< Haggai 2 >

1 And in the seventh month, on the twenty-first of the month, the word of the Lord came, by the hand of Haggai the prophet, saying:
Katika siku ya ishirini na moja ya mwezi wa saba, neno la Bwana lilikuja kupitia nabii Hagai, kusema:
2 Speak to Zerubbabel the son of Shealtiel, the governor of Judah, and to Jesus the son of Jehozadak, the high priest, and to the remainder of the people, saying:
“Sema na Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, na mabaki ya watu. Uwaulize,
3 Who is left among you, who saw this house in its first glory? And how do you see it now? Is it not, in comparison to that, as nothing in your eyes?
‘Ni nani miongoni mwenu aliyebaki ambaye aliiona hii nyumba katika utukufu wake wa mwanzo? Sasa inaonekanaje kwenu? Je, haionekani kwenu kama si kitu?
4 And now be strengthened, Zerubbabel, says the Lord. And be strengthened, Jesus the son of Jehozadak, the high priest. And be strengthened, all people of the land, says the Lord of hosts. For I am with you, says the Lord of hosts.
Lakini sasa uwe imara, ee Zerubabeli,’ asema Bwana. ‘Kuwa imara, ee kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki. Mwe imara, enyi watu wote wa nchi,’ asema Bwana, ‘na mfanye kazi. Kwa kuwa mimi nipo pamoja nanyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
5 And act according to the word that I planted with you when you departed from the land of Egypt. And my Spirit will be in your midst. Do not be afraid.
‘Hili ndilo nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri. Pia Roho wangu anadumu katikati yenu. Msiogope.’
6 For thus says the Lord of hosts: There is yet one brief time, and I will move heaven and earth, and the sea and the dry land.
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Baada ya muda kidogo kwa mara nyingine nitazitikisa mbingu na nchi, bahari na nchi kavu.
7 And I will move all nations. And the Desired of all nations will arrive. And I will fill this house with glory, says the Lord of hosts.
Nitatikisa mataifa yote, nacho kile kinachotamaniwa na mataifa yote kitakuja, nami nitaujaza utukufu katika nyumba hii,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
8 Mine is the silver, and mine is the gold, says the Lord of hosts.
‘Fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
9 Great shall be the glory of this house, the last more than the first, says the Lord of hosts. And in this place, I will bestow peace, says the Lord of hosts.
‘Utukufu wa nyumba hii ya sasa utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa ile nyumba ya mwanzoni,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. ‘Na mahali hapa nitawapa amani,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
10 On the twenty-fourth of the ninth month, in the second year of king Darius, the word of the Lord came to Haggai the prophet, saying:
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilikuja kwa nabii Hagai:
11 Thus says the Lord of hosts: the priests question the law, saying:
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ulizeni makuhani jinsi sheria inavyosema:
12 If a man will have carried sanctified flesh in the pocket of his garment, and the top of it touches his bread, or appetizer, or wine, or oil, or any food, shall it be sanctified? But the priests responded by saying, “No.”
Kama mtu akibeba nyama iliyowekwa wakfu katika pindo la vazi lake, kisha lile pindo likagusa mkate au mchuzi, divai, mafuta au chakula kingine, je, kitu hicho kitakuwa kimewekwa wakfu?’” Makuhani wakajibu, “La hasha.”
13 And Haggai said, “If the polluted in soul will have touched any of all these things, shall it be contaminated?” And the priests responded and said, “It shall be contaminated.”
Kisha Hagai akasema, “Je, kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti akigusa mojawapo ya vitu hivi, kitu hicho kitakuwa kimetiwa unajisi?” Makuhani wakajibu, “Ndiyo, huwa kimenajisiwa.”
14 And Haggai answered and he said: Such is this people, and such is this nation before my face, says the Lord, and such is all the work of their hands. And so all that they have offered there has been contaminated.
Kisha Hagai akasema, “‘Basi ndivyo walivyo machoni pangu hawa watu na taifa hili,’ asema Bwana. ‘Lolote wafanyalo na chochote watoacho hapo ni najisi.
15 And now, consider in your hearts, from this day and beyond, before stone may be placed upon stone in the temple of the Lord:
“‘Sasa fikirini kwa uangalifu kuanzia leo na kuendelea: tafakarini jinsi mambo yalivyokuwa kabla halijawekwa jiwe moja juu ya lingine katika Hekalu la Bwana.
16 when you approached a pile of twenty measures, and they became ten, and you entered to the press, to press out fifty bottles, and they became twenty,
Wakati mtu alipoendea lundo la nafaka la vipimo ishirini, kulikuwa na vipimo kumi tu. Wakati mtu alipoendea pipa la mvinyo ili kuchota vipimo hamsini, kulikuwa na vipimo ishirini tu.
17 how I struck you with a burning wind, and a mildew, and a hailstorm, all the works of your hand, yet there was no one among you who returned to me, says the Lord.
Kazi zenu zote za mikono nilizipiga kwa ukame, ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo, hamkunigeukia mimi,’ asema Bwana.
18 Set your hearts from this day and into the future, from the twenty-fourth day of the ninth month, from the day that the foundations of the temple of the Lord have been uttered, and place it upon your heart.
‘Tangu leo na kuendelea, kuanzia siku hii ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, tafakarini siku ambayo msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa. Tafakarini:
19 Has the seed been germinated yet? And has the vine, and the fig tree, and the pomegranate, and the olive tree still not flourished? From this day on, I will bless you.
Je, bado kuna mbegu iliyobakia ghalani? Mpaka sasa, hakuna mzabibu au mtini, mkomamanga wala mzeituni uliozaa tunda. “‘Kuanzia leo na kuendelea, nitawabariki.’”
20 And the word of the Lord came a second time to Haggai, on the twenty-fourth of the month, saying:
Neno la Bwana likamjia Hagai kwa mara ya pili katika siku ya ishirini na nne ya mwezi kusema:
21 Speak to Zerubbabel the governor of Judah, saying: I will move both heaven and earth.
“Mwambie Zerubabeli mtawala wa Yuda kwamba nitazitikisa mbingu na nchi.
22 And I will overturn the throne of kingdoms, and I will crush the strength of the kingdom of the Gentiles. And I will overturn the four-horse chariot, and its rider; and the horses and their riders shall be brought down, a man by the sword of his brother.
Nitapindua viti vya enzi vya falme, na kuziharibu kabisa nguvu za falme za kigeni. Nitapindua magari ya vita pamoja na waendeshaji wake; farasi na wapanda farasi wataanguka, kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.
23 In that day, says the Lord of hosts, I will take you, Zerubbabel the son of Shealtiel, my servant, says the Lord, and will set you like a seal, for I have chosen you, says the Lord of hosts.
“‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitakuchukua wewe, mtumishi wangu Zerubabeli mwana wa Shealtieli,’ asema Bwana. ‘Nitakufanya kama pete yangu ya muhuri, kwa kuwa nimekuchagua,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”

< Haggai 2 >