< Proverbs 10 >

1 A wise son gladdens the father. Yet truly, a foolish son is the grief of his mother.
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
2 Treasures of impiety will profit nothing. Truly, justice shall liberate from death.
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
3 The Lord will not afflict with famine the soul of the just, and he will overthrow the treacheries of the impious.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
4 The neglectful hand has wrought destitution. But the hand of the steadfast prepares riches. He who advances by lies, this one feeds on the wind. For he is the same as one who runs after flying birds.
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
5 He who gathers the harvest is a wise son. But he who snores in warm weather is a son of confusion.
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6 The blessing of the Lord is on the head of the just. But iniquity covers the mouth of the impious.
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
7 The remembrance of the just is with praises. And the name of the impious shall decay.
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
8 The wise of heart accept precepts. The foolish are cut down by the lips.
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9 He who walks in simplicity walks in confidence. But he who corrupts his ways shall be discovered.
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10 He who winks with the eye gives sorrow. And the foolish in lips shall be beaten.
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11 The mouth of the just is a vein of life. And the mouth of the impious covers iniquity.
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12 Hatred rises up from disputes. And charity covers all offenses.
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13 In the lips of the wise, wisdom is discovered. And a rod is for the back of one who lacks heart.
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14 The wise store away knowledge. But the mouth of the foolish is a neighbor to confusion.
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
15 The substance of the rich is the city of his strength. The fear of the poor is their destitution.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16 The work of the just is unto life. But the fruit of the impious is unto sin.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17 The way of life is for those who observe discipline. But whoever abandons correction wanders astray.
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18 Lying lips conceal hatred; whoever brings forth contempt is unwise.
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19 In a multitude of speaking, sin will not be lacking. But whoever tempers his lips is most prudent.
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20 The tongue of the just is choice silver. But the heart of the impious is exchanged for nothing.
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21 The lips of the just instruct many. But those who are unlearned shall die in destitution of heart.
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
22 The blessing of the Lord causes riches. Affliction will not be a companion to them.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
23 The foolish work wickedness as if in jest. But wisdom is prudence to a man.
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
24 What the impious fear will overwhelm them. The just shall be given their desire.
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
25 Like a passing tempest, so the impious one will be no more. But the just one is like an everlasting foundation.
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
26 Like vinegar to the teeth, and smoke to the eyes, so is a lazy one to those who sent him.
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 The fear of the Lord adds days. And the years of the impious will be shortened.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
28 The expectation of the just is rejoicing. But the hope of the impious will perish.
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
29 The strength of the simple is the way of the Lord, and it is fear to those who work evil.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
30 The just in eternity shall not be moved. But the impious will not live upon the earth.
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
31 The mouth of the just shall bring forth wisdom. The tongue of the depraved will perish.
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
32 The lips of the just consider what is acceptable. And the mouth of the impious considers perversities.
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.

< Proverbs 10 >