< Psalms 2 >
1 Why have the Gentiles been seething, and why have the people been pondering nonsense?
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 The kings of the earth have stood up, and the leaders have joined together as one, against the Lord and against his Christ:
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 “Let us shatter their chains and cast their yoke away from us.”
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 He who dwells in heaven will ridicule them, and the Lord will mock them.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Then will he speak to them in his anger and trouble them with his fury.
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 Yet I have been appointed king by him over Zion, his holy mountain, preaching his precepts.
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 The Lord has said to me: You are my son, this day have I begotten you.
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Ask of me and I will give to you: the Gentiles for your inheritance, and the ends of the earth for your possession.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 You will rule them with an iron rod, and you will shatter them like a potter’s vessel.
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 And now, O kings, understand. Receive instruction, you who judge the earth.
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 Serve the Lord in fear, and exult in him with trembling.
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Embrace discipline, lest at any time the Lord might become angry, and you would perish from the way of the just. Though his wrath can flare up in a short time, blessed are all those who trust in him.
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.