< Leviticus 7 >

1 Likewise, this is the law of the sacrifice for a transgression. It is the Holy of holies.
Hii ndiyo sheria ya sadaka ya hatia. Kwa sababu hiyo ni sadaka takatifu sana.
2 Therefore, where the holocaust is immolated, the victim for a transgression shall also be slain. Its blood shall be poured out all around the altar.
Ni lazima waichinje sadaka ya hatia mahali panapostali kuchinjwa, na ni lazima watainyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
3 They shall offer from it: the rump, and the fat that covers the vital organs,
Mafuta yote yaliyomo ndani yake yataondolewa: mafuta ya mkiani, mafuta yaliyo sehamu za ndani,
4 the two little kidneys, and the fat that is near the sides, and the mesh of the liver with the little kidneys.
zile figo mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake, yaliyo karibu na kiuno, na yanayofunika ini—nyama hii yote lazima iondolewe pamoja na hizo figo.
5 And the priest shall burn them upon the altar. It is the incense of the Lord on behalf of a transgression.
Kuhani ataviteketeza vipande hivi juu ya madhabahu viwe dhabihu iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto. Hii ni sadaka ya hatia
6 Every male of priestly descent shall feed on this flesh in a holy place, because it is the Holy of holies.
Kila mwanaume miongoni mwa familia ya kuhani anaweza kula sehemu ya sadaka hii. Lakini ni lazima iliwe ndani ya mahali patakatifu kwa sababu ni takatifu sana.
7 Just as the sacrifice for sin is offered, so also for a transgression; one law shall be for both sacrifices. It shall belong to the priest who offers it.
Nayo sadaka ya dhambi ni kama ilivyo sadaka ya hatia. Ni sheria ileile hutumika kwa zote mbili. Zote ni mali ya kuhani azitumiaye kufanya upatanisho.
8 The priest who offers the victim of holocaust shall have its skin.
Kuhani atoaye sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya mtu yeyote anaweza kuchuku ngozi ya sadaka hiyo kwa ajili yake mwenyewe.
9 And every sacrifice of fine wheat flour which is baked in the oven, and whatever is prepared on the oven grating or in the frying pan, shall be for the priest who offers it.
Kila sadaka ya nafaka inayookwa mekoni, na kila sadaka kama hiyo ipikwayo kaangoni au kwenye sufuria itakuwa ya kuhani aitoaye.
10 Whether these will be sprinkled with oil, or left dry, an equal measure shall be divided to each one of the sons of Aaron.
Kila sadaka ya nafaka, ama iwe unga mkavu au uliochanganywa na mafuta ya zeitu itakuwa ya ukoo wa Aroni kwa usawa.
11 This is the law of the victim of peace offerings, which is offered to the Lord.
Hii ndiyo sheria ya dhabihu ya sadaka za amani, ambazo watu watazitoa kwa Yahweh.
12 If the oblation will be an act for giving thanks, they shall offer bread without leaven sprinkled with oil, and unleavened wafers anointed with oil, and fine wheat flour fried, and cakes sprinkled and mixed with oil,
Iwapo mtu yeyote anaitoa ili kuonyesha shukrani kwa Yahweh, basi ataitoa pamoja na dhabih uya mikate iliyotengenezwa bila hamira, bali kwa mafuta ya zeituni yaliyochanganywa na unga lakini bila hamira, na maandazi yaliyotengenezwa bila hamira, bali yaliyopakwa mafuta juu yake, na mikate miembamba iliyofanywa kwa unga laini uliochanganywa na mafuta.
13 and also, leavened bread with the sacrifice of thanksgiving, which is immolated for peace offerings.
Kwa kusudi la kutoa shukrani, pia anapaswa kutoa pamoja na sadaka yake ya amani, vipande vya mikate iliyotiwa hamira.
14 Of these, one shall be offered to the Lord as the first-fruits, and one shall be for the priest who will pour out the blood of the victim.
