< Micah 7 >

1 Woe to me, for I have become just like one who gleans the clusters of the vintage in autumn. There is no cluster of grapes to consume; my soul desired figs out of season.
Ole wangu! Kwangu mimi ni kama msimu wa mavuno ulipokwisha, na pia makombo ya mavuno ya zabibu kwenye shamba la mizabibu: Hakuna tena kishamba cha matunda kinachoonekana, hakuna matini ya malimbuka ambayo ninayoyatamani.
2 The holy ones pass away from the land, and there is no one righteous among men. All wait in ambush for blood; a man hunts his brother to death.
Watu waaminifu wamepotelea kutoka kwenye nchi, hakuna mtu mwadilifu katika wanadamu wote. Wote hudanganya katika kusubiri kumwaga damu; kila mtu humuwinda ndugu yake mwenyewe kwa wavu.
3 The evil of their hands, they call good. The leader is demanding, and the judge is yielding, and the great is speaking the desire of his soul, and they have confused it.
Mikono yao ni mizuri mno kwa kufanya madhara. watawala huuliza pesa, hakimu yuko tayari kwa rushwa, na mtu mwenye nguvu anawaambia wengine kile anachokitaka kujipatia. Hivyo ndivyo waundavyo kwa pamoja.
4 Whoever is best among them is like a thorny plant, and he who is righteous is like a thorny hedge. The day of your inspection, your visitation, arrives. Now will be their ruination.
Mtu bora kwao ni kama mitemba, mwadilifu sana ni kama mche wa miba. Imefika siku iliyosemwa nyuma na walinzi wako, siku ya hukumu. Sasa ni mda wa machafuko.
5 Do not be willing to believe a friend. And do not be willing to confide in a commander. From her, who sleeps in your bosom, keep the doors of your mouth closed.
Msimwamini kila jirani; msimuweke kiongozi katika rafiki yeyote. Kuweni makini kuhusiana na kile msemacho hata kwa mwanamke ambaye adanganyaye kwenye mikono yenu.
6 For the son acts with contempt for the father, and the daughter rises up against her mother, the daughter-in-law against her mother-in-law, and a man’s enemies are those of his own household.
Kwa kuwa mwana humfedhehesha baba yake, binti huinuka kushindana na mama yake, na mke wa mwana wa kiume hushindana na mama mkwe wake. Adui wa watu ni watu wa nyumba yake mwenyewe.
7 But I will look towards the Lord. I will wait for God, my Savior. My God will hear me.
Lakini kama kwangu mimi, nitamtazama Yahwe. Nitamsubiri Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu ataniskia.
8 You, my enemy, should not rejoice over me because I have fallen. I will rise up, when I sit in darkness. The Lord is my light.
Usifurahi juu yangu, adui yangu. Niangukapo, nitainuka. Wakati nitakapokuwa nimekaa katika giza, Yahwe atakuwa mwanga kwangu.
9 I will carry the wrath of the Lord, because I have sinned against him, until he may judge my case and execute judgment for me. He will lead me into the light. I will behold his justice.
Kwasababu nimetenda dhambi dhidi ya Yahwe, nitachukua ghadhabu yake hata aniteteapo kosa langu, na kutekeleza hukumu kwa ajili yangu. Atanileta kwenye nuru, na nitamwona akiniokoa kwenye haki yake.
10 And my enemy will look, and she will be covered with confusion, she who says to me, “Where is the Lord your God?” My eyes will look upon her. Now she will be trampled underfoot like the mud of the streets.
Kisha adui yangu atakapoliona hilo, na aibu itamfunika yule aliyeniambia, “Yahwe Mungu wako yuko wapi?” macho yangu yatamtazama; atakanyagwa chini kama tope kwenye mitaa.
11 The day that your walls will be rebuilt, in that day the law will be far away.
Siku ya ya kujenga kuta zako zitafika; siku hiyo mipaka itasogezwa mbali sana.
12 In that day also, they will come towards you even from Assur, and even to the fortified cities, and from the fortified cities even to the river, and from sea to sea, and from mountain to mountain.
Siku hiyo watu watakuja kwako, kutoka Ashuru na miji katika Misri, kutoka Misri hata mto mkubwa, kutoka bahari kwenda bahari, na kutoka mlima kwenda mlima.
13 And the land will be in desolation, because of its inhabitants and because of the fruit of their intentions.
Hizo nchi zitakuwa zimejitenga kwasababu ya watu ambao wanaishi huko sasa, kwasababu ya tunda la matendo yao.
14 With your rod, pasture your people, the flock of your inheritance, living alone in the narrow forest, in the midst of Carmel. They will graze in Bashan and Gilead, as in the ancient days.
Chunga watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako. Wanaishi wenyewe kwenye msitu, katikati ya msitu. Wachunge katika Bashani na Gileadi kama siku za zamani.
15 As in the days of your departure from the land of Egypt, I will reveal miracles to him.
Kama katika siku wakati mlipotoka nje ya nchi ya Misri, nitawaonyesha maajabu.
16 The nations will look, and they will be confounded at the strength of them all. They will place hand over mouth; their ears will be deaf.
Mataifa yataona na kuwa na aibu ya nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye midomo yao; masikio yao yatakuwa kiziwi.
17 They will lick the dust like serpents, and, like the creeping things of the earth, they will be disturbed in their houses. They will dread the Lord our God, and they will fear you.
Watalamba vumbi kama nyoka, kama viumbe vitaambavyo juu ya nchi. Watatoka nje kwenye maficho kwa hofu; watakuja kwako kwa hofu, Yahwe Mungu wetu, na wataogopa kwa sababu yako.
18 What God is like you, who takes away iniquity and passes over the sin of the remnant of your inheritance? No longer will he send forth his fury, because he is willing to be merciful.
Ni nani aliye Mungu kama wewe, wewe uchukuaye dhambi, wewe upitaye juu ya kosa la mabaki ya mrithi wako? Hutunzi hasira yako milele, kwa sababu unapenda kutuonyesha agano lako la aminifu.
19 He will turn back and have mercy on us. He will put away our iniquities, and he will cast all our sins into the depths of the sea.
Tena utakuwa na huruma juu yetu; utayakanyaga maovu chini ya miguu yako. Utazitupa dhambi zetu zote kwenye vilindi vya bahari.
20 You will give the truth to Jacob, mercy to Abraham, which you swore to our fathers from the ancient days.
Utampatia ukweli Yakobo na agano aminifu kwa Abrahamu, ulipoapa kwa babu zetu katika siku za kale.

< Micah 7 >