< 1 Kings 7 >

1 And Solomon was thirteen years building his own house; and he finished all his house.
Ilimchukua Sulemani miaka kumi na tatu kujenga ikulu yake.
2 And he built the house of the forest of Lebanon; its length was a hundred cubits, and its breadth fifty cubits, and its height thirty cubits, upon four rows of cedar-pillars, with cedar-beams upon the pillars;
Aliijenga ikulu iliyoitwa mwitu wa Lebanoni. Urefu wake ulikuwa mita 46, na upanawake ulikuwa mita 23, na kimo chake kilikuwa mita 14. Nayo ilikuwa na safu nne ya nguzo za mierezi na mithili ya mwerezi juu ya nguzo.
3 and it was covered with cedar above upon the side-chambers, which were on forty-five pillars, fifteen in a row.
Paa la ikulu lilikuwa la mwerezi ambalo lilikaa juu ya mihimili. Mihili hiyo ilikuwa imeshikiliwa na nguzo. Kulikuwa na mihimili arobaini na tano, ambayo ilikuwa katika safu kumi na tano.
4 And there were cross-beams in three rows, and window was against window in three ranks.
Nayo mihimili ilikuwa safu tatu, na kila dirisha lilikabili dirisha lingine katika madaraja matatu.
5 And all the doors and posts were square, with an architrave; and window was against window in three ranks.
Milango yote na miimo ilitengenezwa kwa mraba, na madirisha yalikuwa yakikabiliana katika madaraja matatu
6 And he made the porch of pillars; its length was fifty cubits, and its breadth thirty cubits; and there was a porch in front of them; and there were pillars, and steps in front of them.
Akatengeneza baraza lenye uerfu wa mita 23 na upana wa mita 14. Mbele yake kulikuwa na ukumbi ulioezekwa.
7 And he made the porch for the throne where he judged, the porch of judgment; and it was covered with cedar from floor to floor.
Sulemani akajenga baraza yenye kiti cha enzi ambacho alitolea hukumu ya haki. Nayo ilikuwa imeezekwa kwa mwerezi kutoka sakafu moja hadi nyingine.
8 And his house where he dwelt had another court within the porch, which was of the like work. And he made, like to this porch, a house for Pharaoh's daughter, whom Solomon had taken.
Nyumba ya Sulemani ambayo alikusudia kuishi, katika behewa nyingine ndani ya sehemu ya chini ya ikulu, ilitengenezwa kwa kazi hiyo hiyo. Pia alimjengea binti wa Farao nyumba kama hii, ambaye alikuwa mke wake
9 All these [buildings] were of costly stones, hewn stones, according to the measures, sawed with saws, within and without, even from the foundation to the coping, and on the outside as far as the great court.
Majengo haya yalipmbwa kwa vitu vya thamaini, mawe ya thamani, yaliyochongwa na kukatwa kwa msimeno kufuata vipimo sahihi na kulainishwa pande zote. Mawe ya namna hii ndiyo yale yaliyotumika kuanzia kwenye msingi hadi juu, pia na nje hadi kwenye baraza.
10 And the foundations were of costly stones, great stones, stones of ten cubits and stones of eight cubits.
Msingi ulijengwa kwa mawe makubwa sana na ya thamani yenye urefu wa mita 3. 7 na mengine mita 4. 8.
11 And above were costly stones, hewn stones, according to the measures, and cedar.
Kwa juu ilipambwa kwa, mawe ya thamani yaliyochongwa sawa sawa kwa msimeno na kwa mihimili ya mierezi.
12 And the great court round about had three rows of hewn stones, and a row of cedar-beams; and so it was for the inner court of the house of Jehovah, and the porch of the house.
Na behewa kubwa iliyokuwa ikizunguka ikulu ilikuwa na safu tatu za mawe yaliyokatwa na safu moja ya mihimili ya mierezi kama ilivyo kwenye baraza la ndani la hekalu la BWANA na ule ukumbi wa hekalu.
13 And king Solomon sent and fetched Hiram out of Tyre.
Mfalme Sulemani alituma watu kumleta Huramu kutoka Tiro.
