< Psalms 76 >

1 Unto the end. With Praises. A Psalm of Asaph. A Canticle to the Assyrians. In Judea, God is known. In Israel, his name is great.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
2 And his place has been formed with peace. And his dwelling place is in Zion.
Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
3 In that place, he has broken the powers of the bows, the shield, the sword, and the battle.
Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
4 You illuminate wondrously from the mountains of eternity.
Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
5 All the foolish of heart have been disturbed. They have slept their sleep, and all the men of riches have found nothing in their hands.
Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
6 At your rebuke, O God of Jacob, those who were mounted on horseback have fallen asleep.
Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
7 You are terrible, and so, who can withstand you? From thence is your wrath.
Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
8 You have caused judgment to be heard from heaven. The earth trembled and was quieted,
Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
9 when God rose up in judgment in order to bring salvation to all the meek of the earth.
wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
10 For the thinking of man will confess to you, and the legacy of his thinking will keep a feast day to you.
Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
11 Make vows and pay them to the Lord, your God. All you who surround him bring gifts: to him who is terrible,
Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
12 even to him who takes away the spirit of leaders, to him who is terrible with the kings of the earth.
Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.

< Psalms 76 >