< Joshua 18 >

1 And all the sons of Israel gathered together at Shiloh, and there they stationed the Tabernacle of the Testimony. And the land was subjected to them.
Kusanyiko lote la Waisraeli likakusanyika huko Shilo na kusimamisha Hema la Kukutania. Nchi ikawa chini ya utawala wao,
2 But there remained seven tribes of the sons of Israel which had not yet received their possessions.
lakini palikuwa bado makabila saba ya Israeli ambayo yalikuwa hayajapokea urithi wao.
3 And Joshua said to them: “For how long will you draw back in idleness, and not enter to possess the land, which the Lord, the God of your fathers, has given to you?
Hivyo Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtasubiri hata lini ili kuingia kumiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa?
4 Select three men from each tribe, so that I may send them, and they may go forth and circle through the land, and may describe it according to the number of each multitude, and may bring back to me what they have written down.
Chagueni watu watatu kutoka kwenye kila kabila. Nitawatuma hao watu kukagua hiyo nchi na kuniandikia mapendekezo ya mgawanyo wa urithi wa kila kabila. Nao watanirudia.
5 Divide the land for yourselves into seven parts. Let Judah be its bounds on the southern side, and the house of Joseph to the north.
Mtaigawanya hiyo nchi katika sehemu saba. Yuda atabaki katika eneo lake upande wa kusini na nyumba ya Yosefu katika nchi yake upande wa kaskazini.
6 The land that is in the middle, between these, write it down in seven parts. And you shall come to me, so that I may cast lots for you about this, before the Lord your God.
Baada ya kuandika maelezo ya hizo sehemu saba za nchi, yaleteni kwangu, nami nitawapigia kura kwa kura mbele za Bwana Mungu wetu.
7 But there is no portion among you for the Levites. Instead, the priesthood of the Lord is their inheritance. And Gad and Reuben, and the one half tribe of Manasseh, have already received their possessions beyond the Jordan in the eastern region, which Moses, the servant of the Lord, gave to them.”
Hata hivyo, Walawi hawatakuwa na sehemu miongoni mwenu, kwa maana huduma ya ukuhani kwa Bwana ndio urithi wao. Nao Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapata urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, ambako Mose mtumishi wa Bwana aliwapa.”
8 And when the men had risen up, so that they might go out to describe the land, Joshua instructed them, saying, “Circle through the land, and describe it, and return to me, so that I may cast lots for you about this, before the Lord, in Shiloh.”
Watu hao walipokuwa wanaondoka kwenda kuandika vizuri kuhusu hiyo nchi, Yoshua akawaagiza, “Nendeni mkakague hiyo nchi na mwandike maelezo kuihusu. Kisha mrudi kwangu, nami nitawapigia kura hapa Shilo mbele za Bwana.”
9 And so they went out. And surveying it, they divided it into seven parts, writing it in a book. And they returned to Joshua, to the camp at Shiloh.
Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo.
10 And he cast lots before the Lord, at Shiloh, and he divided the land to the sons of Israel, in seven parts.
Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele za Bwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.
11 And the first lot went to the sons of Benjamin, by their families, so that they would possess the land between the sons of Judah and the sons of Joseph.
Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.
12 And their border toward the north was from the Jordan, continuing on, near the side of Jericho in the northern region, and from there, ascending toward the west to the mountains, and extending to the wilderness of Bethaven.
Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni.
13 And it continues to the south beside Luz, which is Bethel. And it descends into Ataroth-addar, at the mountain which is to the south of lower Beth-horon.
Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.
14 And it turns aside, circling toward the sea, to the south of the mountain which looks out toward Beth-horon, toward the southwest. And its exits are toward Kiriath-baal, which is also called Kiriath-jearim, a city of the sons of Judah. This is their region, toward the sea, in the west.
Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.
15 But to the south, the border goes on from the part of Kiriath-jearim toward the sea, and it continues as far as the Fountain of the waters of Nephtoah.
Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa.
16 And it descends to that part of the mountain which looks out toward the Valley of the sons of Hinnom. And it is opposite the northern region, in the furthest part of the Valley of the Rephaim. And it descends into Geennom, (that is, the Valley of Hinnom, ) near the side of the Jebusite toward the south. And it extends to the Fountain of Rogel,
Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli.
17 crossing from there to the north, and going out to En-Shemesh, that is, to the Fountain of the Sun.
Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni.
18 And it passes through to the hills that are opposite the region of the Ascent of Adummim. And it descends to Abenboen, that is, so the stone of Bohan, the son of Reuben. And it continues on, at the northern side, to the plains. And it descends into the flatlands.
Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba.
19 And it advances before Beth-hoglah, to the north. And its exits are to the north, opposite the bay of the very salty sea, in the southern region at the end of the Jordan,
Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.
20 which is its border to the east. This is the possession of the sons of Benjamin, with their borders all around, and by their families.
Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki. Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.
21 And their cities were: Jericho and Beth-hoglah and the Abrupt Valley,
Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo: Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi,
22 Beth-arabah and Zemaraim and Bethel,
Beth-Araba, Semaraimu, Betheli,
23 and Avvim and Parah and Ophrah,
Avimu, Para na Ofra,
24 the town of Ammoni, and Ophni, and Geba: twelve cities, and their villages;
Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
25 Gibeon and Ramah and Beeroth,
Gibeoni, Rama na Beerothi,
26 and Mizpeh and Chephirah and Mozah,
Mispa, Kefira, Moza,
27 and Rekem, Irpeel, and Taralah,
Rekemu, Irpeeli, Tarala,
28 and Zela, Haeleph, and Jebus, which is Jerusalem, Gibeah and Kiriath: fourteen cities, and their villages. This is the possession of the sons of Benjamin, according to their families.
Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake. Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.

< Joshua 18 >