Ni lazima atatoa moja kila aina ya sadaka hizi kama sadaka iliyoletwa kwa Yahweh. Nayo itakuwa ya makuhani wanaonyunyizia damu ya sadaka ya amani kwenye madhabahu.
15 The flesh of it shall be eaten on the same day; neither shall any of it remain until morning.
Mtu anayeleta sadaka ya amani kwa kusudi la kutoa shukrani ni lazima ataila nyama ya sadaka yake siku ya kutoa dhabihu. Hatakiwi kusaza chochote kilicho cha sadaka hiyo hata asubuhi ya pili.
16 If anyone, by a vow or of his own accord, will have offered a sacrifice, it shall be eaten in a similar manner on the same day. But then if any of it will have remained until tomorrow, it is lawful to eat it.
Lakini iwapo dhabihu ya matoleo yake kusudi lake ni nadhiri, au kwa kusudi la sadaka ya hiari, nyama yake italiwa siku iyo hiyo aitoapo dhabihu yake, lakini chochote kinachosalia cha sadaka hiyo kinaweza kuliwa siku inayofuata.
17 Then whatever will be found on the third day shall be consumed with fire.
Hata hivyo, nyama yoyote ya dhabihu inayobaki siku ya tatu ni lazima ichomwe moto.
18 If anyone will have eaten from the flesh of the victim of peace offerings on the third day, the oblation will be nullified; neither will it benefit the one who offered it. But instead, whatever soul will contaminate itself with such foods will be guilty of a betrayal.
Iwapo kipande chochote cha nyama hiyo ya dhabihu kinachobaki kinaliwa katika siku ya tatu, hakitakubalika, wala hakitatolewa kwa aliyeitoa. Kitakuwa ni kitu cha kuchukiza, na mtu akilaye atabeba hatia ya dhambi mwenyewe yake.
19 The flesh that has touched anything unclean shall not be eaten, but it shall be burnt with fire. He that is clean will feed on it.
Nyama yoyote inayogusa kitu kilicho najisi haitaliwa. Ni lazima ichomwe moto. Na kwa ajili ya nyama inayobaki, yeyote aliye safi anaweza kuila.
20 If a soul which is polluted will have eaten from the flesh of the sacrifice of peace offerings, which is offered to the Lord, he shall perish from his people.
Hata hivyo, mtu najisi anayekula nyama kutoka kwenye dhabihu ya matoleo ya amani ambayo ni ya Yahweh yapasa mtu huyu akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
21 And whoever will have touched the uncleanness of man, or of beast, or of anything which is able to defile, and who will have eaten from this kind of flesh, shall be cut off from his people.
Iwapo mtu yeyote anagusa kitu chochote kilichonajisi—iwe ni unajisi wa binadamu, au wa mnyama aliyenajisi, au wa kitu fulani kilichonajisi na chenye kuchukiza, na kisha akala baadhi ya nyama ya dhabihu ya sadaka ya amani iliyotolewa kwa Yahweh, lazima mtu huyo akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.
22 And the Lord spoke to Moses, saying:
Kisha Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
23 Say to the sons of Israel: The fat of a sheep, and of an ox, and of a goat you shall not eat.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'hamruhusiwi kula mafuta ya fahali au kondoo au mbuzi.
24 The fat of a carcass that has died on its own, or of an animal that has been seized by a wild beast, you shall have for various uses.
Mafuta ya mnyama yoyote afaye peke yake bila ya kuwa dhabihu, au mafuta ya mnyama yeyote aliyeraruliwa na wanyama pori, yanaweza kutumika kwa makusudi mengine, lakini hakika hamtayala.
25 If anyone will have eaten the fat which ought to be offered as a burnt sacrifice of the Lord, he shall perish from his people.
Yeyote atakayekula mafuta ya mnyama ambayo watu wanaweza kuyatoa kuwa dhabihu ya iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, mtu huyo lazima atakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake.
