< Joshua 21 >
1 And the leaders of the families of Levi approached Eleazar, the priest, and Joshua, the son of Nun, and the rulers of the extended families of each of the tribes of the sons of Israel.
Basi viongozi wa jamaa ya Walawi, wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa nyingine za makabila ya Israeli
2 And they spoke to them at Shiloh, in the land of Canaan, and they said, “The Lord instructed, by the hand of Moses, that cities should be given to us as habitations, with their suburbs to nourish our cattle.”
huko Shilo katika Kanaani na kuwaambia, “Bwana aliamuru kupitia Mose kuwa mtupe miji ya kuishi yenye sehemu za malisho kwa mifugo yetu.”
3 And so the sons of Israel gave cities and their suburbs from their possessions, in accord with the order of the Lord.
Hivyo kama vile Bwana alivyoamuru, Waisraeli wakawapa Walawi miji ifuatayo pamoja na sehemu zake za malisho kutoka urithi wao wenyewe.
4 And the lot went out for the family of Kohath, of the sons of Aaron, the priest, from the tribes of Judah and Simeon and Benjamin: thirteen cities.
Kura ya kwanza ikaangukia Wakohathi, ukoo kwa ukoo. Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Aroni walipewa miji kumi na mitatu kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini.
5 And to the remainder of the sons of Kohath, that is, to the Levites who were left over, there went, from the tribes of Ephraim and Dan, and from the one half tribe of Manasseh, ten cities.
Wazao wengine waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za makabila ya Efraimu, Dani na nusu ya Manase.
6 And next the lot went out to the sons of Gershon, so that they would receive, from the tribes of Issachar and Asher and Naphtali, and from the one half tribe of Manasseh at Bashan: the number of thirteen cities.
Wazao wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kutoka koo za makabila ya Isakari, Asheri, Naftali na nusu ya Manase huko Bashani.
7 And to the sons of Merari, by their families, from the tribes of Reuben and Gad and Zebulun, there went twelve cities.
Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
8 And so the sons of Israel gave cities and their suburbs to the Levites, just as the Lord instructed by the hand of Moses, distributing to each by lot.
Kwa hiyo Waisraeli wakawapa Walawi miji hii pamoja na sehemu zake za malisho, kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kupitia kwa Mose.
9 From the tribes of the sons of Judah and Simeon, Joshua gave cities, whose names are these:
Kutoka makabila ya Yuda na Simeoni waligawa miji ifuatayo kwa majina
10 to the sons of Aaron, of the families of Kohath of the stock of Levi, (for the first lot went out for them, )
(miji hii walipewa wazao wa Aroni ambao walitokana na koo za Wakohathi wa Walawi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
11 the city of Arba, the father of Anak, which is called Hebron, on the mountain of Judah, and its surrounding suburbs.
Waliwapa Kiriath-Arba (yaani Hebroni), pamoja na sehemu zake za malisho zilizoizunguka, katika nchi ya vilima ya Yuda. (Arba alikuwa baba wa Anaki.)
12 Yet truly, the fields and its villages he had given to Caleb, the son of Jephunneh, as a possession.
Lakini mashamba na vijiji vilivyozunguka mji mkubwa walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.
13 Therefore, he gave to the sons of Aaron the priest, Hebron as a city of refuge, as well as its suburbs, and Libnah, with its suburbs,
Kwa hiyo wazao wa kuhani Aroni wakapewa Hebroni (mji mkuu wa makimbilio kwa ajili ya yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji), Libna,
14 and Jattir, and Eshtemoa,
Yatiri, Eshtemoa,
16 and Ain, and Juttah, and Beth-shemesh, with their suburbs: nine cities from two tribes, just as has been said.
Aini, Yuta na Beth-Shemeshi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji tisa kutoka kwa makabila haya mawili.
17 Then, from the tribe of the sons of Benjamin, he gave Gibeon, and Geba,
Kutoka kabila la Benyamini wakawapa Gibeoni, Geba,
18 and Anathoth, and Almon, with their suburbs: four cities.
Anathothi na Almoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
19 All the cities together of the sons of Aaron, the priest, were thirteen, with their suburbs.
Miji yote waliyopewa makuhani, wazao wa Aroni, ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
20 Yet truly, the remainder of the families of the sons of Kohath, of the stock of Levi, were given this possession:
Koo nyingine za Wakohathi, ambao pia ni Walawi, walipewa miji kutoka kabila la Efraimu:
21 from the tribe of Ephraim, Shechem, one of the cities of refuge, with its suburbs, on mount Ephraim, and Gezer,
Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri,
22 and Kibzaim, and Beth-horon, with their suburbs, four cities;
Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
23 and from the tribe of Dan, Elteke and Gibbethon,
Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni,
24 and Aijalon and Gath-Rimmon, with their suburbs, four cities;
Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
25 then, from the one half tribe of Manasseh, Taanach and Gath-Rimmon, with their suburbs, two cities.
Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili.
26 All the cities were ten, with their suburbs; these were given to the sons of Kohath, of the lesser degree.
Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki.
27 Likewise, to the sons of Gershon, of the stock of Levi, from the one half tribe of Manasseh, went Golan in Bashan, one of the cities of refuge, and Bosra, with their suburbs, two cities;
Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;
28 also, from the tribe of Issachar, Kishion, and Daberath,
kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi,
29 and Jarmuth, and Engannim, with their suburbs, four cities;
Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
30 then, from the tribe of Asher, Mishal and Abdon,
kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni,
31 and Helkath and Rehob, with their suburbs, four cities;
Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
32 likewise, from the tribe of Naphtali, Kedesh in Galilee, one of the cities of refuge, and Hammoth-Dor, and Kartan, with their suburbs, three cities.
Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.
33 All the cities of the families of Gershon were thirteen, with their suburbs.
Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
34 Then, to the sons of Merari, Levites of the lesser degree, by their families, were given, from the tribe of Zebulun, Jokneam and Kartah,
Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta,
35 and Dimnah and Nahalal, four cities with their suburbs;
Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
36 from the tribe of Reuben, beyond the Jordan, opposite Jericho, Bezer in the wilderness, one of the cities of refuge, Misor and Jazer, and Jethson and Mephaath, four cities with their suburbs;
kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa,
37 from the tribe of Gad, Ramoth of Gilead, one of the cities of refuge, and Mahanaim and Heshbon and Jazer, four cities with their suburbs.
Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,
Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
40 All the cities of the sons of Merari, by their families and extended families, were twelve.
Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.
41 And so all the cities of the Levites, in the midst of the possession of the sons of Israel, were forty-eight,
Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho.
42 with their suburbs, each distributed by families.
Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote.
43 And the Lord God gave to Israel all the land that he had sworn he would deliver to their fathers. And they possessed it, and they lived in it.
Kwa hiyo Bwana akawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo.
44 And he gave them peace with all the surrounding nations. And none of their enemies dared to stand against them; instead, they were brought under their sovereignty.
Bwana akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
45 Indeed, not so much as one word that he had promised to provide for them was left empty; instead, everything was fulfilled.
Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri ya Bwana kwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.