< Jeremiah 49 >

1 Against the sons of Ammon. Thus says the Lord: “Does Israel have no sons? Or is there no heir for him? Then why has Milcom possessed the inheritance of Gad, and why have his people lived in his cities?
Juu ya watu wa Amoni, Yahwe asema hivi, “Je Israeli hana watoto? Je hakuna mtu wa kurithi chochote katika Israeli? Kwa nini Moleki aikalie Gadi, na watu wake kukaa katika miji yake?
2 Therefore, behold, the days are approaching, says the Lord, when I will cause the noise of battle to be heard over Rabbah of the sons of Ammon. And it will be scattered into a tumult, and her daughters will be burned with fire. And Israel shall possess those who had possessed him, says the Lord.
Hivyo angalia, siku zinakuja - asema Yahwe - nitakapo sikizisha ishara ya vita juu ya Raba miongoni mwa watu wa Amoni, hivyo itakuwa rundo lililoachwa na binti zake watawasha moto. Maana Israeli atawamiliki wanaommiliki,” asema Yahwe.
3 Wail, O Heshbon! For Ai has been devastated. Cry out, O daughters of Rabbah! Wrap yourselves with haircloth. Mourn and circle the hedges. For Milcom will be led into the transmigration: his priests and his leaders together.
Piga kelele kwa maombolezo, Heshboni, maana Ai utaangamizwa! Piga kelele, Binti za Raba! Vaeni nguo za magunia. Ombolezeni na kukimbia kwa kuchanganyikiwa, maana Moleki anakwenda matekani, pamoja na makuhani na viongozi wake.
4 Why have you gloried in the valleys? Your valley has flowed away, O delicate daughter, for you had confidence in your treasures, and you were saying, ‘Who can approach me?’
Kwa nini mnajivunia nguvu zenu? Nguvu zenu zitakwisha, binti wasioamini, ninyi mnaotumaini utajiri wenu. Mwasema, “Nani atakayekuja kinyume changu?'
5 Behold, I will lead a terror over you, says the Lord, the God of hosts, from those who are all around you. And you will be dispersed, each one from before your sight. There will be no one who will gather together those who are fleeing.
Tazama, nitaleta kitisho juu yenu - hili ni tamko la Yahwe, Bwana wa majeshi - kitisho hiki kitatoka kwao wote wanaowazunguka. Kila mmoja wenu atatawanyika mbele yake. Hakutakuwa na wa kuwakusanya wanaotawanyika.
6 And after this, I will cause the captives of the sons of Ammon to return, says the Lord.”
Lakini baada ya haya nitarejesha mema ya watu wa Amoni - hili ni tamko la Yahwe.”
7 Against Idumea. Thus says the Lord of hosts: “Is there no longer any wisdom in Teman? Counsel has perished from the sons. Their wisdom has become useless.
Juu ya Edomu, Yahwe wa majeshi asema hivi, Je hakuna tena hekima katika Temani? Je ushauri mwema umepotea kutoka kwa wenye ufahamu? Je hekima yao imeharibika?
8 Flee and turn your backs! Descend into the chasm, O inhabitants of Dedan! For I have brought the perdition of Esau over him, the time of his visitation.
Kimbieni! Rudini nyuma! Bakini katika mashimo katika ardhi, wenyeji wa Dedani. Maana naleta maafa ya Esau juu yake wakati ninaomwadhibu.
9 If those who gather grapes had passed by you, would they not have left behind a cluster? If there were thieves in the night, they would seize what was enough for themselves.
Ikiwa wavunaji wa zabibu walikuja kwako, je wasinge acha kidogo? Ikiwa wezi walikuja usiku, je wasingeiba kiasi walichotaka?
10 Yet truly, I have stripped Esau bare. I have revealed his secrets, and he is not able to be concealed. His offspring has been devastated, with his brothers and his neighbors, and he himself will not exist.
Lakini nimempiga Esau kwa ukiwa. Nimefunua maficho yao. Hivyo hataweza kujificha mwenyewe. Watoto wake, ndugu zake, na jirani zake wameharibiwa, wamepotea.
11 Leave behind your orphans. I will make sure that they live. And your widows will hope in me.”
Acha nyuma yatima wako. Nitachukua uhai wao, na wajane wako wanaweza kuniamini.”
12 For thus says the Lord: “Behold, those who judged that they would not drink the cup, will certainly drink. And so, will you be released as if you were innocent? You will not be released as if innocent. Instead, you shall certainly drink.
Maana Yahwe asema hivi, “Tazama, wasiostahili ni lazima wanywe sehemu ya kikombe. Je mnadhani mtaachwa bila kuhadhibiwa? Hapana, maana hakika mtakunywa.
