< Psalms 111 >

1 Alleluia. I will confess to you, O Lord, with my whole heart, in the council of the just and in the congregation.
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 Great are the works of the Lord, exquisite in all his intentions.
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 Confession and magnificence are his work. And his justice remains from age to age.
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4 He has created a memorial to his wonders; he is a merciful and compassionate Lord.
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 He has given food to those who fear him. He will be mindful of his covenant in every age.
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6 He will announce the virtue of his works to his people,
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 so that he may give them the inheritance of the nations. The works of his hands are truth and judgment.
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 All his commands are faithful: confirmed from age to age, created in truth and fairness.
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 He has sent redemption upon his people. He has commanded his covenant for all eternity. Holy and terrible is his name.
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 The fear of the Lord is the beginning of wisdom. A good understanding is for all who do it. His praise remains from age to age.
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.

< Psalms 111 >