< Genesis 28 >

1 And so Isaac called for Jacob, and he blessed him, and he instructed him, saying: “Do not be willing to accept a mate from the family of Canaan.
Basi Isaki akamwita Yakobo, akambariki na akamwamuru, akisema, “Usioe mwanamke wa Kikanaani.
2 But go, and journey to Mesopotamia of Syria, to the house of Bethuel, your mother’s father, and there accept for yourself a wife from the daughters of Laban, your maternal uncle.
Nenda mara moja mpaka Padan-Aramu, kwenye nyumba ya Bethueli baba wa mama yako. Uchukue mke kati ya binti za Labani ambaye ni ndugu wa mama yako.
3 And may God almighty bless you, and may he cause you to increase and also to multiply, so that you may be influential among the people.
Mungu Mwenyezi na akubariki uwe na uzao uongezeke idadi yako upate kuwa jamii kubwa ya watu.
4 And may he give the blessings of Abraham to you, and to your offspring after you, so that you may possess the land of your sojourning, which he promised to your grandfather.”
Na akupe wewe na uzao wako baraka aliyopewa Abrahamu, upate kumiliki nchi unayoishi sasa kama mgeni, nchi ambayo Mungu alimpa Abrahamu.”
5 And when Isaac had dismissed him, setting out, he went to Mesopotamia of Syria, to Laban, the son of Bethuel, the Syrian, the brother to Rebekah, his mother.
Kisha Isaki akamuaga Yakobo, naye akaenda Padan-Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, ndugu wa Rebeka, aliyekuwa mama wa Yakobo na Esau.
6 But Esau, seeing that his father had blessed Jacob and had sent him into Mesopotamia of Syria, to take a wife from there, and that, after the blessing, he had instructed him, saying: ‘You shall not accept a wife from the daughters of Canaan,’
Sasa Esau akajua kuwa Isaki amembariki Yakobo na kumtuma kwenda Padan-Aramu ili achukue mke huko na kwamba alipombariki alimwamuru akisema, “Usioe mke katika binti za Wakanaani,”
7 and that Jacob, obeying his parents, had gone into Syria,
tena kwamba Yakobo amewatii baba yake na mama yake naye amekwenda Padan-Aramu.
8 having evidence also that his father did not look with favor upon the daughters of Canaan,
Esau akatambua jinsi ambavyo baba yake Isaki anavyowachukia binti za Wakanaani.
9 he went to Ishmael, and he took as a wife, beside those he had before, Mahalath, the daughter of Ishmael, Abraham’s son, the sister of Nebaioth.
Ndipo Esau akaenda kwa Ishmaeli, akamwoa Mahalati, ndugu wa Nebayothi na binti wa Ishmaeli mwana wa Abrahamu, kuongezea wale wake wengine aliokuwa nao.
10 Meanwhile Jacob, having departed from Beersheba, continued on to Haran.
Yakobo akatoka Beer-Sheba kwenda Harani.
11 And when he had arrived at a certain place, where he would rest after the setting of the sun, he took some of the stones that lay there, and placing them under his head, he slept in the same place.
Alipofika mahali fulani, akalala hapo kwa sababu jua lilikuwa limetua. Akachukua jiwe moja la mahali pale, akaliweka chini ya kichwa chake akajinyoosha akalala usingizi.
12 And he saw in his sleep: a ladder standing upon the earth, with its top touching heaven, also, the Angels of God ascending and descending by it,
Akaota ndoto ambayo aliona ngazi imesimamishwa juu ya ardhi, ncha yake ikiwa imefika mbinguni na malaika wa Mungu wakawa wakipanda na kushuka juu yake.
13 and the Lord, leaning upon the ladder, saying to him: “I am the Lord, the God of Abraham your father, and the God of Isaac. The land, in which you sleep, I will give to you and to your offspring.
Juu yake alisimama Bwana, akasema, “Mimi ni Bwana, Mungu wa baba yako Abrahamu na Mungu wa Isaki. Nchi ambayo umelala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
14 And your offspring will be like the dust of the earth. You will spread abroad to the West, and to the East, and to the North, and to the Meridian. And in you and in your offspring, all the tribes of the earth shall be blessed.
Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi na mashariki, kaskazini na kusini. Kupitia wewe na uzao wako mataifa yote ya duniani yatabarikiwa.
15 And I will be your guardian wherever you will journey, and I will bring you back into this land. Neither will I dismiss you, until I have accomplished all that I have said.”
Niko pamoja nawe nami nitakulinda kila uendako na nitakurudisha katika nchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapofanya hayo niliyokuahidi.”
16 And when Jacob had awakened from sleep, he said, “Truly, the Lord is in this place, and I did not know it.”
Yakobo alipoamka kutoka usingizini, akawaza, “Hakika Bwana yuko mahali hapa, wala mimi sikujua.”
17 And being terrified, he said: “How terrible this place is! This is nothing other than the house of God and the gateway of heaven.”
Kwa hiyo akaogopa, akasema, “Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka hapa ndipo nyumba ya Mungu ilipo, hili ni lango la mbinguni.”
18 Therefore, Jacob, arising in the morning, took the stone which he had placed under his head, and he set it up as monument, pouring oil over it.
Asubuhi yake na mapema, Yakobo akalichukua lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
19 And he called the name of the city, ‘Bethel,’ which before was called Luz.
Mahali pale akapaita Betheli, ingawa mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.
20 And then he made a vow, saying: “If God will be with me, and will guard me along the way by which I walk, and will give me bread to eat and clothing to wear,
Kisha Yakobo akaweka nadhiri, akisema, “Kama Mungu akiwa pamoja nami na kunilinda katika safari niendayo, akinipa chakula nile na nguo nivae
21 and if I will return prosperously to my father’s house, then the Lord will be my God,
na nirudi salama nyumbani kwa baba yangu, hapo ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu,
22 and this stone, which I have set up as a monument, will be called ‘the House of God.’ And from all the things that you will give to me, I will offer tithes to you.”
nalo jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu na katika yote utakayonipa nitakutolea wewe sehemu ya kumi.”

< Genesis 28 >