13 For I have sworn by myself, says the Lord, that Bozrah will be a desolation, and a disgrace, and a wasteland, and a curse. And all her cities will be a perpetual wilderness.
Maana nimekwisha apa kwangu mimi mwenyewe - asema Yahwe - Hiyo Bozra itakuwa hofu, aibu, magofu, na kitu cha laana. Miji yake yote itakuwa magofu daima.
14 I have heard a report from the Lord, and a legate has been sent to the nations: ‘Gather yourselves together, and go forth against her, and let us rise up to battle.’
Nimesikia habari kutoka kwa Yahwe, na mjumbe ametumwa katika mataifa, 'Kusanyikeni na kumpiga. Jiandaeni kwa vita.'
15 For behold, I have made you little among the nations, contemptible among men.
“Maana tazama, nimekufanya kuwa mdogo kulinganisha na mataifa mengine, yenye kudharauliwa na watu.
16 Your arrogance has deceived you, by the pride of your heart, you who live in the caverns of the rock and who strive to take hold of the height of the hill. But even if you make your nest like that of an eagle, I will pull you down from there, says the Lord.
Na kwa hofu yenu, kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wakaaji wa maeneo ya mwinuko, ninyi mliomiliki vilele vya vilima ili mfanye viota vyenu kama tai. Nitawashusha kutoka huko - asema Yahwe.
17 And Idumea will be a desert. Everyone who passes by it will be stupefied and will hiss over all its wounds.
Edomu atakuwa kitisho kwa kila aipitaye. Kila mtu atatetemeka na kutoa sauti kwa sababu ya maafa yake.
18 Just as Sodom and Gomorrah and their neighbors were overthrown, says the Lord: there will not be a man living there, and no son of man will tend it.
Kama maangamizi ya Sodoma na Gomora na jirani zake,” asema Yahwe, “hakuna atakayeishi pale; hakuna mtu atakayekaa huko.
19 Behold, he will ascend like a lion from the arrogance of the Jordan, against the robust beauty. For I will cause him to rush against her suddenly. And who will be the elect one, whom I may appoint over her? For who is like me? And who can endure me? And who is that pastor who can withstand my countenance?
Tazama, nitapanda kama simba kutoka katika misitu ya Yordani hata eneo la malisho mabichi. Maana nitaharakisha kumfanya Edomu kumkimbia, nami nitamweka mwingine atakayekuwa amechaguliwa kwa usimamizi huo. Maana ni nani aliyekama mimi, ni nani atakayeniagiza kuja? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
20 Because of this, listen to the counsel of the Lord, which he has undertaken concerning Edom, and to his thoughts, which he has devised concerning the inhabitants of Teman. Certainly, the little ones of the flock will cast them down, unless they scatter them with their habitation.
Hivyo sikiliza mipango ambayo Yahwe ameamua dhidi ya Edom, mipango aliyoifanya kinyume cha wakaao Temani. Bila shaka wataondolewa, hata kundi dogo kuliko yote. Nchi yao yenye malisho yao mabichi itageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
21 The earth has been shaken at the noise of their destruction. The outcry of their voice has been heard at the Red Sea.
Kwa kishindo cha kuanguka kwao nchi hutikisika. Sauti ya milio ya kukata tamaa inasikika katika Bahari ya Shamu.
22 Behold, he will ascend like an eagle and will fly. And he will spread his wings over Bozrah. And in that day, the heart of the strong ones of Idumea will be like the heart of a woman giving birth.”
Tazama, mtu fulani atapiga kama tai, na kushuka chini kwa kasi na kueneza mabawa yake juu ya Bozra. Kisha katika siku hiyo, mioyo ya askari wa Edomu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika kuzaa.”
23 Against Damascus. “Hamath has been confounded, with Arpad. For they have heard a most grievous report. They have been stirred up like the sea. Because of anxiousness, they were not able to rest.
Juu ya Dameski: “Hamathi na Arpadi zitaaibika, maana wamesikia habari ya madhara. Wanayeyuka! Wamesumbuka kama bahari, isiyotulia.
24 Damascus has been broken. She has been turned to flight. Trembling has taken hold of her. Anguish and sorrows have seized her, like a woman giving birth.
Dameski umekuwa dhaifu sana. Unageuka kukimbia; hofu imeushika, Maangaiko na maumivu yameupata, kama uchungu wa mwanamke ajifunguaye.
25 How could they have abandoned the praiseworthy city, the city of rejoicing?
Watu wake wanasema, “Umekuwaje mji maarufu, mji ambao nimeufurahia, kabla haujaachwa?
