< Job 31 >

1 I reached an agreement with my eyes, that I would not so much as think about a virgin.
Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
2 For what portion should God from above hold for me, and what inheritance should the Almighty from on high keep?
Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
3 Is not destruction held for the wicked and repudiation kept for those who work injustice?
Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
4 Does he not examine my ways and number all my steps?
Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
5 If I have walked in vanity, or if my foot has hurried towards deceitfulness,
Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
6 let him weigh me in a just balance, and let God know my simplicity.
na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
7 If my steps have turned aside from the way, or if my heart has followed my eyes, or if a blemish has clung to my hands,
Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
8 then may I sow, and let another consume, and let my offspring be eradicated.
na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
9 If my heart has been deceived over a woman, or if I have waited in ambush at my friend’s door,
Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
10 then let my wife be the harlot of another, and let other men lean over her.
na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
11 For this is a crime and a very great injustice.
Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
12 It is a fire devouring all the way to perdition, and it roots out all that springs forth.
Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
13 If I have despised being subject to judgment with my servant or my maid, when they had any complaint against me,
Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
14 then what will I do when God rises to judge, and, when he inquires, how will I respond to him?
kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
15 Is not he who created me in the womb, also he who labored to make him? And did not one and the same form me in the womb?
Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
16 If I have denied the poor what they wanted and have made the eyes of the widow wait;
kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
17 if I have eaten my morsel of food alone, while orphans have not eaten from it;
au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
18 (for from my infancy mercy grew with me, and it came out with me from my mother’s womb; )
kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
19 if I have looked down on him who was perishing because he had no clothing and the poor without any covering,
ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
20 if his sides have not blessed me, and if he were not warmed with the fleece of my sheep;
ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
21 if I have lifted up my hand over an orphan, even when it might seem to me that I have the advantage over him at the gate;
ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
22 then may my shoulder fall from its joint, and may my arm, with all its bones, be broken.
Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
23 For I have always feared God, like waves flowing over me, whose weight I was unable to bear.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
24 If I have considered gold to be my strength, or if I have called purified gold ‘my Trust;’
Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
25 if I have rejoiced over my great success, and over the many things my hand has obtained;
na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
26 if I gazed upon the sun when it shined and the moon advancing brightly,
Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
27 so that my heart rejoiced in secret and I kissed my hand with my mouth,
na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
28 which is a very great iniquity and a denial against the most high God;
hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
29 if I have been glad at the ruin of him who hated me and have exulted that evil found him,
Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
30 for I have not been given my throat to sin by asking for a curse on his soul;
Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
31 if the men around my tabernacle have not said: “He might give us some of his food, so that we will be filled,”
Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
32 for the foreigner did not remain at the door, my door was open to the traveler;
(hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
33 if, as man does, I have hidden my sin and have concealed my iniquity in my bosom;
Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
34 if I became frightened by an excessive crowd, and the disrespect of close relatives alarmed me, so that I would much rather have remained silent or have gone out the door;
kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
35 then, would he grant me a hearing, so that the Almighty would listen to my desire, and he who judges would himself write a book,
Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
36 which I would then carry on my shoulder and wrap around me like a crown?
Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
37 With each of my steps, I would pronounce and offer it, as if to a prince.
Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
38 So, if my land cries out against me, and if its furrows weep with it,
Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
39 if I have used its fruits for nothing but money and have afflicted the souls of its tillers,
ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
40 then, may thistles spring forth for me instead of grain, and thorns instead of barley. (This ended the words of Job.)
ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.

< Job 31 >