26 Likewise, you shall not take as food the blood of any animals at all, whether of birds or beasts.
Hamtakula damu yoyote katika mojawapo ya nyumba zenu, ama iwe kutoka kwa ndege au mnyama.
27 Every soul that will have eaten blood shall perish from his people.
Yeyote alaye damu yoyote, mtu huyo lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.'”
28 And the Lord spoke to Moses, saying:
Kwa hiyo Yahweh akazungumza na Musa na akasema,
29 Speak to the sons of Israel, saying: Whoever offers a victim of peace offerings to the Lord, let him also offer at the same time a sacrifice, that is, its libations.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Yeye atoaye dhabidhu ya sadaka ya amani kwa Yahweh lazima alete sehemu ya dhabihu yake kwa Yahweh.
30 He shall hold in his hands the fat of the victim, and the breast. And when he will have offered and consecrated both to the Lord, he shall deliver them to the priest,
Mikono yake mwenyewe lazima iilete hiyo sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto. Naye atayaleta hayo mafuta pamoja na kidari, ili kwamba kidari kiweze kutikiswa kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
31 who shall burn the fat upon the altar. But the breast shall be for Aaron and his sons.
Kuhani atayachoma mafuta hayo juu ya madhabahu, lakini kile kidari kitakuwa mali ya Aroni na uzao wake.
32 Likewise also, the right shoulder of the victim of peace offerings shall fall to the priest as first-fruits.
Ni lazima utatoa paja la kulia kwa kuhani kama sadaka iliyotokana na dhabihu ya sadaka yako ya amani.
33 Among the sons of Aaron, whoever will have offered the blood and the fat, the same one shall also have the right shoulder for his portion.
Yule kuhani, mmoja wa wazao wa Aroni, atoaye damu na mafuta ya sadaka ya amani—ni lazima atapata paja la kulia kama mgao wake wa sadaka.
34 So then, the breast that is lifted up, and the shoulder that is separated, I have taken from the sons of Israel, from their victims of peace offerings, and I have given these to Aaron the priest and to his sons, as a law in perpetuity, from all the people of Israel.
Kwa kuwa nimetwaa kidari, na paja la sadaka ya kutikiswa kutoka kwa watu wa Israeli uwe mchango wao, na amepewa Aroni kuhani na wanawe kuwa mgao wao wa kawaida.
35 This is the anointing of Aaron and his sons, by the ceremonies of the Lord, in the day when Moses offered them, so that they may fulfill the priesthood,
Huu ndiyo mgao wa Aroni na uzao wake utokanao na matoleo yaliyofanywa kwa Yahweh kwa moto, siku ile Musa alipowaweka wakfu ili kumtumikia Yahweh katika kazi ya kuhani.
36 and this is what the Lord instructed to be given to them by the sons of Israel, as a perpetual observance in their generations.
Huu ndio mgao ambao Yahweh aliamru waweze kupewa kutoka kwa watu wa Israeli, katika siku hiyo aliyowatia mafuta ya upako wawe makuhani. Nao utakuwa mgao wao wa kila siku katika vizazi vyote.
37 This is the law of the holocaust, and of the sacrifice for sin, and for transgression, and for consecration, and for the victims of peace offerings,
Hii ndiyo sheria ya sadaka ya kuteketezwa, ya sadaka ya nafaka, ya sadaka ya dhambi, ya sadaka ya hatia, ya sadaka ya kuweka wakfu, na ya dhabihu, ya sadaka za amani,
38 which the Lord appointed to Moses on mount Sinai, when he commanded the sons of Israel to offer their oblations to the Lord in the desert of Sinai.
ni sheria ambazo Yahweh alizitoa kwa Musa kwenye Mlima Sinai siku aliyowaamru watu wa Israeli kutoa dhabihu zao kwa Yahweh katika jangwa la Sinai.'”

< Leviticus 7 >