< 1 Chronicles 6 >

1 The sons of Levi: Gershom, Kohath, and Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
2 And the sons of Kohath: Amram, Jizhar, and Hebron, and Uzziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
3 And the children of Amram: Aaron, and Moses, and Miriam. And the sons of Aaron: Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar.
Wana wa Amramu walikuwa Aruni, Musa, Miriamu. Wana wa Aruni walikuwa Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.
4 Eleazar begot Phinehas; Phinehas begot Abishua,
Eleazari akawa baba wa Finehasi, na Finehasi akawa baba wa Abishua.
5 and Abishua begot Bukki, and Bukki begot Uzzi,
Abishua akawa baba wa Buki, na Buki akawa baba wa Uzi.
6 and Uzzi begot Zerahiah, and Zerahiah begot Meraioth;
Uzi akawa baba wa Zerahia, na Zerahia akawa baba wa Meraioti.
7 Meraioth begot Amariah, and Amariah begot Ahitub,
Meraioti akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
8 and Ahitub begot Zadok, and Zadok begot Ahimaaz,
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Ahimazi.
9 and Ahimaaz begot Azariah, and Azariah begot Johanan,
Ahimazi akawa baba wa Azaria, na Azaria akawa baba wa Yohanani.
10 and Johanan begot Azariah (he is it that exercised the priesthood in the house that Solomon built in Jerusalem);
Yohanani akawa baba wa Azaria, aliye hudumu katika hekalu alilo lijenga Sulemani ndaniya Yerusalemu.
11 and Azariah begot Amariah, and Amariah begot Ahitub,
Azaria akawa baba wa Amaria, na Amaria akawa baba wa Ahitubi.
12 and Ahitub begot Zadok, and Zadok begot Shallum,
Ahitubi akawa baba wa Zadoki, na Zadoki akawa baba wa Shalumu.
13 and Shallum begot Hilkijah, and Hilkijah begot Azariah,
Shalumu akawa baba wa Hilikia, na Hilikia akawa baba wa Azaria.
14 and Azariah begot Seraiah, and Seraiah begot Jehozadak,
Azaria akawa baba Seraia, na Seraia akawa baba wa Yehozadaki.
15 and Jehozadak went away, when Jehovah carried away Judah and Jerusalem by the hand of Nebuchadnezzar.
Yehozadaki akaenda matekani Yahweh alipo wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.
16 The sons of Levi: Gershom, Kohath, and Merari.
Wana wa Levi walikuwa Gerishomu, Kohathi, na Merari.
17 And these are the names of the sons of Gershom: Libni and Shimei.
Wana wa Gerishomu walikuwa Libini na Shimei.
18 And the sons of Kohath: Amram, and Jizhar, and Hebron, and Uzziel.
Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
19 The sons of Merari: Mahli and Mushi. And these are the families of Levi according to their fathers.
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Hawa walikuwa koo za Walawi kwa familia za baba zao.
20 Of Gershom: Libni his son, Jahath his son, Zimmah his son,
Uzao wa Gerishomu ulianza na mwanae Libini. Mwana wa Libini alikuwa Jahathi. Mwanae alikuwa Zima.
21 Joah his son, Iddo his son, Zerah his son, Jeathrai his son.
Mwanae alikuwa Yoa. Mwanae alikuwa alikuwa Ido. Mwanae alikuwa Zera. Mwanae alikuwa Yeatherai.
22 The sons of Kohath: Amminadab his son, Korah his son, Assir his son,
Uzao wa Kohathi ulianza na mwanae Aminadabu. Mwanae alikuwa Kora. Mwanae alikuwa Asiri.
23 Elkanah his son, and Ebiasaph his son, and Assir his son,
Mwanae alikuwa Elikana. Mwanae alikuwa Ebiasa. Mwanae alikuwa Asiri.
24 Tahath his son, Uriel his son, Uzziah his son, and Saul his son.
Mwanae alikuwa Tahathi. Mwanae alikuwa Urieli. Mwanae alikuwa uzia. Mwanae alikuwa Shauli.
25 And the sons of Elkanah: Amasai and Ahimoth.
Wana wa Elikana walikuwa Amasai, Ahimothi, na Elikana.
26 Elkanah, — the sons of Elkanah: Zophai his son, and Nahath his son,
Mwana wa huyu Elikana wa pili alikuwa Zofai. Mwanae alikuwa Nahathi.
27 Eliab his son, Jeroham his son, Elkanah his son.
Mwanae alikuwa Eliabu. Mwanae alikuwa Yehoramu. Mwanae alikuwa Elikana.
