< Psalms 88 >

1 A Canticle Psalm to the sons of Korah. Unto the end. For Mahalath, to answer the understanding of Heman the Ezrahite. O Lord, God of my salvation: I have cried out, day and night, in your presence.
Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
2 Let my prayer enter in your sight. Incline your ear to my petition.
Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
3 For my soul has been filled with evils, and my life has drawn near to Hell. (Sheol h7585)
Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
4 I am considered to be among those who will descend into the pit. I have become like a man without assistance,
Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5 idle among the dead. I am like the wounded sleeping in sepulchers, whom you no longer remember, and who have been repelled by your hand.
Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6 They have lain me in the lower pit: in dark places and in the shadow of death.
Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
7 Your fury has been confirmed over me. And you have brought all your waves upon me.
Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
8 You have sent my acquaintances far from me. They have set me as an abomination to themselves. I was handed over, yet I did not depart.
Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9 My eyes languished before destitution. All day long, I cried out to you, O Lord. I stretched out my hands to you.
Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
10 Will you perform wonders for the dead? Or will physicians raise to life, and so confess to you?
Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
11 Could anyone declare your mercy in the sepulcher, or your truth from within perdition?
Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
12 Will your wonders be known in the darkness, or your justice in the land of oblivion?
Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
13 And I have cried out to you, O Lord, and in early morning, my prayer will come before you.
Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
14 Lord, why do you reject my prayer? Why do you turn your face away from me?
Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
15 I am poor, and I have been amid hardships from my youth. And, though I have been exalted, I am humbled and disturbed.
Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
16 Your wrath has crossed into me, and your terrors have disturbed me.
Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
17 They have surrounded me like water, all day long. They have surrounded me, all at once.
Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
18 Friend and neighbor, and my acquaintances, you have sent far away from me, away from misery.
Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.

< Psalms 88 >