14 He was a widow's son of the tribe of Naphtali, and his father was a man of Tyre, a worker in brass; and he was full of wisdom and understanding and knowledge, to do all kinds of works in brass. And he came to king Solomon, and made all his work.
Huramu alikuwa mwana wa mjane wa kabila ya Naftali; baba yake alikuwa mtu wa Tiro, mfua shaba. Huramu alikuwa mwingi wa hekima na ufahamu na stadi za kufanya kazi kubwa za shaba. Aliletwa kwa mfalme ili kufanya kazi zilizohusiana na shaba kwa mfalme.
15 And he formed the two pillars of brass; the height of one pillar was eighteen cubits, and a line of twelve cubits encompassed the second pillar.
Huramu alizilemba zile nguzo mbili za shaba, kila moja ilikuwa na kimo cha mita 8. 3 na mzingo wa mita 5. 5.
16 And he made two capitals of molten brass, to set upon the tops of the pillars; the height of the one capital was five cubits, and the height of the other capital was five cubits;
Akatengeneza taji mbili za shaba za kuwekwa juu ya zile nguzo. Kimo cha kila taji ilikuwa mita 2. 3.
17 [and] nets of checker-work, wreaths of chain-work, for the capitals which were upon the top of the pillars; seven for the one capital and seven for the other capital.
Kulikuwa na nyavu za kuwa kama kazi ya kusuka, na masongo ya mikufu, kwa ajili ya kuvipamba vile vichwa vya nguzo, nayo yailikuwa saba kwa kila kichwa.
18 And he made pomegranates, namely two rows round about upon the one network, to cover the capitals that were upon the top of the pillars; and so he did for the other capital.
Kwa hiyo Huramu akafanya safu mbili za komamanga kuzunguka vile vichwa vya nguzo ili kuvipamba vile vichwa.
19 And the capitals that were upon the top of the pillars were of lily-work [as] in the porch, four cubits.
Zile taji kwenye vile vichwa vya nguzo za ukumbi zilikuwa zimepambwa kwa maua, yenye vimo vya mita 1. 8.
20 And the capitals upon the two pillars, above also, close to the enlargement which was behind the network, had two hundred pomegranates in rows round about, [also] on the other capital.
Hizo taji kwenye hizo nguzo mbili kwenye vichwa vyake, karibu yake kulikuwa na makomamanga mia mbili yote yakiwa kwenye safu.
21 And he set up the pillars for the porch of the temple; and he set up the right pillar, and called its name Jachin; and he set up the left pillar, and called its name Boaz.
Alisimamisha nguzo kwenye ukumbi wa hekalu. Ile nguzo ya kuume akaipa jina la Yakini, na ile ya kushoto akaipa jina la Boazi.
22 And upon the top of the pillars was lily-work; and the work of the pillars was finished.
Na juu ya zile nguzo kulikuwa na mapambo kama maua. Hivyo ndivyo zile nguzo zilivyotengenezwa.
23 And he made the sea, molten, ten cubits from brim to brim, round all about; and its height was five cubits; and a line of thirty cubits encompassed it round about.
Tena akafanya bahari ya kusubu ya, yenye mita 2. 3 kutoka ukingo hadi ukingo, kimo chake kilikuwa mita 4. 6, mziingo wake ulikuwa mita 13. 7.
24 And under the brim of it round about there were colocynths, encompassing it, ten in a cubit enclosing the sea round about; two rows of colocynths, cast when it was cast.
Na chini ya ile bahari kulikuwa na vibuyu vilivyoizunguka, vilikuwa vibuyu kumi na nane katika kila mita, vilivyowekwa katika kila hicho kipande wakati bahari inapokuwa kalibu.
25 It stood upon twelve oxen, three looking toward the north, and three looking toward the west, and three looking toward the south, and three looking toward the east; and the sea was above upon them, and all their hinder parts were inward.
Bahari ikakaa juu ya makisai kumi na mbili, tatu, zilitazama kaskazini, tatu zikitazama magharibi, tatu zikitazama kusini na tatu zikitazama kaskazini. Ile bahari iliwekwa juu yao, na pande zao zote za nyuma zilikuwa ndani.
26 And its thickness was a hand-breadth, and its brim was like the work of the brim of a cup, with lily-blossoms; it held two thousand baths.