28 And the sons of Samuel: the firstborn Vashni and Abijah.
Wana wa Samwali walikuwa mzaliwa wa kwanza, Yoeli, na Abija, wa pili.
29 The sons of Merari: Mahli; Libni his son, Shimei his son, Uzza his son,
Mwana wa Merari alikuwa Mahili. Mwanae alikuwa Libini.
30 Shimea his son, Haggijah his son, Asaiah his son.
Mwanae alikuwa Shimei. Mwanae alikuwa Uza. Mwanae alikuwa Shimea. Mwanae alikuwa Hagia. Mwana alikuwa Asaia.
31 And these are they whom David set over the service of song in the house of Jehovah after that the ark was in rest.
Haya ndio majina ya wanaume ambao Daudi waliwaeka kusimamia muziki katika nyumba ya Yahweh, baada ya sanduku kuja hapo.
32 And they ministered before the tabernacle of the tent of meeting with singing, until Solomon had built the house of Jehovah in Jerusalem; and they attended to their office according to their order.
Walitumika kwa kuimba mbele ya hema, hema la kukutania, mpaka Sulemani alipo jenga nyumba ya Yahweh ndani ya Yerusalemu. Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa.
33 And these are they that attended, and their sons: Of the sons of the Kohathites: Heman the singer, the son of Joel, the son of Samuel,
Hawa walitumika pamoja na wana wao. Katika makabila ya Wakohathi alitoka Hemani mwana muziki. Babu zake walikuwa hawa, kurudi nyuma ya wakati: Hemani alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Samweli.
34 the son of Elkanah, the son of Jeroham, the son of Eliel, the son of Toah,
Samweli alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Yerohamu. Yerohamu alikuwa mwana wa Elieli. Elieli alikuwa mwana wa Toa.
35 the son of Zuph, the son of Elkanah, the son of Mahath, the son of Amasai,
Toa alikuwa mwana wa Zufi. Zufi alikuwa mwana wa Elikana. Elikana alikuwa mwana wa Mahathi. Mahathi alikuwa mwana wa Amasai. Amasai alikuwa mwana wa Elikana.
36 the son of Elkanah, the son of Joel, the son of Azariah, the son of Zephaniah,
Elikana alikuwa mwana wa Yoeli. Yoeli alikuwa mwana wa Azaria. Azaria alikuwa mwana wa Zefania.
37 the son of Tahath, the son of Assir, the son of Ebiasaph, the son of Korah,
Zefania alikuwa mwana wa Tahathi. Tahathi alikuwa mwana wa Asiri. Asiri alikuwa mwana wa Ebiasa. Ebiasa alikuwa mwana wa Kora.
38 the son of Jizhar, the son of Kohath, the son of Levi, the son of Israel.
Kora alikuwa mwana wa Izhari. Izhari alikuwa mwana wa Kohathi. Kohathi alikuwa mwana wa Levi. Levi alikuwa mwana wa Israeli.
39 And his brother Asaph, who stood on his right hand: Asaph, the son of Berechiah, the son of Shimea,
Msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliye simama mkono wake wa kuume. Asafu alikuwa mwana Berekia. Berekia alikuwa mwana wa Shimea.
40 the son of Michael, the son of Baaseiah, the son of Malchijah,
Shimea alikuwa mwana Mikaeli. Mikaeli alikuwa mwana wa Baaseia. Baaseia alikuwa mwana wa Malikiya.
41 the son of Ethni, the son of Zerah, the son of Adaiah,
Malikiya alikuwa mwana wa Ethini. Ethini alikuwa mwana wa Zera. Zera alikuwa mwana wa Adaia.
42 the son of Ethan, the son of Zimmah, the son of Shimei,
Adaia alikuwa mwana wa Ethani. Ethani alikuwa mwana wa Zima. Zima alikuwa mwana wa Shimei.
43 the son of Jahath, the son of Gershom, the son of Levi.
Shimei alikuwa mwana wa Yahathi. Yahathi alikuwa mwana wa Gerishomu. Gerishomu alikuwa mwana wa Levi.
44 And their brethren the sons of Merari were on the left hand: Ethan the son of Kishi, the son of Abdi, the son of Malluch,
Upande wa mkono wa koshoto wa Hemani walikuwa wasaidizi wake wana wa Merari. Alikuwa Ethani mwana wa Kishi. Kishi alikuwa mwana wa Abdi. Abdi alikuwa mwana wa Maluki.
45 the son of Hashabiah, the son of Amaziah, the son of Hilkijah,
Maluki alikuwa mwana wa Hashabia. Hashabia alikuwa mwana wa Amazia. Amazia alikuwa mwana wa Hilikia.
