< Job 6 >

1 But Job, responding, said:
Kisha Ayubu akajibu:
2 I wish that my sins, for which I deserve wrath, and the calamity that I endure, were weighed out on a balance.
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 Compared to the sand of the sea, they would appear heavier, and so my words are full of sorrow.
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For the arrows of the Lord are in me, my spirit drinks of their indignation, and the terrors of the Lord are soldiers against me.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 Will the wild ass bray when he has grass? Or will the ox bellow when he stands before a full manger?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 Or can one eat bland food, which is not seasoned with salt? Or can anyone taste that which, if tasted, causes death?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 The things that my soul was unwilling to touch before, now, because of anguish, are my foods.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 Who will grant that my petition may arrive and that God may bestow on me what I expect,
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 and that he who, at first, had crushed me, will let loose his hand and cut me down?
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 And may this be my consolation, that in afflicting me with sorrow, although he might not be lenient with me, I still do not contradict the words of the Holy One.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 For what is my strength, that I may continue? Or what is my goal, so that I may act patiently?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 My strength is not the strength of stones, nor is my flesh made of bronze.
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Behold, there is no help for me in myself, and my loved ones also have withdrawn from me.
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 He who takes away mercy from his friend, abandons the fear of the Lord.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 My brethren have disregarded me, like a torrent that passes swiftly through the steep valleys.
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 Those who fear frost, snow will rush over them.
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 At that time, when they are scattered, they will perish, and when it becomes hot, they will be freed from their place.
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 The paths of their steps are entangled; they will walk in vain and will perish.
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 Consider the paths of Thema, the ways of Saba, and wait a little while.
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 They have been thrown into confusion, just as I had hoped; they have even come to me and are overwhelmed with shame.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 Now you have arrived, and merely by seeing my affliction, you are afraid.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Did I say: “Bring to me and give to me from your necessities?”
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 or, “Free me from the hand of the enemy and rescue me from the hand of the strong?”
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Teach me, and I will be silent, and if by chance I have been ignorant of anything, instruct me.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 Why have you diminished the words of truth, when there is none of you who is able to offer proof against me?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 You prepare speeches as so much noise, and you offer words into the wind.
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 You encroach upon the orphan, and you strive to undermine your friend.
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 Such is true, so finish what you have begun. Listen closely, and see if I lie.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Respond, I beg you, without contention, and, speaking what is just, pass judgment.
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 And you will not find iniquity on my tongue, nor will foolishness resound in my throat.
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

< Job 6 >