< Psalms 45 >

1 Unto the end. For those who will be changed. To the sons of Korah, toward understanding. A Canticle for the Beloved. My heart has uttered a good word. I speak of my works to the king. My tongue is like the pen of a scribe who writes quickly.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
2 You are a brilliant form before the sons of men. Grace has been poured freely into your lips. Because of this, God has blessed you in eternity.
Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Fasten your sword to your thigh, O most powerful one.
Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
4 With your splendor and your excellence extended, proceed prosperously, and reign for the sake of truth and meekness and justice, and so will your right hand lead you wondrously.
Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
5 Your arrows are sharp; the people will fall under you, with the hearts of the enemies of the king.
Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
6 Your throne, O God, is forever and ever. The scepter of your kingdom is a scepter of true aim.
Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
7 You have loved justice and hated iniquity. Because of this, God, your God, has anointed you, before your co-heirs, with the oil of gladness.
Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
8 Myrrh and balsam and cinnamon perfume your garments, from the houses of ivory. From these, they have delighted you:
Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
9 the daughters of kings in your honor. The queen assisted at your right hand, in clothing of gold, encircled with diversity.
Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
10 Listen, daughter, and see, and incline your ear. And forget your people and your father’s house.
Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11 And the king will desire your beauty. For he is the Lord your God, and they will adore him.
Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
12 And the daughters of Tyre will entreat your countenance with gifts: all the rich men of the people.
Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
13 All the glory of the daughter of its king is inside, in golden fringes,
Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
14 clothed all around with diversities. After her, virgins will be led to the king. Her neighbors will be brought to you.
Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
15 They will be brought with gladness and exultation. They will be led into the temple of the king.
Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
16 For your fathers, sons have been born to you. You will establish them as leaders over all the earth.
Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
17 They will remember your name always, for generation after generation. Because of this, people will confess to you in eternity, even forever and ever.
Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.

< Psalms 45 >