46 the son of Amzi, the son of Bani, the son of Shemer,
Hilikia alikuwa mwana wa Amzi. Amzi alikuwa mwana wa Bani. Bani alikuwa mwana wa Shemeri.
47 the son of Mahli, the son of Mushi, the son of Merari, the son of Levi.
Shemeri alikuwa mwana wa Mahili. Mahili alikuwa mwana wa Mushi. Mushi alikuwa mwana wa Merari. Merari alikuwa mwana wa Levi.
48 And their brethren the Levites were given for all the service of the tabernacle of the house of God.
Walawi, alipangiwa kufanya kazi zote za hema, nyumba ya Mungu.
49 And Aaron and his sons offered upon the altar of the burnt-offering, and on the altar of incense, for all the work of the most holy place, and to make atonement for Israel, according to all that Moses the servant of God had commanded.
Aruni na wana wake walitoa sadaka katika madhabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketeza; na sadaka katika madhabahu ya uvumba kwa kazi zote katika pa patakatifu. Hizi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli, kwa kadiri ya yote ambayo Musa mtumishi wa Mungu aliwaamuru.
50 And these are the sons of Aaron: Eleazar his son, Phinehas his son, Abishua his son,
Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo: Mwana wa Aruni alikuwa Eleazari. Mwana Eleazari alikuwa Finehasi. Mwana wa Finehasi alikuwa Abishua.
51 Bukki his son, Uzzi his son, Zerahiah his son,
Mwana wa Abishua alikuwa Buki. Mwana wa Buki alikuwa Uzi. Mwana wa Buki alikuwa Zerahia.
52 Meraioth his son, Amariah his son, Ahitub his son,
Mwana wa Zerahia alikuwa Meraiothi. Mwana wa Meraiothi alikuwa Amaria. Mwana wa Amaria alikuwa Ahitubi.
53 Zadok his son, Ahimaaz his son.
Mwana wa Ahitubi alikuwa Zadoki. Mwana wa Zadoki alikuwa Ahimazi.
54 And these are their dwelling-places according to their encampments, within their borders. For the sons of Aaron, of the family of the Kohathites, for theirs was the lot;
Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao).
55 and they gave them Hebron in the land of Judah, and its suburbs round about it;
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda na nchi ya malisho,
56 but the fields of the city, and the hamlets thereof gave they to Caleb the son of Jephunneh.
lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 And to the children of Aaron they gave the city of refuge, Hebron; and Libnah and its suburbs, and Jattir, and Eshtemoa and its suburbs,
Kwa wazao wa Aruni waliwapa: Hebroni ( mji wa makimblio), na Libina pamoja na nchi ya malisho, Yatiri, Eshitemoa pamoja na nchi ya malisho,
58 and Hilen and its suburbs, Debir and its suburbs,
Hileni pamoja na nchi ya malisho, na Debiri pamoja na nchi ya malisho.
59 and Ashan and its suburbs, and Beth-shemesh and its suburbs;
Waliwapa uzao wa Aruni: Ashani pamoja na nchi ya malisho na Bethi Shemeshi pamoja na nchi ya malisho;
60 and, out of the tribe of Benjamin, Geba and its suburbs, and Allemeth and its suburbs, and Anathoth and its suburbs: all their cities, thirteen cities, according to their families.
na kutoka katika kabila la Benjamini walipewa Geba pamoja na nchi ya malisho, Alemethi pamoja na nchi ya malisho, na Anothothi na nchi ya malisho. Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu.
61 And to the children of Kohath that remained [were given] by lot out of the families of the tribe [of Ephraim and of the tribe of Dan and] of the half tribe, half Manasseh, ten cities.
Uzao mwengine wa Kohathi waliwapa kwa sehemu miji kumi kutoka kwa kabila la Manase.
62 And to the children of Gershom according to their families out of the tribe of Issachar, and out of the tribe of Asher, and out of the tribe of Naphtali, and out of the tribe of Manasseh in Bashan, thirteen cities.
Kwa uzao wa Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri, Naftali, na nusu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 To the children of Merari [were given] by lot, according to their families, out of the tribe of Reuben, and out of the tribe of Gad, and out of the tribe of Zebulun, twelve cities.
Kwa uzao wa Merari walipewa miji kumi, kulingana na koo zao, kutoka kwa makabila ya Rubeni, Gadi, na Zebuluni.
64 And the children of Israel gave to the Levites the cities and their suburbs.
Hivyo watu wa Israeli walitoa hii miji pamoja na nchi za malisho kwa Walawi.
