< Micah 1 >

1 The word of the Lord that came to Micah the Moreshethite, in the days of Jotham, Ahaz, and Hezekiah, kings of Judah, which he saw about Samaria and Jerusalem.
Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
2 All peoples, listen. And may the earth and its fullness pay attention. And may the Lord God be a witness to you, the Lord from his holy temple.
Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
3 For behold, the Lord will go forth from his place. And he will descend, and he will trample over the high places of the earth.
Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
4 And the mountains will be consumed under him, and the valleys will be torn apart, like wax before the face of fire, and like waters that rush swiftly downward.
Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
5 All this is for the wickedness of Jacob and for the sins of the house of Israel. What is the wickedness of Jacob? Is it not Samaria? And what is the loftiness of Judah? Is it not Jerusalem?
Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
6 And I will place Samaria like a pile of stones in the field, when a vineyard is planted. And I will pull down its stones into the valley, and I will reveal her foundations.
“Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
7 And all her graven images will be cut to pieces, and all her rewards will be burned with fire, and I will place all her idols in perdition. For they have been gathered together from the pay of a kept woman, and even to the pay of a kept woman, they will return.
Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
8 I will lament and wail about this. I will go out despoiled and naked. I will make a howl like the dragons, and a mourning like the ostriches.
Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
9 For her wound has been in despair. For it has come even to Judah. It has touched the gate of my people, even to Jerusalem.
Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
10 Do not be willing to announce it in Gath; may you not lament with tears. In the house of Dust, besprinkle yourselves with dust.
Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
11 And cross over to your dwelling place, Beauty, bewildered by disgrace. She did not depart, who dwells at the place of departure. The House nearby, which remained firm by herself, will receive mourning from you.
Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
12 For she has been weakened in goodness, who dwells in bitterness. For disaster has descended from the Lord to the gate of Jerusalem.
Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
13 A tumult of four-horse chariots has stupefied the inhabitants of Lachish. The beginning has been sin for the daughter of Zion, because in you have been found the evil deeds of Israel.
Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
14 Because of this, she will send emissaries to the inheritance of Gath: the house of Lying in order to deceive the kings of Israel.
Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
15 Nevertheless, I will lead an heir to you, who dwell in Mareshah: the glory of Israel will reach all the way to Adullam.
Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
16 Become bald and shaved for your delicate sons. Increase your baldness like the eagle. For they have been carried into captivity from you.
Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.

< Micah 1 >