< Leviticus 15 >

1 And the Lord spoke to Moses and Aaron, saying:
Yahwe alizungumza na Musa na Haruni, akisema,
2 Speak to the sons of Israel, and say to them: The man who undergoes a flow of seed shall be unclean.
“Waambie watu wa Israeli, na sema kwao, 'Wakati mtu yeyote kisonono kimemwathiri mwili wake unatoa ugiligili, anakuwa najisi.
3 And then he shall be judged subject to this fault, if a filthy fluid, at each moment, adheres to his flesh and gathers there.
Unajisi wake unatokana na athari ya kisonono. Iwe mwili wake unatoa ugiligili au umekoma, huo ni unajisi.”
4 Every bed on which he sleeps shall be unclean, and every place where he sits.
Kitanda chochote anachokilalia kitakuwa najisi, na kila kitu ambacho anakaa juu yake kitakuwa najisi.
5 If any man has touched his couch, he shall wash his clothes, and having washed with water, he shall be unclean until evening.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na awe amenajisika mpaka jioni.
6 If he will have sat where that man has sat, he shall also wash his clothes, and having washed with water, he shall be unclean until evening.
Yeyote anayekaa katika kitu chochote ambacho mtu ambaye ameathiriwa na kisonono alikaa, mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
7 Whoever has touched his flesh shall wash his clothes, and having washed with water, he shall be unclean until evening.
Na yeyote anayegusa mwili wa ambaye ameathirika na kisonono lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na awe najisi hadi jioni.
8 If such a man has cast his spittle upon him who is clean, he shall wash his clothes, and having washed with water, he shall be unclean until evening.
Kama mtu ambaye anaona majimaji kama hayo kwa mtu fulani ambaye ametakasika, ndipo mtu huyo lazima afue nguo zake na aoge kwenye maji, na atakuwa najisi hata jioni.
9 The saddle on which he has sat shall be unclean.
Tandiko lolote ambalo ambaye anamajimaji ya kisonono atalikalia litakuwa najisi.
10 And whatever has been under him who has undergone a flow of seed shall be polluted until evening. Whoever carries any of these things shall wash his clothes, and having washed with water, he shall be unclean until evening.
Yeyote anayegusa kitu chochote kilichokuwa chini ya mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni, na yeyote anayebeba vitu hivyo lazima afue nguo zake na aoge katika maji; atanajisika mpaka jioni.
11 All whom such a one has touched, not having washed his hands before, shall wash his clothes, and having washed with water, he shall be unclean until evening.
Ambaye anamajimaji kama hayo akimgusa kabla kwanza ya kuosha kwa maji safi mikono yake, mtu aliyeguswa lazima afue nguo zake na aoge katika maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
12 If he has touched an earthen vessel, it shall be broken. But if it is a wooden vessel, it shall be washed with water.
Chungu chochote cha udongo ambacho ambaye anamajimaji kama hayo akigusa lazima kivunjwe, na kila chombo cha mti lazima kioshwe na maji safi.
13 If he who suffers from this affliction will have been healed, he shall number seven days after his cleansing, and having washed his clothes and his entire body in living water, he shall be clean.
Wakati mwenye kisonono anapotakaswa katika kisonono chake, ndipo lazima ahesabu kwaajili yake siku saba kwaajili ya kutakasika kwake; ndipo afue nguo na aoshe mwili wake kwenye maji yatiririkayo. Ndipo atakuwa safi.
14 Then, on the eighth day, he shall take two turtledoves or two young pigeons, and he shall advance, in the sight of the Lord, toward the door of the tabernacle of the testimony, and he shall give these to the priest,
Katika siku ya nane lazima achukue njiwa wawili au kinda mbili za njiwa na aje mbele za Yahwe pakuingilia kwenye hema ya mkutano; pale lazima atoe hao ndege kwa kuhani.
15 who shall offer one for sin, and the other as a holocaust. And he shall pray for him before the Lord, so that he may be cleansed from the flow of his seed.
Lazima kuhani awatoe, moja kama sadaka ya dhambi na nyingine kama ya kuteketezwa, na kuhani lazima afanye upatanisho kwaajili yake mbele za Yahwe kwaajili ya kisonono chake.
16 A man from whom the seed of sexual intercourse goes out shall wash his entire body with water, and he shall be unclean until evening.
Kama mtu yeyote ametokwa na shahawa, ndipo lazima aoge mwili wake wote katika maji; atanajisika mpaka jioni.
17 The garment or skin which he will have, he shall wash with water, and it shall be unclean until evening.
Kila vazi au ngozi ambayo juu yake kuna shahawa lazama paoshwe kwa maji; itakuwa najisi mpaka jioni.
