< Joshua 8 >

1 Then the Lord said to Joshua: “You should not fear, and you should not dread. Take with you the entire multitude of fighters, and rising up, ascend to the town of Ai. Behold, I have delivered into your hand its king and people, and the city and the land.
Yahweh akamwambia Yoshua, “Usiogope; usivunjike moyo. Chukua pamoja nawe watu wa vita. Pandeni kwenda Ai. Tazama nimemtia mkononi mwako mfalme wa Ai, watu wake, mji wake na nchi yake.
2 And you shall do to the city of Ai, and to its king, just as you did to Jericho, and to its king. Yet truly, the spoils, and all the living things, you shall plunder for yourselves. Set an ambush against the city behind it.”
Mtafanya hivyo pia huko Ai na mfalme wake kama mlivyofanya kwa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mtachukua nyara na mifugo kwa ajili yenu. Pangeni mashambulizi ya uviziaji nyuma ya mji.”
3 And Joshua rose up, and the entire army of warriors with him, so that they might ascend against Ai. And he sent thirty thousand elect strong men in the night.
Basi Yoshua aliinuka na akawachukua kwenda Ai watu wote wa vita. Kisha Yoshua akachagua watu elfu thelathini - wenye nguvu na ujasiri - na aliwatuma waende wakati wa usiku.
4 And he instructed them, saying: “Set an ambush behind the city. You shall withdraw not far away, and let everyone be prepared.
Aliwaamuru, “Tazama, mtalala katika hali ya mashambulizi ya uviziaji dhidi ya mji, kwa nyuma yake. Usiende mbali sana na mji, lakini ninyi nyote muwe tayari.
5 But I and the remainder of the multitude that is with me will approach from the opposite side of the city. And when they come out against us, we will flee and turn our backs, just as we did before,
Mimi pamoja na watu wote walio pamoja nami tutaukaribia mji. Na wakati watakapokuja kutushambulia sisi, tutawakimbia kama tulivyofanya hapo mwanzo.
6 until, pursuing us, they are drawn away from the city. For they will think that we are fleeing as before.
Watatoka nje watukimbize mpaka hapo tutakapokuwa tumewavuta mbali sana na mji, watasema, “Wanatukimbia kama walivyofanya mara ya mwisho.' Hivyo tutawakimbia na kwenda mbali.
7 Then, while we are fleeing and they are pursuing, you shall rise up from the ambush, and you shall lay waste to the city. And the Lord your God will deliver it into your hands.
Kisha mtapanda kutoka sehemu mliyojificha, na mtauteka mji. Yahweh Mungu wenu atawapa mkononi mwenu.
8 And when you have seized it, set it on fire. And you shall do all that I have ordered.”
Tazama nimewaamuru, mtakapouteka mji, mtauchoma moto. Mtayafanya haya wakati mtakapotii agizo lililotolewa katika neno la Yahweh.”
9 And he sent them away, and they traveled to the place of the ambush, and they settled between Bethel and Ai, toward the western region of the city of Ai. But Joshua remained for that night in the midst of the people.
Yoshua akawatuma, na wakaenda sehemu ya uviziajia, na wakajificha kati ya Betheli na Ai sehemu ya magharibi ya Ai. Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku ule.
10 And rising at first light, he reviewed his troops, and he went up, with the elders at the front of the army, surrounded by an auxiliary of fighters.
Yoshua aliamka asubuhi na mapema na akawaandaa tayari wanajeshi wake, Yoshua na wazee wa Israeli walishambuliwa watu wa Ai.
11 And when they had arrived, and had ascended from the opposite side of the city, they stood toward the northern region of the city. And there was a valley in the middle, between them and the city.
Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda na kuukaribia mji. Walisogea karibu na mji na wakapiga kambi sehemu ya kasikazini mwa Ai. Kulikuwa na bonde kati yao na Ai.
12 Now he had chosen five thousand men, and he had positioned them in ambush between Bethel and Ai, at the western part of the same city.
Alichukua watu wapatao elfu tano hivi na akawaweka katika hali ya kuvizia katika upande wa magharibi mwa mji kati ya Betheli na Ai.
13 Yet truly, all the remainder of the army was arranged in a line to the north, so that the very end of that multitude reached to the western region of the city. Then Joshua went out that night, and he stood in the middle of the valley.
