< Psalms 120 >
1 A Canticle in steps. When troubled, I cried out to the Lord, and he heard me.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 O Lord, free my soul from lips of iniquity and from the deceitful tongue.
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 What will be given to you, or what will be added to you, for a deceitful tongue?:
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 the sharp arrows of the powerful, along with the burning coals of desolation.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Woe to me, for my sojourning has been prolonged. I have lived with the inhabitants of Kedar.
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 My soul has long been a sojourner.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 With those who hated peace, I was peaceful. When I spoke to them, they fought against me without cause.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.