18 The woman with whom he has had sexual intercourse shall be washed with water, and she shall be unclean until evening.
Na kama mwanamke na mwanaume watalala pamoja na kunakutokwa kwa shahawa kwenda kwa mwanamke, lazima wote wawili waoge katika maji; watakuwa najisi mpaka jioni.
19 The woman who, at the return of the month, undergoes the flow of blood shall be separated for seven days.
Mwanamke anapokuwa kwenye hedhi, ataendelea kunajisika kwa siku saba, na yeyote anayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
20 All who will touch her shall be unclean until evening.
Chochote anacholala juu yake wakati wa hedhi kitakuwa najisi; kila kitu ambacho anakalia kitakuwa pia najisi.
21 And everything on which she sleeps or sits, in the days of her separation, shall be polluted.
Yeyote anayegusa kitanda chake lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
22 Whoever will have touched her bed shall wash his clothes, and having washed himself with water, he shall be unclean until evening.
Yeyote anayegusa chochote ambacho amekikalia lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; mtu huyo anakuwa najisi mpaka jioni.
23 Anyone who will have touched any item on which she has sat shall wash his clothes, and having washed himself with water, he shall be polluted until evening.
Iwe juu ya kitanda au kitu chochote juu ya popote atakapokaa, kama akikigusa, mtu huyo atakuwa najisi mpaka jioni.
24 If a man has sexual intercourse with her in the time of her monthly flow of blood, he shall be unclean for seven days, and every bed on which he sleeps shall be polluted.
Kama mwanaume yeyote akilala naye, na unajisi wa mwanamke ukamgusa, atakuwa amenajisika siku saba. Kila kitanda ambacho anakilalia mwanaume huyo kitanajisika.
25 The woman who undergoes a flow of blood many days beyond her time of menstruation, or whose blood does not cease to flow after the menstrual blood, as long as she is subject to this affliction, she shall be unclean, just as if she were in her time of menstruation.
Kama mwanamke ametokwa damu kwa siku nyingi ambayo siyo kipindi cha hedhi yake, au ikitoka zaidi ya kipindi chake cha hedhi, wakati wote wa siku za kunajisika, atakuwa kama alikuwa kwenye siku zake za hedhi. Yeye ni najisi.
26 Every bed on which she sleeps, and every item on which she sits, shall be polluted.
Kila kitanda anachokilalia wakati wote wa kutokwa damu itakuwa kwake sawa tu kama kitanda anacholalia wakati wa hedhi, na kila kitu ambacho anakalia kitakuwa najisi, kama tu unajisi wa hedhi yake.
27 Whoever will have touched these shall wash his clothes, and having washed himself with water, he shall be unclean until evening.
Na yeyote anayegusa kitu kati ya vitu hivyo atakuwa najisi; lazima yeye afue nguo zake na aoge mwenyewe kwenye maji, na atakuwa amenajisika mpaka jioni.
28 If the blood has stopped and has ceased to flow, she shall number seven days for her purification,
Lakini kama mwanamke ametakasika katika kutokwa na damu, ndipo atahesabu kwaajili yake siku saba, baada ya hizo atakuwa safi.
29 and on the eighth day she shall offer for herself, to the priest, two turtledoves or two young pigeons, at the door of the tabernacle of the testimony.
Katika siku ya nane atachukua kwake njiwa wawili au kinda wawili wa njiwa na atawaleta kwa kuhani pakuingilia hema ya mkutano.
30 And he shall offer one for sin, and the other as a holocaust, and he shall pray for her before the Lord, and for the flow of her uncleanness.
Huyo kuhani atatoa ndege mmoja kama sadaka ya dhambi na mwingine kama sadaka ya kuteketezwa, na atafanya upatanisho kwaajili ya huyo mbele ya Yahwe kwaajili unajisi wa mwanamke atokwaye damu.
31 Therefore, you shall teach the sons of Israel to be cautious of uncleanness, so that they may not die in their filth, when they will have polluted my tabernacle, which is among them.
Hivi ndivyo lazima uwatenge watu wa Israeli katika unajisi wao, hivyo hawatakufa tokana na unajisi wao, kwa kuchafua hema langu, ambapo naishi kati yao.
32 This is the law of him who undergoes a flow of seed, or who is polluted by sexual intercourse,
Huu ndio utaratibu kwa kila ambaye anakisonono, kwaajili kila mwanaume ambaye shahawa yake inatoka na inamfanya kuwa najisi,
33 and of her who is separated in the time of menstruation, or who has a continual flow of blood, and of the man who sleeps with her.
kwaajili ya mwanamke ambaye yuko katika kipindi cha hedhi, kwaajili ya yeyote aliye na kisonono, awe mwanaume au mwanamke, na kwaajili ya yeyote anayelala na mwanamke najisi.

< Leviticus 15 >