Bahari ilikuwa nene kama upana wa mkono, na ukingo wake ulikuwakama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi huingia bathi elfu mbili za maji.
27 And he made ten bases of brass: four cubits was the length of one base, and the breadth four cubits, and the height three cubits.
Huramu akatengeneza makalio kumi ya shaba. Kila kalio lilkuwa na urefu wa mita 1. 8, upana wa mita 1. 8, na kimo cha mita 1. 3.
28 And the work of the bases was this: they had panels, and the panels were between the fillets.
Hivi ndivyo kazi za makalio zilivyofanywa. Yalikuwa na papi ambazo zilikaa kati kati ya vipandio,
29 And on the panels that were between the fillets were lions, oxen and cherubim; and over the fillets there was a base above; and beneath the lions and oxen were garlands of festoon-work.
na juu ya papi na vipandio kulikuwa na simba, makisai, na makerubi. Chini na juu simba kulikuwa na masongo ya kazi ya kufuliwa.
30 And every base had four wheels of brass, and axles of brass; and on its four corners were shoulder-pieces: under the laver were shoulder-pieces molten, behind every garland.
Kila kalio lilikuwa na magurudumu ya shaba na vipini, na pande zake nne na miguu yake minne ilikuwa na mataruma chini ya birika. Chini ya birika yalikuweko mataruma ya kusubu yenye masongo katika kila upande.
31 And the mouth of it within the crown and above was a cubit; and its mouth was rounded, [as] the work of the base, a cubit and a half; and also upon its mouth was sculpture; but their panels were square, not round.
Na kinywa chake kilikuwa cha kuviringana, chenye upana wa sentimita araobaini na sita, na ile taji ilikuwa na sentimita ishirini na tatu. Na kinywa chake kilikuwa na nakshi, na papi zake zilikuwa za mraba, na wala siyo za mvringo.
32 And the four wheels were under the panels; and the supports of the wheels were in the base; and the height of a wheel was a cubit and half a cubit.
Yale magurudumu mawili yalikuwa chini ya papi, na mikono ya magurudumu yalikuwa ndani ya makalio. Kimo cha yale magurudumu kilikuwa sentimeta sitini na tisa.
33 And the work of the wheels was like the work of a chariot wheel: their supports, and their rims, and their spokes and their naves were all molten.
Yale magurudumu yalikuwa kama ya gari. Mikono yake, na maduara, matindi yake, na vipande vya ndani vyote vilikuwa vya kusubu.
34 And there were four shoulder-pieces to the four corners of one base; of the base itself were its shoulder-pieces.
Kulikuwa na mataruma manne katika pande zake nne za makalio, yaliyokuwa yameshikamanishwa na kalio lenyewe.
35 And in the top of the base there was a circular elevation of half a cubit round about; and on the top of the base its stays and its panels were of the same.
Juu ya makalio kulikuwa na duara yenye kina cha sentimita ishirini na tatu, na juu ya makalio mashikio yake na papi zake zikiwa zimeshikamanishwa.
36 And he engraved on the plates of its stays and on its panels cherubim, lions and palm-trees, according to the space upon each; and garlands were round about.
Juu ya mabamba na papi zake Huramu akachora makerubi, simba, na mitende ambayo ilifunika nafasi ya juu, nayo ilikuwa imezungukwa na masongo.
37 After this [manner] he made the ten bases: all of them had one casting, one measure, one form.
Alitengeneza makalio kumi kwa jinsi hii. Yote yalikuwa yametengenezwa kwa kufanana, na yalikuwa ya vipimo sawa, na sura inayofanana.
38 And he made ten lavers of brass: one laver contained forty baths; every laver was four cubits; upon every one of the ten bases one laver.
Huramu akatengeneza birika kumi za shaba. Birika moja liliweza kubeba bathi arobaini za maji. Kila birika lilikuwa mita 1. 8 toka birika moja hadi jingine na kulikuwa na birika moja katika kila kalio kati ya yale kumi.
39 And he put the bases, five on the right side of the house, and five on the left side of the house; and he set the sea on the right side of the house eastward, over against the south.
