< Psalms 81 >
1 Unto the end. For the wine and oil presses. A Psalm of Asaph himself. Exult before God our helper. Sing joyfully to the God of Jacob.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 Take up a psalm, and bring forth the timbrel: a pleasing Psalter with stringed instruments.
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 Sound the trumpet at the new moon, on the noteworthy day of your solemnity,
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 for it is a precept in Israel and a judgment for the God of Jacob.
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 He set it as a testimony with Joseph, when he went out of the land of Egypt. He heard a tongue that he did not know.
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 He turned the burdens away from his back. His hands had been a slave to baskets.
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 You called upon me in tribulation, and I freed you. I heard you within the hidden tempest. I tested you with waters of contradiction.
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 My people, listen and I will call you to testify. If, O Israel, you will pay heed to me,
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 then there will be no new god among you, nor will you adore a foreign god.
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 For I am the Lord your God, who led you out of the land of Egypt. Widen your mouth, and I will fill it.
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 But my people did not hear my voice, and Israel was not attentive to me.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 And so, I sent them away, according to the desires of their heart. They will go forth according to their own inventions.
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 If my people had heard me, if Israel had walked in my ways,
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 I would have humbled their enemies, as if it were nothing, and I would have sent my hand upon those who troubled them.
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 The enemies of the Lord have lied to him, and their time will come, in every age.
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 And he fed them from the fat of the grain, and he saturated them with honey from the rock.
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”