< Psalms 48 >
1 A Canticle Psalm. To the sons of Korah, on the second Sabbath. The Lord is great and exceedingly praiseworthy, in the city of our God, on his holy mountain.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
2 Mount Zion is being founded with the exultation of the whole earth, on the north side, the city of the great king.
Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
3 In her houses, God will be known, since he will support her.
Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
4 For behold, the kings of the earth have been gathered together; they have convened as one.
Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
5 Such did they see, and they were astonished: they were disturbed, they were moved.
walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
6 Trembling took hold of them. In that place, their pains were that of a woman in labor.
Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
7 With a vehement spirit, you will crush the ships of Tarshish.
Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
8 As we have heard, so we have seen, in the city of the Lord of hosts, in the city of our God. God has founded it in eternity.
Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
9 We have received your mercy, O God, in the midst of your temple.
Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
10 According to your name, O God, so does your praise reach to the ends of the earth. Your right hand is full of justice.
Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
11 Let mount Zion rejoice, and let the daughters of Judah exult, because of your judgments, O Lord.
Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
12 Encircle Zion and embrace her. Discourse in her towers.
Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
13 Set your hearts on her virtue. And distribute her houses, so that you may discourse of it in another generation.
yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
14 For this is God, our God, in eternity and forever and ever. He will rule us forever.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.