Alitengeneza makalio tano upande wa kusini unaoelekea upande wa hekalu. Akatengeneza bahari katika upande wa mashariki, ukielekea upande wa kusini wa hekalu.
40 And Hiram made the lavers, and the shovels, and the bowls. So Hiram ended doing all the work that he made for king Solomon [for] the house of Jehovah:
Huramu akatengeneza birika na koleo na besini la kunyunyizia. Kisha akamaliza kazi yote aliyofanya kwa mfalme Sulemani katika hekalu la BWANA:
41 two pillars, and the globes of the capitals that were on the top of the pillars, two; and the two networks, to cover the two globes of the capitals which were on the top of the pillars;
Zile nguzo mbili, na lile besini lakawa kama taji ambalo lilikuwa juu ya zile nguzo, na nyavu mbili za mapambo za kufunika zile besini mbili za kuwa kama taji zilizokuwa juu ya nguzo.
42 and the four hundred pomegranates for the two networks, two rows of pomegranates for one network, to cover the two globes of the capitals which were upon the pillars;
Kisha akatengeneza makomamanga mia nne kwa ajili ya zile nyavu mbili za mapambo: safu mbili za makomamamanga kwa kila kazi ya nyavu kwa ajili ya kufunikia zile besini mbili kama taji iliyo juu ya nguzo,
43 and the ten bases, and the ten lavers on the bases;
yale makalio kumi, na birika kumi kwenye makalio.
44 and one sea, and the twelve oxen under the sea;
Akatengeneza bahari na makisai kumi chini yake;
45 and the pots, and the shovels, and the bowls. And all these things, which Hiram made king Solomon for the house of Jehovah, were of bright brass.
na masufuria, koleo, birika na vyombo vingine vyote. Huramu akivitengeneza kwa shaba iliyosuguliwa, kwa ajili ya mfalme Sulemani, na kawa ajili ya hekalu la BWANA.
46 In the plain of the Jordan did the king cast them, in the clay-ground between Succoth and Zaretan.
Mfalme alivisubu katika uwanda wa Yorodani, katika udongo mfinyanzi kati ya Sukoti na Zarethani.
47 And Solomon left all the vessels [unweighed] from their exceeding number; the weight of the brass was not ascertained.
Sulemani hakuvipima vyombo vyote kwa sababu vilikuwa vingi mno kuvipima, na kwa sababu uzito wa shaba ulikuwa hauwezi kupimwa.
48 And Solomon made all the vessels that were [in] the house of Jehovah: the golden altar; and the table of gold, whereon was the shewbread;
Sulemani akatengeneza mapambo yote yaliyokuwa kwenye hekalu la BWANA kwa kutumia dhahabu: Ile madhabahu ya dhahabu na ile meza ambayo iliwekwa mikate ya wonyesho.
49 and the candlesticks of pure gold, five on the right, and five on the left, before the oracle; and the flowers, and the lamps, and the tongs of gold,
Vile vinara vya dhahabu, ambavyo vitano vilikuwa upande wa kulia na vitano mkono wa kushoto, mbele ya chumba cha ndani, vilikuwa vya dhahabu safi, na maua, na taa na koleo zilikuwa za dhahabu.
50 and the basons, and the knives, and the bowls, and the cups, and the censers of pure gold; and the hinges of gold, for the folding-doors of the inner house, the most holy place, [and] for the doors of the house, of the temple.
Vile vikombe, na makasi, mabakuri, na vijiko, na vyetezo vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi. na bawaba za dhahabu za milango ya ndani, ambazoo ndio mahali patakatifu sana, na milango ya ukumbi mkubwa, vyote vilitengenezwa kwa dhahabu.
51 And all the work was finished that king Solomon made for the house of Jehovah. And Solomon brought in the things that David his father had dedicated; the silver and the gold and the vessels he put among the treasures of the house of Jehovah.
Kwa njia hii, kazi yote ambayo mfalme Sulemani alifanya kwa ajili ya hekalu ilimalizika. Kwa Sulemani akaviingiza ndani yake vitu vile vilivyokuwa vimewekwa wakfu na Daudi, baba yake, na fedha na dhahabu, na mapambo, na vile vya ndani ya hazina ya BWANA.

< 1 Kings 7 >