< Jeremiah 22 >

1 Thus says the Lord: “Descend to the house of the king of Judah, and there you shall speak this word.
Bwana asema hivi, “Nenda kwenye nyumba ya mfalme wa Yuda, utangaze neno hili huko.
2 And you shall say: Listen to the word of the Lord, O king of Judah, who sits upon the throne of David: you and your servants, and your people, who enter through these gates.
Ukaseme, 'Ewe Mfalme wa Yuda, wewe aliyeketi kiti cha Daudi, usikilize neno la Bwana. Nisikilizeni, enyi watumishi wake, na ninyi, watu wake mnaokuja kwa malango haya.
3 Thus says the Lord: Exercise judgment and justice, and free anyone who is oppressed by violence from the hand of a false accuser. And do not be willing to sadden the new arrival, or the orphan, or the widow, nor should you burden them unfairly. And you shall not shed innocent blood in this place.
Bwana asema hivi, “Fanya haki na uadilifu, na mtu yeyote ambaye ameibiwa-muokoeni kutoka mkononi mwa mshindani. Usimtendee mabaya mgeni yeyote katika nchi yako, au yatima au mjane. Usifanye vurugu au kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa.
4 For if you will indeed accomplish this word, then there will enter through the gates of this house kings from the stock of David, sitting on his throne, and riding on chariots and on horses: they, and their servants, and their people.
Kwa kuwa mkifanya mambo hayo, basi wafalme wanaoketi kiti cha Daudi wataingia milango ya nyumba hii wakiendesha gari na farasi, yeye, watumishi wake, na watu wake!
5 But if you will not listen to these words, I swear by myself, says the Lord, that this house will be in desolation.
Lakini ikiwa hamsikilizi maneno haya kutoka kwangu ambayo nimeyasema-hili ndilo tamko la Bwana-basi nyumba hii ya kifalme itaharibiwa.'”
6 For thus says the Lord about the house of the king of Judah: You are to me like Gilead, the head of Lebanon. Certainly, I will make you desolate, with uninhabitable cities.
Kwa maana Bwana asema hivi juu ya nyumba ya mfalme wa Yuda, “Wewe uko kama Gileadi, au kama kilele cha Lebanoni kwangu. Hata hivyo nitakugeuza kuwa jangwa, katika miji isiyo na wenyeji.
7 And I will sanctify over you the destroying man and his weapons. And they will cut down your select cedars and throw them violently into the fire.
Kwa kuwa nimewaagiza waharibifu kuja juu yenu! Watu wenye silaha zao watakata mierezi yako iliyo bora na kuiacha kuanguka kwenye moto.
8 And many nations will pass through this city. And each one will say to his neighbor: ‘Why has the Lord acted in this way toward this great city?’
Kisha mataifa mengi yatapita kwenye mji huu. Kila mtu atamwambia yule anayefuata, “Mbona Bwana amefanya hivi kwa jiji hili kuu?”
9 And they will answer: ‘It is because they abandoned the covenant of the Lord their God, and they adored strange gods and served them.’
Na mwingine atajibu, “Kwa sababu waliiacha agano la Bwana, Mungu wao, wakainama kwa miungu mingine, wakaiabudu.”
10 You should not choose to weep for the dead, nor should you mourn over them with tears. Lament for him who is departing, for he will return no more, nor will he see his native land again.
Usilie kwa ajili ya aliyekufa. Usiomboleze kwa ajili yake. Lakini mlilie mtu yeyote anayeingia kifungoni, kwa maana hatarudi tena kuiona nchi aliyozaliwa.'
11 For thus says the Lord to Shallum, the son of Josiah, the king of Judah, who reigned in place of his father, who has departed from this place: He will not return here again.
Maana Bwana asema hivi juu ya Yehoahazi, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyekuwa mfalme badala ya Yosia babaye, 'ametoka mahali hapa, wala hatarudi.
12 Instead, he will die in the place to which I have transferred him, and he will not see this land anymore.
Atakufa huko mahali ambapo walimchukua mateka, na hataiona tena nchi hii.'
13 Woe to one who builds his house with injustice and his upper rooms without judgment, who oppresses his friend without cause and does not pay him his wages.
Ole mtu yeyote anayejenga nyumba yake kwa uovu na vyumba vyake vya juu katika udhalimu; ambao wengine hufanya kazi, lakini hawalipwi.
14 And he says: ‘I will build a broad house for myself, with spacious upper rooms.’ He makes windows for himself, and he builds the roof out of cedar, and he paints it with red ocher.
Ole mtu yeyote atakayesema, 'Nitajenga nyumba ndefu na vyumba vya juu vipana, na hujenga madirisha mapana, na kuta zenye mwerezi, na huipaka rangi nyekundu.'
15 Will you reign because you compare yourself to the cedar? Did your father not eat and drink, and act with judgment and justice, so that it would be well with him?
Je, hii ndiyo inakufanya uwe mfalme mzuri, kwamba unataka kuwa na mbao za mwerezi? Je baba yako hakula na kunywa, lakini lakini alifanya hukumu na haki? Kisha mambo yakawa mazuri kwa ajili yake.
