< Psalms 77 >

1 Unto the end. For Jeduthun. A Psalm of Asaph. I cried out to the Lord with my voice, to God with my voice, and he attended to me.
Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
2 In the days of my tribulation, I sought God, with my hands opposite him in the night, and I was not deceived. My soul refused to be consoled.
Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
3 I was mindful of God, and I was delighted, and I was distressed, and my spirit fell away.
Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
4 My eyes anticipated the vigils. I was disturbed, and I did not speak.
Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
5 I considered the days of antiquity, and I held the years of eternity in my mind.
Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6 And I meditated in the night with my heart, and I was distressed, and I examined my spirit.
Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7 So then, will God reject for eternity? Will he not continue to allow himself to show favor?
Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8 Or, will he cut off his mercy in the end, from generation to generation?
Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9 And would God ever forget to be merciful? Or, would he, in his wrath, restrict his mercies?
Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
10 And I said, “Now I have begun. This change is from the right hand of the Most High.”
Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11 I was mindful of the works of the Lord. For I will be mindful from the beginning of your wonders,
Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12 and I will meditate on all your works. And I will take part in your intentions.
Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13 Your way, O God, is in what is holy. Which God is great like our God?
Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14 You are the God who performs miracles. You have made your virtue known among the peoples.
Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15 With your arm, you have redeemed your people, the sons of Jacob and of Joseph.
Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
16 The waters saw you, O God, the waters saw you, and they were afraid, and the depths were stirred up.
Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17 Great was the sound of the waters. The clouds uttered a voice. For your arrows also pass by.
Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
18 The voice of your thunder is like a wheel. Your flashes have illuminated the whole world. The earth has quaked and trembled.
Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
19 Your way is through the sea, and your paths are through many waters. And your traces will not be known.
Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
20 You have conducted your people like sheep, by the hand of Moses and Aaron.
Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.

< Psalms 77 >