< 2 Corinthians 6 >
1 But [as] fellow-workmen, we also beseech that ye receive not the grace of God in vain:
Basi, tukiwa wafanyakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msikubali ile neema mliyopokea kutoka kwa Mungu ipotee bure.
2 (for he says, I have listened to thee in an accepted time, and I have helped thee in a day of salvation: behold, now [is the] well-accepted time; behold, now [the] day of salvation: )
Mungu asema hivi: “Wakati wa kufaa nimekusikiliza, wakati wa wokovu nikakusaidia.” Basi, sasa ndio wakati wa kufaa, sasa ndiyo siku ya wokovu!
3 giving no manner of offence in anything, that the ministry be not blamed;
Kusudi tusiwe na lawama yoyote katika utumishi wetu, hatupendi kumwekea mtu yeyote kizuio chochote.
4 but in everything commending ourselves as God's ministers, in much endurance, in afflictions, in necessities, in straits,
Badala yake, tunajionyesha kuwa kweli watumishi wa Mungu kwa kila kitu: kwa uvumilivu mwingi wakati wa mateso, shida na taabu.
5 in stripes, in prisons, in riots, in labours, in watchings, in fastings,
Tumepigwa, tumetiwa gerezani na kuzomewa hadharani; tumefanya kazi tukachoka; tumekesha na kukaa bila kula.
6 in pureness, in knowledge, in longsuffering, in kindness, in [the] Holy Spirit, in love unfeigned,
Tunajionyesha kuwa watumishi wa Mungu kwa usafi wa moyo, elimu, uvumilivu na wema; kwa Roho Mtakatifu, kwa upendo usio na unafiki,
7 in [the] word of truth, in [the] power of God; through the arms of righteousness on the right hand and left,
kwa ujumbe wa kweli na kwa nguvu ya Mungu. Uadilifu ndiyo silaha yetu upande wa kulia na upande wa kushoto.
8 through glory and dishonour, through evil report and good report: as deceivers, and true;
Tuko tayari kupata heshima na kudharauliwa, kulaumiwa na kusifiwa. Twadhaniwa kuwa waongo, kumbe twasema kweli;
9 as unknown, and well known; as dying, and behold, we live; as disciplined, and not put to death;
kama wasiojulikana, kumbe twajulikana kwa wote, kama waliokufa, lakini mwonavyo, sisi ni wazima kabisa.
10 as grieved, but always rejoicing; as poor, but enriching many; as having nothing, and possessing all things.
Ingawa tumeadhibiwa, hatukuuawa; ingawa tunayo huzuni, twafurahi daima; ingawa tu maskini hohehahe, lakini twatajirisha watu wengi; twaonekana kuwa watu tusio na chochote, kumbe tuna kila kitu.
11 Our mouth is opened to you, Corinthians, our heart is expanded.
Ndugu Wakorintho, tumezungumza nanyi kwa unyofu; mioyo yetu iko wazi kabisa.
12 Ye are not straitened in us, but ye are straitened in your affections;
Kama mnaona kuna kizuizi chochote kile, kizuizi hicho kiko kwenu ninyi wenyewe, na si kwa upande wetu.
13 but for an answering recompense, (I speak as to children, ) let your heart also expand itself.
Sasa nasema nanyi kama watoto wangu, wekeni mioyo yenu wazi kama nasi tulivyofanya.
14 Be not diversely yoked with unbelievers; for what participation [is there] between righteousness and lawlessness? or what fellowship of light with darkness?
Msiambatane na watu wasioamini. Je, wema na uovu vyapatana kweli? Mwanga na giza vyawezaje kukaa pamoja?
15 and what consent of Christ with Beliar, or what part for a believer along with an unbeliever?
Kristo anawezaje kupatana na Shetani? Muumini ana uhusiano gani na asiyeamini?
16 and what agreement of God's temple with idols? for ye are [the] living God's temple; according as God has said, I will dwell among them, and walk among [them]; and I will be their God, and they shall be to me a people.
Hekalu la Mungu lina uhusiano gani na sanamu za uongo? Maana sisi ni hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu mwenyewe alivyosema: “Nitafanya makao yangu kwao, na kuishi kati yao; Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
17 Wherefore come out from the midst of them, and be separated, saith [the] Lord, and touch not [what is] unclean, and I will receive you;
Kwa hiyo Bwana asema pia: “Ondokeni kati yao, mkajitenge nao, msiguse kitu najisi, nami nitawapokea.
18 and I will be to you for a Father, and ye shall be to me for sons and daughters, saith [the] Lord Almighty.
Mimi nitakuwa Baba yenu, nanyi mtakuwa watoto wangu, waume kwa wake, asema Bwana Mwenye Uwezo.”