16 He judged the case of the poor and the indigent for their good. Was this not because he knew me, says the Lord?
Alihukumu maneno ya masikini na mhitaji. Ilikuwa vizuri. Je, huku siko kunijua mimi? - hili ni tamko la Bwana.
17 Yet truly, your eyes and your heart are toward avarice and the shedding of innocent blood, and toward false accusations and the pursuit of evil deeds.
Lakini hakuna kitu machoni na moyoni mwako isipokuwa wasiwasi kwa faida yako isiyo ya haki na kwa kumwaga damu isiyo na hatia, kwa ukandamizaji kuwatendea jeuri wengine.
18 Because of this, thus says the Lord toward Jehoiakim, the son of Josiah, king of Judah: They will not mourn for him by saying, ‘Alas,’ to a brother, or, ‘Alas,’ to a sister. They will not make a noise for him and say, ‘Alas,’ to a master, or, ‘Alas,’ to a nobleman.
Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda. Hawatamwomboleza wakisema 'ole, ndugu yangu! au 'Ole, dada yangu!' Hawataomboleza kwa kusema 'Ole, bwana! ' au 'ole, utukufu!'
19 He will be buried with the burial of a donkey, having rotted and been thrown out of the gates of Jerusalem.
Atazikwa maziko ya punda, ataburuzwa mbali na kutupwa nje ya milango ya Yerusalemu.
20 Ascend to Lebanon and cry out! And utter your voice in Bashan, and cry out to those passing by. For all your lovers have been crushed.
Panda milima ya Lebanoni piga kelele. Paza sauti yako Bashani. Piga kelele kutoka kwenye milima ya Abarimu, kwa maana marafiki zako wote wataharibiwa.
21 I spoke to you in your abundance, and you said, ‘I will not listen.’ This has been your way from your youth, for you have not listened to my voice.
Nilinena nawe wakati ulioko salama, lakini ukasema, 'Sitasikia.' Hii ilikuwa desturi yako tangu ujana wako, kwani hukusikiliza sauti yangu.
22 The wind will feed all your shepherds, and your lovers will go into captivity. And then you will be confounded, and you will be ashamed of all your wickedness.
Upepo utawalisha wachungaji wako wote, na marafiki zako watakwenda kufungwa. Hakika wewe utakuwa na aibu na kufadhaika kwa matendo yako yote mabaya.
23 You who sit in Lebanon, and who nest in the cedars, in what way did you mourn when suffering came to you, like the suffering of a woman giving birth?
Wewe mfalme, wewe ambaye huishi katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni, wewe aliyefanya kiota kati ya mierezi, utakuwa na hali ya kuhurumiwa utakapopata utungu kama wakati wa kuzaa.”
24 As I live, says the Lord, if Jeconiah, the son of Jehoiakim, the king of Judah, were a ring on my right hand, I would remove him from there.
“Kama mimi niishivyo-hili ndilo tamko la Bwana-hata kama wewe, Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, ulikuwa alama ya mkono wangu wa kulia, ningekuangusha.
25 And I will deliver you into the hand of those who seek your life, and into the hand of those whose face you dread, and into the hand of Nebuchadnezzar, the king of Babylon, and into the hand of the Chaldeans.
Kwa kuwa nimewatia mikono ya wale wanaotaka uhai wenu na kwenye mkono wa wale ambao mnawaogopa, hata mkononi mwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli na Wakaldayo.
26 And I will send you, and your mother who conceived you, into a foreign land, in which you were not born, and there you shall die.
Nitawatupa wewe na mama yako aliyekuzaa katika nchi nyingine, nchi ambayo hujazaliwa, na huko utakufa.
27 And to the land about which they lift up their mind, thinking to return there, they shall not return.
Na kuhusu eneo hili ambalo watataka kurudi, hawatarudi hapa.
28 Is this man, Jeconiah, a broken earthenware vessel? Is he a vessel which is entirely unpleasing? Why have they been cast out, he and his offspring, cast out even into a land that they have not known?
Je! Hiki ni chombo kilichodharauliwa na kilichopasuka? Je, Konia ni chombo kilichodharauliwa? Kwa nini wamemtupa yeye na wazao wake, kumpeleka katika nchi wasiyoijua?
29 O earth, O earth, O earth! Listen to the word of the Lord!
Ee Ardhi, Ardhi, Ardhi! Sikieni neno la Bwana!
30 Thus says the Lord: Write: this man is barren; he is a man who will not prosper in his days. For there will not be a man from among his offspring who will sit upon the throne of David, or have authority in Judah, anymore.”
Bwana asema hivi, 'Andika juu ya mtu huyu Konia Yeye hatakuwa na mtoto. Hatafanikiwa wakati wa siku zake, wala hakuna hata mmoja kati ya uzao wake atakayefanikiwa au kuketi tena kwenye kiti cha Daudi na kutawala juu ya Yuda.'”

< Jeremiah 22 >