Waliwapanga wanajeshi wote, jeshi kuu katika upande wa kasikazini mwa mji, na walinzi wa nyuma upande wa magharibi mwa mji. Yoshua alilala bondeni usiku ule.
14 And when the king of Ai had seen this, he hurried in the morning, and he went out with the entire army of the city. And he arranged them in a line opposite the desert, not knowing that an ambush lay hidden behind his back.
Na ilikuwa alipoona hilo mfalme wa Ai, yeye pamoja na jeshi lake, waliamka asubuhi na mapema na walitoka kwa haraka kwenda kuwashambulia Israeli katika eneo linalokabili bonde la Mto Yordani. Hakujua kuwa kulikuwa na shambulizi la kuvizia lilikuwa linasubiria kushambulia kutokea kwa nyuma ya mji.
15 Yet truly, Joshua, and all of Israel, withdrew from the place, pretending to be afraid, and fleeing along the way of the wilderness.
Yoshua na Waisraeli wote walikubali wenyewe kushindwa mbele yenu, na wakakimbia kuelekea nyikani.
16 And they pursued them, shouting together and encouraging one another. And when they had withdrawn from the city,
Watu wote waliokuwa kwenye mji waliitwa kwa pamoja waende mbele yao, na walienda mbele ya Yoshua na kwa jinsi hiyo walivutwa mbali na mji.
17 and indeed not one remained in the city of Ai and of Bethel who did not pursue after Israel, (leaving the towns open after they had rushed out, )
Hapakuwa na mtu mme aliyesalia Ai na Betheli ambaye alikuwa hajaenda nje kuwafuatilia waisraeli. Na walipokuwa wanawafuatilia Waisraeli, Wakatoka na waliuacha mji wazi.
18 the Lord said to Joshua: “Lift up the shield that is in your hand, toward the city of Ai. For I will deliver it to you.”
Yahweh akamwambia Yoshua, “Nyosha mkuki huo ulio mkononi mwako kuelekea Ai, kwa kuwa nitaitia Ai mikononi mwako.” Yoshua akaunyosha mkuki uliokuwa mkononi mwake kuuelekea mji.
19 And when he had lifted up the shield toward the city, the ambush, which lay hidden, rose up quickly. And advancing to the city, they seized it, and set it on fire.
Wanajeshi waliojificha katika hali ya kuvizia walitoka upesi katika eneo lao mara tu alipounyosha mkono wake. Walikimbia mbio na kuuingia mji na kuuteka. Na kwa haraka wakauchoma moto mji.
20 Now the men of the city who were pursuing Joshua, looking back and seeing the smoke of the city rising up even to heaven, were no longer able to flee in one direction or another, especially since those who had pretended to flee, and who were heading toward the wilderness, had turned back very strongly against those who were pursuing them.
Watu wa Ai waligeuka na kuangalia nyuma. Waliona moshi kutoka katika mji ukipanda kwenda angani, na hawakuweza kutoroka kwa njia hii au ile. Kwa kuwa wanajeshi wa Israelei waliokuwa wamekimbia katika nyika, sasa walirudi kuwakabili wale waliokuwa wanawafuatilia.
21 And Joshua, and all of Israel, seeing that the city had been captured, and that the smoke of the city was ascending, returned and struck down the men of Ai.
Na wakati Yoshua na Israeli wote walipoona kuwa wale watu wa kuvizia wameuteka mji kwa ule moshi uliokuwa ukipanda, waligeuka nyuma na kuwaua watu wa Ai.
22 Then too, those who had seized and set the city on fire, departing from the city toward their own men, began to strike the enemies in the middle. Therefore, since the adversaries were cut off from both sides, none of so great a multitude was saved.
Na wanajeshi wengine wa Israeli, wale waliokuwa wameingia ndani ya mji, walitoka nje ili kuwashambulia. Hivyo, watu wa Ai walikamatwa katikati ya majeshi ya Israeli, baadhi katika upande huu na wengine katika upande ule.
23 Also, they apprehended the king of the city of Ai, alive, and they brought him before Joshua.
Lakini walimhifadhi mfalme wa Ai, ambaye walimteka akiwa hai, na kisha wakamleta kwa Yoshua.
24 And so, after all were slain who had pursued Israel fleeing toward the wilderness, and after they fell by the sword in the same place, the sons of Israel returned and struck the city.
