< Joshua 12 >

1 These are the kings whom the sons of Israel struck down, and whose land they possessed beyond the Jordan, toward the rising of the sun, from the torrent Arnon as far as mount Hermon, with the entire eastern region that looks out toward the wilderness:
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
2 Sihon, the king of the Amorites, who lived at Heshbon, and who had dominion from Aroer, which is situated on the bank of the torrent Arnon, and the valley in the middle, and one half of Gilead, as far as the torrent Jabbok, which is the border of the sons of Ammon,
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 and from the wilderness, as far as the sea of Chinneroth toward the east, and to the Sea of the Wilderness, which is the very salty sea, to the eastern region, along the way that leads to Beth-jeshimoth, and from the southern region that lies under the descending slope of Pisgah,
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
4 to the border of Og, the king of Bashan; from the remnant of the Rephaim, who lived in Ashtaroth, and at Edrei, and who had dominion on mount Hermon, and at Salecah, and into all of Bashan, even to its limits;
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 with Geshur and Maacati, and one half of Gilead, these were the borders of Sihon, the king of Heshbon.
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Moses, the servant of the Lord, and the sons of Israel struck them down. And Moses delivered their land into the possession of the Reubenites, and the Gadites, and the one half tribe of Manasseh.
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 These are the kings of the land, whom Joshua and the sons of Israel struck down across the Jordan, toward the western region, from Baalgad in the field of Lebanon, as far as the mountain, part of which ascends to Seir. And Joshua delivered it as a possession to the tribes of Israel, to each one in their divisions,
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
8 both in the mountains and in the plains and fields. In the descending slopes, and in the wilderness, and in the south, there too was the Hittite and the Amorite, the Canaanite and the Perizzite, the Hivite and the Jebusite.
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
9 The king of Jericho, one; the king of Ai, which is beside Bethel, one;
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
10 the king of Jerusalem, one; the king of Hebron, one;
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
11 the king of Jarmuth, one; the king of Lachish, one;
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
12 the king of Eglon, one; the king of Gezer, one;
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
13 the king of Debir, one; the king of Geder, one;
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
14 the king of Hormah, one; the king of Arad, one;
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
15 the king of Libnah, one; the king of Adullam, one;
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
16 the king of Makkedah, one; the king of Bethel, one;
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
17 the king of Tappuah, one; the king of Hepher, one;
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
18 the king of Aphek, one; the king of Lasharon, one;
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
19 the king of Madon, one; the king of Hazor, one;
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
20 the king of Shimron, one; the king of Achshaph, one;
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
21 the king of Taanach, one; the king of Megiddo, one;
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
22 the king of Kadesh, one; the king of Jokneam of Carmel, one;
mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
23 the king of Dor and of the province of Dor, one; the king of the nations of Gilgal, one;
mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
24 the king of Tirzah, one. All the kings were thirty-one.
mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.

< Joshua 12 >