< 1 Samuel 4 >

1 And what Samuel had said happened to all Israel. And Israel went out against the Philistines to battle, and encamped beside Eben-ezer; and the Philistines encamped in Aphek.
Nalo neno la Samweli likaja kwa Israeli yote. Basi Waisraeli walitoka kwenda kupigana dhidi ya Wafilisti. Waisraeli wakapiga kambi huko Ebenezeri, nao Wafilisti wakapiga kambi huko Afeki.
2 And the Philistines put themselves in array against Israel; and the battle spread, and Israel was routed before the Philistines; and they slew in battle array in the field about four thousand men.
Wafilisti wakapanga safu za majeshi yao kupambana na Israeli, wakati vita vilipoenea, Israeli wakashindwa na Wafilisti, ambao waliwaua askari wa Israeli wapatao 4,000 kwenye uwanja wa vita.
3 And the people came into the camp; and the elders of Israel said, Why has Jehovah smitten us to-day before the Philistines? Let us fetch ourselves the ark of the covenant of Jehovah out of Shiloh, that it may come among us, and save us out of the hand of our enemies.
Askari waliporudi kambini, wazee wa Israeli wakawauliza, “Kwa nini Bwana ameruhusu leo tushindwe mbele ya Wafilisti? Tuleteni Sanduku la Agano la Bwana kutoka Shilo, ili lipate kwenda pamoja nasi, na kutuokoa kutoka mikono ya adui zetu.”
4 So the people sent to Shiloh, and they brought from thence the ark of the covenant of Jehovah of hosts, who sitteth between the cherubim; and the two sons of Eli, Hophni and Phinehas, were there by the ark of the covenant of God.
Hivyo wakawatuma watu huko Shilo, nao wakalichukua Sanduku la Agano la Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekaa kwenye kiti chake cha enzi kati ya makerubi. Nao wale wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, walikuwako huko pamoja na Sanduku la Agano la Mungu.
5 And it came to pass when the ark of the covenant of Jehovah came into the camp, that all Israel shouted with a great shout, so that the earth shook.
Wakati Sanduku la Agano la Bwana lilikuja kambini, Waisraeli wote wakapiga kelele kwa sauti kuu hata ardhi ikatikisika.
6 And the Philistines heard the noise of the shout, and said, What is the noise of this great shout in the camp of the Hebrews? And they understood that the ark of Jehovah had come into the camp.
Wafilisti waliposikia makelele wakauliza, “Ni nini makelele haya yote katika kambi ya Waebrania?” Walipofahamu kuwa Sanduku la Bwana limekuja kambini,
7 And the Philistines were afraid, for they said, God is come into the camp. And they said, Woe unto us! for there has not been such a thing heretofore.
Wafilisti wakaogopa, wakasema, “Mungu amekuja kambini, ole wetu. Halijatokea jambo kama hili tangu hapo.
8 Woe unto us! who shall deliver us out of the hand of these mighty gods? these are the gods that smote the Egyptians with every plague in the wilderness.
Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa kutoka mikononi mwa miungu hii yenye nguvu? Ni miungu ile iliyowapiga Wamisri kwa mapigo ya aina zote huko jangwani.
9 Shew yourselves valiant and be men, ye Philistines, that ye may not have to be servants to the Hebrews, as they have been servants to you: be men, and fight.
Tuweni hodari, enyi Wafilisti! Tuweni wanaume, la sivyo mtakuwa watumwa wa Waebrania, kama wao walivyokuwa kwenu. Kuweni wanaume, mpigane!”
10 And the Philistines fought, and Israel was routed, and they fled every man to his tent; and there was a very great slaughter, and there fell of Israel thirty thousand footmen.
Basi Wafilisti wakapigana, nao Waisraeli wakashindwa na kila mtu akakimbilia hemani mwake. Mauaji yalikuwa makubwa sana, Israeli wakapoteza askari 30,000 waendao kwa miguu.
11 And the ark of God was taken; and the two sons of Eli, Hophni and Phinehas, died.
Sanduku la Mungu likatekwa, na hao wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, wakauawa.
