< 1 Chronicles 16 >
1 And they brought in the ark of God, and set it in the midst of the tent that David had spread for it; and they presented burnt-offerings and peace-offerings before God.
Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
2 And when David had ended offering up the burnt-offerings and the peace-offerings, he blessed the people in the name of Jehovah.
Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
3 And he dealt to every one of Israel, both man and woman, to every one a loaf of bread and a measure [of wine] and a raisin-cake.
Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
4 And he appointed certain of the Levites to do the service before the ark of Jehovah, and to celebrate, and to thank and praise Jehovah the God of Israel:
Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
5 Asaph the chief, and second to him Zechariah, Jeiel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Mattithiah, and Eliab, and Benaiah and Obed-Edom, and Jeiel, with instruments of lutes and with harps; and Asaph sounding with cymbals;
Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
6 and Benaiah and Jahaziel the priests with trumpets continually, before the ark of the covenant of God.
nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
7 Then on that day David delivered first [this psalm] to give thanks to Jehovah through Asaph and his brethren.
Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
8 Give thanks unto Jehovah, call upon his name; Make known his acts among the peoples.
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
9 Sing unto him, sing psalms unto him; Meditate upon all his wondrous works.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
10 Glory in his holy name: Let the heart of them rejoice that seek Jehovah.
Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
11 Seek Jehovah and his strength, Seek his face continually;
Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
12 Remember his wondrous works which he hath done; His miracles, and the judgments of his mouth:
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
13 Ye seed of Israel his servant, Ye sons of Jacob, his chosen ones.
enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14 He, Jehovah, is our God; His judgments are in all the earth.
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
15 Be ye ever mindful of his covenant, The word which he commanded to a thousand generations, —
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
16 Which he made with Abraham, And of his oath unto Isaac;
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
17 And he confirmed it unto Jacob for a statute, Unto Israel for an everlasting covenant,
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
18 Saying, Unto thee will I give the land of Canaan, The lot of your inheritance;
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
19 When ye were a few men in number, Of small account, and strangers in it.
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
20 And they went from nation to nation, And from one kingdom to another people.
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
21 He suffered no man to oppress them, And reproved kings for their sakes,
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
22 [Saying, ] Touch not mine anointed ones, And do my prophets no harm.
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
23 Sing unto Jehovah, all the earth; Publish his salvation from day to day.
Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
24 Declare his glory among the nations, His wondrous works among all peoples.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
25 For Jehovah is great, and exceedingly to be praised; And he is terrible above all gods.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
26 For all the gods of the peoples are idols; But Jehovah made the heavens.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
27 Majesty and splendour are before him; Strength and gladness in his place.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
28 Give unto Jehovah, ye families of peoples, Give unto Jehovah glory and strength!
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
29 Give unto Jehovah the glory of his name! Bring an oblation, and come before him: Worship Jehovah in holy splendour.
mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
30 Tremble before him, all the earth: The world also is established, it shall not be moved.
Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
31 Let the heavens rejoice, and let the earth be glad; And let them say among the nations, Jehovah reigneth!
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
32 Let the sea roar, and the fulness thereof; Let the field exult, and all that is therein.
Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
33 Then shall the trees of the forest sing out at the presence of Jehovah, For he cometh to judge the earth.
Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
34 Give thanks unto Jehovah, for he is good; For his loving-kindness [endureth] for ever.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
35 And say, Save us, O God of our salvation, And gather us, and deliver us from the nations, To give thanks unto thy holy name, To triumph in thy praise.
Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
36 Blessed be Jehovah the God of Israel, from eternity and to eternity! And all the people said, Amen! and praised Jehovah.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
37 And he left there, before the ark of the covenant of Jehovah, Asaph and his brethren, to do the service before the ark continually, as every day's duty required;
Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
38 and Obed-Edom, and their brethren, sixty-eight; Obed-Edom also, the son of Jeduthun, and Hosah as doorkeepers.
Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
39 And Zadok the priest, and his brethren the priests, before the tabernacle of Jehovah in the high place that was at Gibeon,
Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
40 to offer up burnt-offerings to Jehovah on the altar of burnt-offering continually, morning and evening, and according to all that is written in the law of Jehovah, which he commanded Israel;
ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
41 and with them Heman and Jeduthun, and the rest that were chosen, who were expressed by name, to give thanks to Jehovah, because his loving-kindness [endureth] for ever;
Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
42 and with them, [with] Heman and Jeduthun, trumpets and cymbals for those that should sound aloud; and the musical instruments of God. And the sons of Jeduthun were at the gate.
Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
43 And all the people departed every one to his house; and David returned to bless his household.
Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.