Ilikuwa baada ya Israeli walipokuwa wamemaliza kuuwaua wenyeji wote wa Ai katika uwanda kariibu na nyika mahali walipowafuata, na baada ya wao wote, hata yule wa mwisho, walipokuwa wamekwisha kulala kwa ncha ya upanga, Waisraeli wote walirudi Ai. Waliuteka mji kwa ncha ya upanga.
25 Now there were twelve thousand persons who had fallen on the same day, from man even to woman, the entire city of Ai.
Wale wote walikufa siku hiyo walikuwa watu elfu kumi na mbili elfu, wanaume na wanawake, wote ni watu wa Ai.
26 Truly Joshua did not draw back his hand, which he had stretched out on high, keeping hold of the shield until all the inhabitants of Ai were put to death.
Yoshua hakuukunja mkono wake ambao alikuwa ameunyosha huku akishikilia mkuki wake, mpaka pale alipowateketeza kabisa watu wote wa Ai.
27 Then the sons of Israel divided among themselves the cattle and the plunder of the city, just as the Lord had instructed Joshua.
Waisraeli walichukua tu wanyama na nyara kutoka katika mji kwa ajili yao wenyewe, kama Yahweh alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
28 And he set fire to the city, and he caused it to be a perpetual tomb.
Yoshua aliichoma Ai na kuigeuza kuwa kichuguu cha mapango. Ni mahali palipoachwa ukiwa hata leo.
29 Also, he suspended the king on a gallows, until evening and the setting of the sun. And Joshua instructed, and they took down his dead body from the hanging tree. And they cast it at the very entrance of the city, gathering a great pile of stones upon it, which remains even to the present day.
Alimtundika mfalme wa Ai juu ya mti mpaka jioni. Na jua lilipokuwa linaenda kuzama, Yoshua aliwaagiza na wakautoa mwili wa mfalme wakaushusha chini ya mti na kuutupa mbele ya malango ya mji. Huko wakaweka kichuguu kikubwa cha mawe juu yake. Kichuguu hicho kimebaki huko hata leo.
30 Then Joshua built an altar to the Lord, the God of Israel, on Mount Ebal,
Kisha Yoshua akajenga madhabahu kwa Yahweh, Mungu wa Israeli katika Mlima wa Ebali,
31 just as Moses, the servant of the Lord, had instructed to the sons of Israel, and this was written in the book of the law of Moses: truly, an altar of uncut stones, which iron has not touched. And he offered holocausts upon it to the Lord, and he immolated victims as peace-offerings.
kama vile Musa mtumishi wa Yahweh alivyowaagiza watu wa Israeli, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa: “Madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna mtu yeyote aliyetumia zana ya chuma.” Na allimtolea Yahweh sadaka ya kuteketezwa juu yake na wakatoa sadaka ya amani.
32 And he wrote on the stones, the Deuteronomy of the law of Moses, which he had set in order before the sons of Israel.
Na huko aliandika juu ya mawe nakala ya sheria za Musa mbele ya watu wa Israeli.
33 Then all the people, and those greater by birth, and the commanders and judges were standing on both sides of the ark, in the sight of the priests who were carrying the ark of the covenant of the Lord, with both the new arrival and the native born, one half part of them beside Mount Gerizim, and one half beside Mount Ebal, just as Moses, the servant of the Lord, had instructed. And first, certainly, he blessed the people of Israel.
Waisraeli wote, wazee wao, maafisa, na waamuzi wao walisimama katika sehemu mbili za sanduku mbele ya makuhani na Walawi ambao hulibeba sanduku la Agano la Yahweh - wageni pamoja na wazalia, nusu yao walisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu walisimama mbele ya Mlima Ebali. Waliwabariki watu wa Israeli kama Musa mtumishi wa Yahweh alivyowaagiza hapo mwanzo.
34 After this, he read all the words of the blessing and the cursing, and all the things that were written in the book of the law.
Baada ya hayo, Yoshua alisoma maneno yote ya sheria, baraka na laana, kama zilivyoandikwa katika kitabu cha sheria.
35 He left nothing untouched out of those things that Moses had ordered, and he repeated everything before the entire multitude of Israel, with the women and the little ones, and the new arrivals who were staying among them.
Halikusalia hata neno moja katika yote ambayo Musa alimwagiza Yoshua ambalo halikusomwa mbele ya kusanyiko la Waisraeli lilojumuisha wanawake, watoto wadogo na wageni walioishi miongoni mwao.

< Joshua 8 >