< 1 Samuel 23 >
1 And they told David, saying, Behold, the Philistines fight against Keilah, and they rob the threshing-floors.
Wakamwambia Daudi, “Tazama, Wafilisti wanaupiga Keila na wanapora nafaka inayopurwa.”
2 And David inquired of Jehovah, saying, Shall I go and smite these Philistines? And Jehovah said to David, Go and smite the Philistines, and save Keilah.
Hivyo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, na akamuuliza,” Je, niondoke niwapige hawa Wafilisti? BWANA akamwambia Daudi, “Nenda ukawapige Wafilisti na kuokoa Keila.”
3 But David's men said to him, Behold, we are afraid here in Judah; how much more then if we go to Keilah against the armies of the Philistines?
Daudi akaambiwa na watu wake, “Angalia, hapa Yuda tunaogopa. Je, si zaidi sana kama tutaenda Keila kupambana na majeshi ya Wafilisti?”
4 And David inquired of Jehovah yet again. And Jehovah answered him and said, Arise, go down to Keilah; for I will give the Philistines into thy hand.
Ndipo Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya msaada, bado tena, BWANA akamjibu, “Amka, uteremke hadi Keila. Maana nitakupatia ushindi dhidi ya Wafilisti.”
5 And David and his men went to Keilah, and fought against the Philistines, and brought away their cattle, and smote them with a great slaughter. So David saved the inhabitants of Keilah.
Daudi na watu wake wakaenda Keila na kupigana na Wafilisti. Wakahamisha ng'ombe wao na kuwapiga kwa mauaji makubwa mno. Hivyo Daudi akawaokoa wenyeji wa Keila.
6 And it came to pass, when Abiathar the son of Ahimelech fled to David to Keilah, he came down with an ephod in his hand.
Abiathari mwana wa Ahimeleki alipokuwa amekimbilia kwa Daudi huko Keila, alibeba naivera mkononi mwake.
7 And it was told Saul that David had come to Keilah. Then Saul said, God has cast him off into my hand; for he is shut in, by entering into a city that has gates and bars.
Sauli aliambiwa kwamba Daudi amekwenda Keila. Sauli akasema, “Mungu amemweka mkononi mwangu. Bila shaka amefungiwa ndani kwa sababu ameingia katika mji ulio na malango na makomeo.”
8 And Saul summoned all the people to war, to go down to Keilah, to besiege David and his men.
Sauli akayaita majeshi yake yote kwa ajili ya vita, waende hadi Keila, wamteke Daudi na watu wake.
9 And when David knew that Saul devised mischief against him, he said to Abiathar the priest, Bring the ephod.
Daudi alijua kwamba Sauli alikuwa anapanga njama za kumdhuru yeye. Ndipo akamwambia kuhani Abiathari kuhani, “Ulete hapa naivera.”
10 Then said David, Jehovah, God of Israel, thy servant hath heard for certain that Saul seeketh to come to Keilah, to destroy the city for my sake.
Kisha Daudi akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, mtumishi wako hakika amesikia kwamba Sauli anatafuta namna ya kuja Keila, ili auteketeze mji kwa ajili yangu.
11 Will the citizens of Keilah deliver me up into his hand? will Saul come down, as thy servant hath heard? Jehovah, God of Israel, I beseech thee, tell thy servant. And Jehovah said, He will come down.
Je, watu wa Keila watanisalimisha mkononi mwake? Je, Sauli atashuka hadi huko, kama mtumishi wako alivyosikia? BWANA, Mungu wa Israeli, nakusihi, tafadhali mwambie mtumishi wako. “BWANA akasema, “Atakuja huko.”
12 And David said, Will the citizens of Keilah deliver up me and my men into the hand of Saul? And Jehovah said, They will deliver [thee] up.
Kisha Daudi akauliza, “Je, watu wa Keila watanisalimisha mimi na watu wangu katika mkono wa Sauli?” BWANA akasema, “Watu hao watawasalimisha kwao.”
13 Then David and his men, about six hundred, arose and departed out of Keilah, and went whithersoever they could go. And it was told Saul that David had escaped from Keilah, and he forbore to go forth.
Kisha Daudi na watu wake, waliokuwa kama mia sita, walitoka na kwenda mbali na Keila, na wakazunguka kila sehemu. Kisha Sauli akaambiwa kwamba Daudi ametoroka kutoka Keila, hivyo akasitisha kumfuatia.
14 And David abode in the wilderness in strongholds, and abode in the mountain in the wilderness of Ziph. And Saul sought him every day, but God did not give him into his hand.
Daudi alikaa ngomeni katika jangwa, kwenye nchi ya milima katika jangwa la Zifu. Kila siku Sauli alimtafuta, lakini Mungu hakumweka mkononi mwake.
