< Isaiah 57 >
1 The just man perishes, and there is no one who acknowledges it in his heart; and men of mercy are taken away, for there is no one who understands. For the just man has been taken away before the face of malice.
Mwenye haki hupotea, wala hakuna hata mmoja awazaye hilo moyoni mwake; watu wanaomcha Mungu huondolewa, wala hakuna hata mmoja anayeelewa kuwa wenye haki wameondolewa ili wasipatikane na maovu.
2 Let peace arrive. Let he who has walked in his righteousness find rest on his bed.
Wale waendao kwa unyofu huwa na amani; hupata pumziko walalapo mautini.
3 But come here, you sons of the prophetess, you offspring of an adulterous man and a fornicating woman.
“Lakini ninyi: Njooni hapa, ninyi wana wa wachawi, ninyi wazao wa wazinzi na makahaba!
4 Whom are you mocking? Against whom have you opened your mouth wide and wagged your tongue? Are you not sons of wickedness, a lying offspring,
Mnamdhihaki nani? Ni nani mnayemcheka kwa dharau, na kumtolea ndimi zenu? Je, ninyi si watoto wa waasi, uzao wa waongo?
5 who are being consoled by idols under every leafy tree, immolating little children at the torrents, under the high rocks?
Mnawaka tamaa katikati ya mialoni na chini ya kila mti uliotanda matawi; mnawatoa kafara watoto wenu kwenye mabonde na chini ya majabali yenye mianya.
6 Your portion is in the currents of the torrent; this is your lot! And you yourselves have poured out libations to them; you have offered sacrifice. Should I not be angry over these things?
“Sanamu zilizo katikati ya mawe laini ya mabondeni ndizo fungu lenu; hizo ndizo sehemu yenu. Naam, kwa hizo mmemimina sadaka za vinywaji, na kutoa sadaka za nafaka. Katika haya yote, niendelee kuona huruma?
7 Upon a high and lofty mountain, you have placed your bed, and you have ascended to that place to immolate victims.
Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka, huko ulikwenda kutoa dhabihu zako.
8 And behind the door, and beyond the post, you have set up your memorial. For you uncovered yourself next to me, and you received an adulterer. You widened your bed, and you formed a pact with them. You loved their bed with an open hand.
Nyuma ya milango yako na miimo yako umeweka alama zako za kipagani. Kwa kuniacha mimi, ulifunua kitanda chako, umepanda juu yake na kukipanua sana; ulifanya patano na wale ambao unapenda vitanda vyao, nawe uliangalia uchi wao.
9 And you have adorned yourself for the king with ointments, and you have increased your cosmetics. You have sent your representatives to distant places, and you have debased yourself all the way to Hell. (Sheol )
Ulikwenda kwa Moleki ukiwa na mafuta ya zeituni, na ukaongeza manukato yako. Ukawatuma wajumbe wako mbali sana, ukashuka kwenye kaburi lenyewe! (Sheol )
10 You have been wearied by the multitude of your own ways. Yet you did not say, “I will cease.” You have found life by your own hand; because of this, you have not prayed.
Ulikuwa umechoshwa na njia zako zote, lakini hukusema, ‘Hakuna tumaini.’ Ulipata uhuisho wa nguvu zako, kwa sababu hiyo hukuzimia.
11 For whose sake have you been anxiously afraid, so that you would lie and not be mindful of me, nor consider me in your heart? For I am silent, and I am like someone who does not see, and so you have forgotten me.
“Ni nani uliyemhofu hivyo na kumwogopa hata ukawa mwongo kwangu, wala hukunikumbuka au kutafakari hili moyoni mwako? Si ni kwa sababu nimekuwa kimya muda mrefu hata huniogopi?
12 I will announce your justice, and your works will not benefit you.
Nitaifunua haki yako na matendo yako, nayo hayatakufaidi.
13 When you cry out, let your followers free you. But the wind will carry them all away; a breeze will take them up. But he who has faith in me will inherit the earth and will possess my holy mountain.
Utakapolia kwa kuhitaji msaada, sanamu zako ulizojikusanyia na zikuokoe! Upepo utazipeperusha zote, pumzi peke yake itazipeperusha, Lakini mtu atakayenifanya kimbilio lake, atairithi nchi na kuumiliki mlima wangu mtakatifu.”
14 And I will say: “Make way! Grant passage! Move to the side of the path! Take the obstacles out of the way of my people!”
Tena itasemwa: “Jengeni, jengeni, itengenezeni njia! Ondoeni vikwazo katika njia ya watu wangu.”
15 For this is said by the Most High, the Sublime One, who dwells in eternity. And his name is Holy, for he dwells in the exalted and holy place, and he acts with a restrained and humble spirit, to revive the spirit of the humble, and to revive the heart of the contrite.
Kwa maana hili ndilo asemalo Aliye juu, yeye aliyeinuliwa sana, yeye aishiye milele, ambaye jina lake ni Mtakatifu: “Ninaishi mimi mahali palipoinuka na patakatifu, lakini pia pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na mwenye roho ya unyenyekevu, ili kuzihuisha roho za wanyenyekevu na kuihuisha mioyo yao waliotubu.
16 For I will not contend unceasingly, and I will not be angry to the end. For I will exhale my breath, and the Spirit will go forth from my face.
Sitaendelea kulaumu milele, wala sitakasirika siku zote, kwa kuwa roho ya mwanadamu ingezimia mbele zangu: yaani pumzi ya mwanadamu niliyemuumba.
17 Because of the iniquity of his avarice, I was angry, and I struck him down. I concealed my face from you, and I was angry. And he went astray by wandering in his heart.
Nilighadhibika na tamaa yake ya dhambi; nilimwadhibu, nikauficha uso wangu kwa hasira, na bado aliendelea katika njia zake za tamaa.
18 I saw his ways, and I healed him, and I led him back again, and I restored consolations to him and to those who mourn for him.
Nimeziona njia zake, lakini nitamponya, nitamwongoza na kumrudishia upya faraja,
19 I created the fruit of the lips: peace, peace to him who is far away, and peace to him who is near, said the Lord, and I healed him.
nikiumba sifa midomoni ya waombolezaji katika Israeli. Amani, amani, kwa wale walio mbali na kwa wale walio karibu,” asema Bwana. “Nami nitawaponya.”
20 But the impious are like the raging sea, which is not able to be quieted, and its waves stir up dirt and mud.
Bali waovu ni kama bahari ichafukayo, ambayo haiwezi kutulia, mawimbi yake hutupa takataka na matope.
21 There is no peace for the impious, says the Lord God.
Mungu wangu asema, “Hakuna amani kwa waovu.”