapiga mishale wao wakawarushia watumishi wako kutoka ukutani, na baadhi ya watumishi wa mfalme wameuawa, na mtumishi wako Uria mhiti pia ameuawa.”
25 Then David said to the messenger, Thus shalt thou say to Joab: Let not this thing displease thee, for the sword devours one as well as another: make thy battle strong against the city, and overthrow it; — and encourage him.
Kisha Daudi akamwambia mjumbe, “Mwambie hivi Yoabu, 'Usiruhusu jamba hili likuhuzunishe, kwa maana upanga huangamiza huyu kama uangamizavyo na mwingine. Vifanye vita vyako kuwa vyenye nguvu zaidi dhidi ya mji, na uuteke.' Mtie moyo Yoabu.”
26 And the wife of Urijah heard that Urijah her husband was dead, and she mourned for her husband.
Hivyo mke Uria aliposikia kwamba mme wake amekufa, akaomboleza sana kwa ajili yake.
27 And when the mourning was past, David sent and fetched her to his house, and she became his wife, and bore him a son. But the thing that David had done was evil in the sight of Jehovah.
Huzuni yake ilipoisha, Daudi akatuma na kumchukua kwake katika kasri lake, naye akawa mkewe na akamzalia mwana. Lakini alichokifanya Daudi hakikumpendeza Yahwe.