< 1 Chronicles 24 >
1 And the divisions of the sons of Aaron: the sons of Aaron, Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar.
Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 And Nadab and Abihu died before their father, and had no children; and Eleazar and Ithamar exercised the priesthood.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
3 And David distributed them, both Zadok of the sons of Eleazar, and Ahimelech of the sons of Ithamar, according to their office in their service.
Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
4 And there were more head-men found of the sons of Eleazar than of the sons of Ithamar, and [thus] were they divided: of the sons of Eleazar there were sixteen heads of fathers' houses, and eight of the sons of Ithamar according to their fathers' houses.
Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
5 And they were divided by lot, one with another; for the princes of the sanctuary and the princes of God were of the sons of Eleazar and of the sons of Ithamar.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
6 And Shemaiah the son of Nethaneel the scribe, [one] of the Levites, inscribed them before the king, and the princes, and Zadok the priest, and Ahimelech the son of Abiathar, and the chief fathers of the priests and Levites: one father's house was drawn for Eleazar, and one drawn for Ithamar.
Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
7 And the first lot came forth for Jehoiarib, the second for Jedaiah,
Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
8 the third for Harim, the fourth for Seorim,
ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
9 the fifth for Malchijah, the sixth for Mijamin,
ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
10 the seventh for Hakkoz, the eighth for Abijah,
ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
11 the ninth for Jeshuah, the tenth for Shecaniah,
ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
12 the eleventh for Eliashib, the twelfth for Jakim,
ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
13 the thirteenth for Huppah, the fourteenth for Jeshebeab,
ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
14 the fifteenth for Bilgah, the sixteenth for Immer,
ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
15 the seventeenth for Hezir, the eighteenth for Happizez,
ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
16 the nineteenth for Pethahiah, the twentieth for Ezekiel,
ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
17 the twenty-first for Jachin, the twenty-second for Gamul,
ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
18 the twenty-third for Delaiah, the twenty-fourth for Maaziah.
ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
19 This is their ordering in their service to come into the house of Jehovah, according to their ordinance, through Aaron their father, as Jehovah the God of Israel had commanded him.
Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
20 And as for the rest of the sons of Levi: of the sons of Amram, Shubael; of the sons of Shubael, Jehdeiah.
Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
21 Of Rehabiah, of the sons of Rehabiah, the head was Jishijah.
Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
22 Of the Jizharites, Shelomoth; of the sons of Shelomoth, Jahath.
Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
23 — And the sons [of Hebron]: Jerijah [the head], Amariah the second, Jahaziel the third, Jekameam the fourth.
Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
24 The sons of Uzziel, Micah; of the sons of Micah, Shamir;
Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
25 the brother of Micah was Jishijah; of the sons of Jishijah, Zechariah.
Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
26 The sons of Merari: Mahli and Mushi; the sons of Jaaziah, his son.
Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
27 The sons of Merari by Jaaziah his son: Shoham, and Zaccur, and Ibri.
Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
28 Of Mahli: Eleazar, who had no sons.
Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
29 Of Kish, the sons of Kish: Jerahmeel.
Wana wa Kishi: Yerameli
30 And the sons of Mushi: Mahli, and Eder, and Jerimoth. These were the sons of the Levites according to their fathers' houses.
wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
31 These likewise cast lots just as their brethren the sons of Aaron before David the king, and Zadok, and Ahimelech, and the chief fathers of the priests and Levites, — the chief fathers just as the youngest of their brethren.
Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.