15 And David saw that Saul had come out to seek his life; and David was in the wilderness of Ziph in a wood.
Daudi aliona kwamba Sauli amejitokeza kuangamiza maisha yake; basi Daudi alikuwa katika jjangwa la Zifu huko Horeshi.
16 And Jonathan Saul's son arose, and went to David into the wood, and strengthened his hand in God.
Kisha Yonathani, mwana wa Sauli, akaamuka akaenda kwa Daudi huko Horshi, naye akamtia moyo amtumainie Mungu.
17 And he said to him, Fear not; for the hand of Saul my father will not find thee; and thou shalt be king over Israel, and I shall be next to thee; and that also Saul my father knows.
Akamwambia, “Usiogope. Kwa maana mkono wa baba yangu Sauli hautakupata. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, na mimi nitakuwa msaidizi wako. Baba yangu Sauli pia anajua hivyo.”
18 And they two made a covenant before Jehovah; and David abode in the wood, and Jonathan went to his house.
Basi wote wawili wakafanya agano mbele za BWANA. Kisha Daudi alibaki Horeshi, na Yonathani akaenda nyumbani.
19 And the Ziphites came up to Saul to Gibeah, saying, Does not David hide himself with us in strongholds in the wood, on the hill of Hachilah, which is on the south of the waste?
Nndipo Wazifi wakamwendea Sauli huko Gibea wakisema, “Je, Daudi hakujificha kati yetu kwenye ngome huko Horeshi, juu ya mlima wa Hakila, ulioko kusini mwa Yeshimoni?
20 And now, O king, come down according to all the desire of thy soul to come down; and it will be for us to deliver him up into the king's hand.
Basi uje, mfalme! Kulingana na matakwa yako, uje! Kazi yetu itakuwa kumtia katika mkono wa mfalme.”
21 And Saul said, Blessed be ye of Jehovah; for ye have compassion upon me.
Sauli akasema, “Mbarikiwe na BWANA. Kwa sababu mmenihurumia.
22 Go, I pray you, make yet more sure, and know and see his place where his track is, who has seen him there; for it is told me that he deals very subtilly.
Nendeni, mhakikishe sawasawa. Tafuteni na kujua maficho yake yako wapi na ni nani amemwona huko. Nimeambiwa kwamba yeye ni mjanja sana.
23 And see, and ascertain all the lurking-places where he hides himself, and come ye again to me with sure information, that I may go with you; and it shall come to pass, if he be in the land, that I will search him out throughout the thousands of Judah.
Kwa hiyo chunguzeni, mjue sehemu zote anakojificha. Baadaye rudini kwangu mkiwa na taarifa kamili, na kisha nitaongozana nanyi. Ikiwa yupo katika nchi, nitamtafuta kutoka miongoni mwa elfu zote za Yuda.”
24 And they arose and went to Ziph before Saul; but David and his men were in the wilderness of Maon, in the plain on the south of the waste.
Ndipo wakaamka na kwenda hadi Zifu mbele ya Sauli. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa katika jangwa la Maoni, huko Araba upande wa kusini mwa Yeshimoni.
25 And Saul and his men went to seek [him]. And they told David; and he came down from the rock, and abode in the wilderness of Maon. And Saul heard [that], and he pursued after David in the wilderness of Maon.
Sauli na watu wake wakaenda kumtafuta Daudi. Na Daudi akaambiwa habari hiyo, hivyo akateremka hadi kwenye mlima wa miamba na akakaa katika jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hivyo, akamfukuza Daudi katika Jangwa la Maoni.
26 And Saul went on this side of the mountain, and David and his men on that side of the mountain; and David made haste to get away from Saul; and Saul and his men sought to surround David and his men to take them.
Sauli akaenda akawa upande mmoja wa mlima, na Daudi na watu wake walikuwa wakienda upande mwingine wa mlima. Daudi kwa haraka akatoweka akae mbali na Sauli. Kwa sababu Sauli na watu wake walikuwa wakimzunguka Daudi na watu wake wawakamate,
27 But there came a messenger to Saul, saying, Haste thee and come; for the Philistines have made a raid against the land.
mjumbe mmoja akaja kwa Sauli na kusema, “Njoo, harakisha maana Wafilisti wamepanga uvamizi juu ya nchi.”
28 And Saul returned from pursuing after David, and went against the Philistines; therefore they called that place Sela-hammahlekoth.
Kwa hiyo Sauli akarudi asimfuatie Daudi na akaenda kupambana na Wafilisti. Kwa hiyo sehemu ile iliitwa Mwamba wa Maficho.
29 And David went up from thence, and abode in the strongholds of Engedi.
Daudi akapanda kutoka huko na kukaa katika ngome ya Engedi.