< Job 33 >

1 Therefore, hear my speeches, Job, and listen to all my words.
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 Behold, I have opened my mouth; let my tongue speak along with my throat.
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 My words are from my simple heart, and my lips will speak a pure judgment.
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 The Spirit of God made me, and the breath of the Almighty gave me life.
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 If you can, answer me, and oppose me to my face.
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 Behold, God has made me, just as he also has made you, and I, likewise, have been formed of the same clay.
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 So, truly, do not let my wonders terrify you, and do not let my eloquence be burdensome to you.
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 For you have spoken in my hearing, and I have heard the voice of your words, saying:
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 “I am clean and without sin; I am immaculate, and there is no iniquity in me.
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 Yet he has discovered blame in me, and so he has treated me like his enemy.
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 He has put my feet in fetters; he has kept watch over all my ways.”
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 Therefore, it is for this reason that you have not been justified. For I tell you that God is greater than man.
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 Do you contend against him because he has not responded to all of your words?
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 God speaks once, and he does not repeat the same thing a second time.
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 Through a dream in a vision of the night, when a deep sleep falls over men, and they are sleeping in their beds,
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 then, he opens the ears of men, and, educating them, he teaches discipline,
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 so that he may divert a man from the things that he is doing, and may free him from pride,
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 rescuing his soul from corruption and his life from passing away by the sword.
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 Likewise, he rebukes by sorrow in bed, and he causes all of his bones to become weak.
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 Bread becomes abominable to him in his life, and, to his soul, the meat which before he desired.
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 His body will waste away, and his bones, which had been covered, will be revealed.
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 His soul has approached corruption, and his life has drawn near to what is deadly.
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 If there were an angel speaking for him, one among thousands, to declare the fairness of the man,
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 he will have mercy on him, and he will say, “Free him, so that he will not descend to destruction. I have found a reason to be favorable to him.
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 His body is consumed by suffering. Let him return to the days of his youth.”
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 He will beg pardon from God, and he will be soothing to him; and he will look upon his face in jubilation, and he will restore his justice to man.
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 He will consider mankind, and he will say: “I have sinned and truly I have offended, yet I was not treated as I deserved.”
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 He has freed his soul from continuing into destruction, so that, in living, it may see the light.
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 Behold, all these things God works three times within each one,
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 so that he may revive their souls from corruption and enlighten them with the light of life.
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 Pay attention Job, and listen to me; and remain silent, while I speak.
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 Yet, if you have anything to say, answer me and speak, for I want you to be treated justly.
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 But if you do not have anything to say, then listen to me. Be quiet and I will teach you wisdom.
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”

< Job 33 >