26 For this reason, her young men will fall in her streets. And all the men of battle will be silenced in that day, says the Lord of hosts.
Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika mitaa yake na askari wake wote watateketea siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi.”
27 And I will kindle a fire at the wall of Damascus, and it will devour the defensive walls of Ben-hadad.”
“Maana nitawasha moto katika kuta za Dameski, nami nitazivunja ngome za Beni Hadadi.”
28 Against Kedar and against the kingdoms of Hazor, which Nebuchadnezzar, the king of Babylon, has struck down. Thus says the Lord: “Rise up and ascend to Kedar, and lay waste to the sons of the East.
Juu ya Kedari na falme za Hazori, Yahwe amwambia hivi Nebukadneza (Basi Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa akienda kuyashambulia maeneo haya): “Inuka na uipige Kedari na kuwaharibu wale watu wa mashariki.
29 They will seize their tabernacles and their flocks. And they will take for themselves their tents, and all their vessels, and their camels. And they will call down a terror upon them on every side.
Jeshi lake litachukua hema zao na makundi yao, nguzo za hema yao, na vitu vyao vyote. Watachukua ngamia wao kutoka kwa watu wa Kedari na kuwambia, 'Hofu ipo pande zote!”
30 Flee, go away urgently! Sit in deep pits, you who inhabit Hazor, says the Lord. For Nebuchadnezzar, the king of Babylon, has undertaken a counsel against you, and he has devised plans against you.
Kimbia, Tangatanga mbali! Kaa katika maandaki ardhini, mkaao Hazori - asema Yahwe - maana Nebukadneza mfalme wa Babeli amepanga mpango kinyume chenu. Kimbieni! Geukeni!
31 Rise up, and ascend to a nation that is quiet and lives in confidence, says the Lord. They have neither gates nor bars. They dwell alone.
Simama! lishambulie taifa lililokatika amani, waishio salama,” asema Yahwe. Hawana malango wala nguzo ndani yao, na watu wake wanakaa wenyewe.
32 And their camels will be a spoil, and the multitude of their cattle will be a prey. And I will disperse, into every wind, those who have shaved their hair. And from all their confines, I will lead great destruction over them, says the Lord.
Maana farasi wao watakuwa mateka, na wingi wa mali zao utakuwa mateka wa vita. Kisha nitawatawanya katika kila upepo wanaonyoa pembe za nywele zao, nami nitaleta madhara juu yao kutoka kila upande - hili ni tamko ya Yahwe.
33 And Hazor will be a habitation for serpents, deserted even unto eternity. No man will abide there, nor will a son of man tend it.”
Hazori utakuwa makao ya mbwea, nchi isiyofaa daima. Hakuna atakayeishi huko; hakuna mwanadamu atakayekaa huko.”
34 The word of the Lord that came to Jeremiah the prophet against Elam, in the beginning of the reign of Zedekiah, the king of Judah, saying:
Hili ni neno la Yahwe lililomwijia Yeremia nabii kuhusu Elamu. Ilikuwa wakati wa mwanzo wa kutawala kwake Sedekia mfalme wa Yuda, naye akasema,
35 “Thus says the Lord of hosts: Behold, I will break the bow of Elam, and the summit of their strength.
“Yahwe wa majeshi asema hivi: Tazama, ninakaribia kumvunja mpiga upinde wa Elamu, sehemu kuu ya nguvu zao.
36 And I will lead the four winds over Elam, from the four corners of heaven. And I will scatter them into all these winds. And there will be no nation to which the fugitives of Elam will not travel.
Maana nitaleta pepo nne kutoka katika pande nne za mbingu, nami nitawatawanya watu wa Elamu katika pepo hizo zote. Hakuta kuwa na taifa ambalo kwalo waliotawanywa kutoka Elamu hawatakwenda.
37 And I will cause Elam to be terrified before their enemies and in the sight of those who seek their life. And I will lead an evil over them, the wrath of my fury, says the Lord. And I will send the sword after them, until I consume them.
Hivyo nitawavunjavunja Elamu mbele ya adui zao na mbele ya watafutao uhai wao. Maana nitaleta maangamizo dhidi yao, hasira ya gadhabu yangu - hili ni tamko la Yahwe - nami nitapeleka upanga nyuma yao hata nitakapowafuta wote.
38 And I will set my throne in Elam, and I will perish the kings and princes from there, says the Lord.
Kisha nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme na viongozi wao kutoka huko - asema Yahwe -
39 But in the last days, I will cause the captives of Elam to return, says the Lord.”
na itakuwa siku zijazo kwamba nitarejesha mema ya Elamu - asema Yahwe.”

< Jeremiah 49 >