65 And they gave by lot out of the tribe of the children of Judah, and out of the tribe of the children of Simeon, and out of the tribe of the children of Benjamin, these cities which were mentioned by name.
Walitoa kwa sehemu miji iliyo tajwa awali kutoka katika kabila la Yuda, Simeoni, na Benjamini.
66 And to the families of the children of Kohath who had the cities of their territory out of the tribe of Ephraim,
Kwa baadhi ya koo za Wakohathi walitoa miji kutoka kwa kabila la Efraimu.
67 they gave the city of refuge, Shechem and its suburbs in mount Ephraim; and Gezer and its suburbs,
Waliwapa: Shekemu ( mji wa makimbilio) pamoja na nchi ya malisho katika milima ya Efraimu, Gezeri na nchi ya malisho,
68 and Jokmeam and its suburbs, and Beth-horon and its suburbs,
Jokimeamu pamoja na nchi ya malisho, Bethi Horoni pamoja na nchi ya malisho,
69 and Ajalon and its suburbs, and Gath-Rimmon and its suburbs;
Aiyaloni pamoja na nchi ya malisho, na Gathi Rimoni pamoja na nchi ya malisho.
70 and out of the half tribe of Manasseh: Aner and its suburbs, and Bileam and its suburbs, — for the families of the children of Kohath that remained.
Nusu ya kabila la Manase waliwapa Wakohathi: Aneri pamoja na nchi ya malisho na Bileamu pamoja na nchi ya malisho. Hizi zikawa mali za koo za Wakohathi.
71 To the children of Gershom [were given] out of the family of the half tribe of Manasseh: Golan in Bashan and its suburbs, and Ashtaroth and its suburbs;
Kwa uzao wa Gerishomu kutoka koo za nusu ya kabila la Manase, waliwapa: Golani huko Baashani na nchi ya malisho na Ashitarothi pamoja na nchi ya malisho.
72 and out of the tribe of Issachar: Kedesh and its suburbs, Dobrath and its suburbs,
Kabila la Isakari liliwapa uzao wa Gerishomu: Kedeshi pamoja na nchi ya malisho, Dabera pamoja na nchi ya malisho,
73 and Ramoth and its suburbs, and Anem and its suburbs;
Ramothi pamoja na nchi ya malisho, na Anemu pamoja na nchi ya malisho.
74 and out of the tribe of Asher: Mashal and its suburbs, and Abdon and its suburbs,
Isakari alipokea kutoka kwa kabila la Asheri: Mashali pamoja na nchi ya malisho, Abdoni pamoja na nchi ya malisho,
75 and Hukok and its suburbs, and Rehob and its suburbs;
Hukoki pamoja na nchi ya malisho, na Rehobu pamoja na nchi ya malisho.
76 and out of the tribe of Naphtali: Kedesh in Galilee and its suburbs, and Hammon and its suburbs, and Kirjathaim and its suburbs.
Walipokea kutoka kabila la Naftali: Kedeshi iliyo Galileya pamoja na nchi ya malisho, Hamoni pamoja na nchi ya malisho, na Kiriathaimu pamoja na nchi ya malisho.
77 To the children of Merari that remained [were given] out of the tribe of Zebulun, Rimmono and its suburbs, [and] Tabor and its suburbs;
Kwa Walawi wengine, uzao wa Merari, walipewa kutoka kabila la Zebuluni: Rimono pamoja na nchi ya malisho na Tabori pamoja na nchi ya malisho.
78 and on the other side of the Jordan by Jericho, on the east side of the Jordan, out of the tribe of Reuben: Bezer in the wilderness and its suburbs, and Jahzah and its suburbs,
Kwa wao pia walipewa, upande wa pili wa Yordani huko Yeriko, kwa upande wa mashariki mwa mto: Bezeri katika jangwa pamoja na nchi ya malisho, Yahzahi pamoja na nchi ya malisho,
79 and Kedemoth and its suburbs, and Mephaath and its suburbs;
Kedemothi pamoka na nchi ya malisho, ma Mefathi pamoja na nchi ya malisho. Hizi zilitolewa kutoka kabila la Rubeni.
80 and out of the tribe of Gad: Ramoth in Gilead and its suburbs, and Mahanaim and its suburbs,
Walawi walipokea kutoka kabila la Gadi: Ramothi ya Gileadi pamoja na nchi ya malisho, Mahanaimu pamoja na nchi ya malisho,
81 and Heshbon and its suburbs, and Jaazer and its suburbs.
Heshiboni pamoja na nchi ya malisho, na Yazeri pamoja na nchi ya malisho.

< 1 Chronicles 6 >