12 And there ran a man of Benjamin out of the battle, and came to Shiloh the same day, with his clothes rent and with earth upon his head.
Siku ile ile mtu mmoja wa kabila la Benyamini akakimbia kutoka kwenye uwanja wa vita na kwenda Shilo, nguo zake zikiwa zimeraruka na akiwa na mavumbi kichwani mwake.
13 And when he came, behold, Eli was sitting upon the seat by the way-side watching; for his heart trembled for the ark of God. And the man came to tell it in the city, and all the city cried out.
Alipofika, Eli alikuwa ameketi juu ya kiti chake kando ya barabara akiangalia, kwa sababu moyo wake ulikuwa na hofu kwa ajili ya Sanduku la Mungu. Mtu yule alipoingia mjini na kueleza kilichokuwa kimetokea, mji wote ukalia.
14 And Eli heard the noise of the crying, and said, What is the noise of this tumult? And the man came hastily, and told Eli.
Eli akasikia kelele za kilio, naye akauliza, “Ni nini maana ya makelele haya?” Yule mtu akafanya haraka kwenda kwa Eli,
15 Now Eli was ninety-eight years old; and his eyes were set, that he could not see.
wakati huu Eli alikuwa na miaka tisini na minane nayo macho yake yalikuwa yamepofuka na hakuweza kuona.
16 And the man said to Eli, I am he that came out of the battle, and I have fled to-day out of the battle. And he said, What has taken place, my son?
Akamwambia Eli, “Mimi nimetoka vitani sasa hivi, nimekimbia kutoka huko leo hii.” Eli akamuuliza, “Je, mwanangu, ni nini kimetokea huko?”
17 And the messenger answered and said, Israel has fled before the Philistines, and there has been also a great slaughter among the people, and thy two sons also, Hophni and Phinehas, are dead, and the ark of God is taken.
Yule mtu aliyeleta habari akajibu, “Israeli amekimbia mbele ya Wafilisti, nalo jeshi limepata hasara kubwa. Pia wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa, na Sanduku la Mungu limetekwa.”
18 And it came to pass, when he mentioned the ark of God, that he fell from off the seat backward by the side of the gate, and his neck broke, and he died; for the man was old, and heavy. And he had judged Israel forty years.
Mara alipotaja Sanduku la Mungu, Eli alianguka kutoka kwenye kiti chake kwa nyuma kando ya lango. Shingo yake ikavunjika naye akafa, kwa kuwa alikuwa mzee tena mzito. Alikuwa amewaongoza Israeli kwa miaka arobaini.
19 And his daughter-in-law, Phinehas' wife, was with child, near to be delivered; and when she heard the tidings that the ark of God was taken, and that her father-in-law and her husband were dead, she bowed herself and travailed; for her pains came upon her.
Mkwewe, mke wa Finehasi, alikuwa mjamzito na karibu wakati wa kujifungua. Aliposikia habari kwamba Sanduku la Mungu limetekwa na ya kuwa baba mkwe wake na mumewe wamekufa, akapata utungu naye akajifungua lakini akazidiwa na utungu.
20 And as she was dying, the women that stood by her said, Fear not; for thou hast borne a son. But she did not answer, neither did she take it to heart.
Alipokuwa akifa, wanawake waliokuwa wanamhudumia wakamwambia, “Usikate tamaa, umemzaa mwana.” Lakini hakujibu wala kuweka maanani.
21 And she named the child Ichabod, saying, The glory is departed from Israel; because the ark of God was taken, and because of her father-in-law and her husband.
Alimwita yule mtoto Ikabodi, akisema, “Utukufu umeondoka katika Israeli,” kwa sababu ya kutekwa kwa Sanduku la Mungu na vifo vya baba mkwe na mumewe.
22 And she said, The glory is departed from Israel, for the ark of God is taken.
Akasema, “Utukufu umeondoka katika Israeli, kwa kuwa Sanduku la Mungu limetekwa.”

< 1 Samuel 4 >