< Leviticus 21 >

1 The Lord also said to Moses: Speak to the priests, the sons of Aaron, and you shall say to them: Do not allow a priest to be contaminated by the death of his citizens,
Bwana akamwambia Mose, “Sema na makuhani, wana wa Aroni, uwaambie: ‘Kamwe kuhani asijitie unajisi kwa utaratibu wa kiibada kwa ajili ya mtu wake yeyote anayekufa,
2 except only by his blood-relatives and near-relatives, that is, by a father or mother, or by a son or daughter, or also a brother,
isipokuwa jamaa wake wa karibu, kama vile mama yake au baba yake, mwanawe au binti yake, ndugu yake,
3 or a virgin sister, who is not married to a husband.
au dada yake asiyeolewa ambaye anamtegemea kwa kuwa hana mume, kwa ajili ya hao aweza kujitia unajisi.
4 But not even by the leader of his people shall he be contaminated.
Kamwe asijitie unajisi mwenyewe kutokana na wale watu ambao anahusiana nao kwa kuoana, na hivyo kujitia unajisi.
5 Neither shall they shave their head or their beard, and they shall not make incisions in their flesh.
“‘Kamwe makuhani wasinyoe nywele za vichwa vyao wala wasinyoe pembeni mwa ndevu zao, au kuweka chale kwenye miili yao.
6 They shall be holy to their God, and they shall not pollute his name. For they offer the incense of the Lord and the bread of their God, and because of this they shall be holy.
Lazima wawe watakatifu kwa Mungu wao, na kamwe wasilinajisi jina la Mungu wao. Kwa sababu ndio wanaotoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana, chakula cha Mungu wao, hivyo lazima wawe watakatifu.
7 They shall not take as a wife a promiscuous woman, or a prostitute, or her who has been repudiated by her husband. For they are consecrated to their God,
“‘Kamwe wasioe wanawake waliojinajisi kwa ukahaba, au waliopewa talaka na waume wao, kwa sababu makuhani ni watakatifu kwa Mungu wao.
8 and they offer the bread of the presence. Therefore, let them be holy, for I also am holy: the Lord, who sanctifies them.
Waoneni kuwa watakatifu, kwa sababu ndio wanaotoa chakula cha Mungu wenu. Kumbukeni kuwa ni watakatifu, kwa sababu Mimi Bwana ni mtakatifu, Mimi niwafanyaye ninyi kuwa watakatifu.
9 If the daughter of a priest will have been taken into prostitution, and will have violated the name of her father, she shall be consumed by fire.
“‘Ikiwa binti wa kuhani anajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamwaibisha baba yake; lazima achomwe kwa moto.
10 The high priest, that is, the priest who is the greatest among his brothers, upon whose head the oil of anointing has been poured, and whose hands have been consecrated for the priesthood, and who has been vested with the holy vestments: he shall not expose his head; he shall not rend his vestments.
“‘Kuhani mkuu, yule miongoni mwa ndugu zake ambaye amekwisha kutiwa mafuta kwa kumiminiwa juu ya kichwa chake, na ambaye amewekwa wakfu kuvaa mavazi ya ukuhani, kamwe asiache nywele zake bila kufunikwa, wala asirarue nguo zake.
11 And he shall not enter to any dead body whatsoever; likewise, not even by his father or mother shall he be contaminated.
Kamwe asiingie mahali palipo maiti ndani. Kamwe asijitie unajisi, hata kwa ajili ya baba yake au mama yake,
12 Neither shall he exit from the holy places, lest he pollute the Sanctuary of the Lord. For the oil of the holy anointing of his God is upon him. I am the Lord.
wala asiondoke mahali patakatifu pa Mungu wake au kupanajisi, kwa sababu amewekwa wakfu kwa mafuta ya Mungu wake. Mimi ndimi Bwana.
13 He shall take a virgin as his wife.
“‘Mwanamke kuhani atakayemwoa lazima awe bikira.
14 But a widow, or one who has been repudiated or defiled, or also a mistress, he shall not accept, but only a maiden from among his own people.
Kamwe asimwoe mjane, au mwanamke aliyepewa talaka, wala mwanamke aliyejinajisi kwa ukahaba, bali atamwoa tu bikira kutoka miongoni mwa watu wake,
15 He shall not mingle the stock of his family with the common people of his nation. For I am the Lord, who sanctifies him.
na hivyo hatawatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. Mimi ndimi Bwana, nimfanyaye mtakatifu.’”
16 And the Lord spoke to Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
17 Say to Aaron: A man from your offspring, throughout their families, who has a blemish, shall not offer the bread to his God.
“Mwambie Aroni: ‘Kwa vizazi vijavyo, hakuna mzao wako mwenye dosari atakayekaribia kutoa chakula cha Mungu wake.
18 Neither shall he approach to minister to him: if he is blind, if he is lame, if he is small, or large, or has a crooked nose,
Hakuna mtu mwenye dosari yoyote awezaye kukaribia: hakuna mtu aliye kipofu au kiwete, au aliyeharibika uso au asiye na viungo kamili,
19 if his foot or hand is broken,
hakuna mtu mwenye mguu au mkono uliolemaa,
20 if he has a bulging back or bleary eyes, or if he has a white spot in his eye, or a chronic scab, or a skin disease on his body, or a hernia.
au mwenye kibiongo au aliyedumaa, au aliye na tatizo la macho, au aliye na uvimbe wenye usaha au majipu, au aliyehasiwa.
21 Anyone from the offspring of Aaron, the priest, who has a blemish, shall not approach to offer sacrifices to the Lord, nor the bread to his God.
Hakuna mzao wa kuhani Aroni mwenye kilema chochote atakayekaribia kutoa sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Kama ana kilema, kamwe asikaribie kutoa chakula cha Mungu wake.
22 Nevertheless, he shall eat from the loaves which are offered in the Sanctuary.
Anaweza kula chakula kitakatifu sana cha Mungu wake, pia hata chakula kitakatifu.
23 But even so, he may not enter within the veil, nor approach to the altar. For he has a blemish, and he must not contaminate my Sanctuary. I am the Lord, who sanctifies them.
Lakini kwa sababu ya kilema chake, kamwe asikaribie karibu na pazia wala kukaribia madhabahu, asije akanajisi mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye watakatifu.’”
24 Therefore, Moses spoke to Aaron, and to his sons, and to all of Israel, everything that had been commanded to him.
Basi Mose akamwambia Aroni jambo hili na wanawe, pamoja na Waisraeli wote.

< Leviticus 21 >