< Ezra 7 >
1 Now after these things, during the reign of Artaxerxes, the king of the Persians, Ezra, the son of Seraiah, the son of Azariah, the son of Hilkiah,
Baada ya mambo haya, wakati wa utawala wa Artashasta mfalme wa Uajemi, Ezra mwana wa Seraya, mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,
2 the son of Shallum, the son of Zadok, the son of Ahitub,
mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu,
3 the son of Amariah, the son of Azariah, the son of Meraioth,
mwana wa Amaria, mwana wa Azaria, mwana wa Merayothi,
4 the son of Zerahiah, the son of Uzzi, the son of Bukki,
mwana wa Zerahia, mwana wa Uzi, mwana wa Buki,
5 the son of Abishua, the son of Phinehas, the son of Eleazar, the son of Aaron, priest from the beginning,
mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi, mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani mkuu Aroni.
6 this same Ezra, ascended from Babylon; and he was a proficient scribe in the law of Moses, which the Lord God gave to Israel. And the king granted to him his every petition. For the hand of the Lord, his God, was over him.
Huyu Ezra alipanda kutoka Babeli. Alikuwa mwalimu mwenye ujuzi mzuri katika sheria ya Mose, ambayo Bwana, Mungu wa Israeli, alikuwa ametoa. Mfalme alikuwa amempa Ezra kila kitu alichoomba, kwa maana Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye.
7 And some from the sons of Israel, and from the sons of the priests, and from the sons of the Levites, and from the singing men, and from the gatekeepers, and from the temple servants ascended to Jerusalem, in the seventh year of king Artaxerxes.
Pia baadhi ya Waisraeli, wakiwemo makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu na watumishi wa Hekalu, nao walikuja Yerusalemu mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
8 And they arrived at Jerusalem in the fifth month, in the same seventh year of the king.
Ezra aliwasili Yerusalemu mwezi wa tano wa mwaka wa saba wa utawala wa Mfalme Artashasta.
9 For on the first day of the first month, he began to ascend from Babylon, and on the first day of the fifth month, he arrived at Jerusalem. For the good hand of his God was over him.
Ezra alianza safari yake kutoka Babeli tangu siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, naye akawasili Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano, kwa maana mkono wa neema wa Mungu wake ulikuwa juu yake.
10 For Ezra prepared his heart, so that he might search the law of the Lord, and so that he might keep and teach precept and judgment in Israel.
Kwa maana Ezra alikuwa amejitoa kwa moyo wote kujifunza na kushika sheria ya Bwana na kuwafundisha watu wa Israeli amri na sheria zake.
11 Now this is a copy of the letter of the edict, which king Artaxerxes gave to Ezra, the priest, a scribe well-taught in the words and precepts of the Lord and in his ceremonies in Israel:
Hii ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alikuwa amempa Ezra aliyekuwa kuhani na mwalimu, mtu aliyeelimika katika mambo yahusuyo maagizo na amri za Bwana kwa Israeli.
12 “Artaxerxes, king of kings, to Ezra, the priest, a very learned scribe of the law of the God of heaven: a greeting.
Artashasta, mfalme wa wafalme, Kwa Ezra kuhani, mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni: Salamu.
13 It has been decreed by me, that whosoever wishes, among the people of Israel and their priests and Levites within my kingdom, to go to Jerusalem, may go with you.
Sasa naamuru kwamba mtu yeyote Mwisraeli katika ufalme wangu, pamoja na makuhani na Walawi, ambaye anataka kwenda Yerusalemu pamoja nawe aweza kwenda.
14 For you have been sent from the face of the king and his seven counselors, so that you may visit Judea and Jerusalem by the law of your God, which is in your hand,
Unatumwa na mfalme na washauri wake saba kuchunguza kuhusu Yuda na Yerusalemu kulingana na Sheria ya Mungu wako, iliyoko mkononi mwako.
15 and so that you may carry the silver and gold, which the king and his counselors have freely offered to the God of Israel, whose tabernacle is in Jerusalem.
Zaidi ya hayo, uchukue pamoja nawe fedha na dhahabu ambazo mfalme na washauri wake wamempa Mungu wa Israeli kwa hiari, Mungu ambaye maskani yake yako Yerusalemu,
16 And all the silver and gold, as much as you will find in the entire province of Babylon, and which the people will wish to offer, and which some of the priests will offer freely to the house of their God, which is in Jerusalem,
pia fedha na dhahabu zote unazoweza kupata kutoka jimbo la Babeli, pamoja na sadaka za hiari watakazotoa watu na makuhani kwa ajili ya Hekalu la Mungu wao katika Yerusalemu.
17 accept it freely. And with this money, carefully purchase calves, rams, lambs, and their sacrifices and libations, and offer these upon the altar of the temple of your God, which is in Jerusalem.
Hakikisha kwamba fedha hizi zimetumika kununua mafahali, kondoo dume na wana-kondoo pamoja na sadaka za nafaka na sadaka za vinywaji, uvitoe dhabihu juu ya madhabahu ya Hekalu la Mungu wenu katika Yerusalemu.
18 But also, whatever it will please you and your brothers to do with the remainder of the silver and gold, do so in accord with the will of your God.
Kisha wewe na Wayahudi ndugu zako mnaweza kufanya lolote linaloonekana jema sana kwa fedha na dhahabu zilizosalia, kulingana na mapenzi ya Mungu wenu.
19 Likewise, the vessels that have been given to you for the ministry of the house of your God, deliver these to the sight of God in Jerusalem.
Uvitoe kwa Mungu wa Yerusalemu vyombo vyote ulivyokabidhiwa kwa ajili ya ibada katika Hekalu la Mungu wako.
20 Then, whatever more will be needed for the house of your God, as much as is necessary for you to spend, it shall be given from the treasury, and from the king’s finances,
Kitu kingine chochote kinachohitajika kwa ajili ya Hekalu la Mungu wenu ambacho unatakiwa kukitoa, waweza kukitoa kutoka hazina ya mfalme.
21 and by me. I, king Artaxerxes, have appointed and decreed to all the keepers of the public treasury, those who are beyond the river, that whatever Ezra, the priest, a scribe of the law of the God of heaven, shall ask of you, you shall provide it without delay,
Mimi, Mfalme Artashasta, sasa naagiza watunza hazina wote wa Ngʼambo ya Mto Frati kutoa kwa bidii chochote kwa Ezra kuhani na mwalimu wa Sheria ya Mungu wa mbinguni atakachohitaji kwenu,
22 even up to one hundred talents of silver, and up to one hundred cors of wheat, and up to one hundred baths of wine, and up to one hundred baths of oil, and truly salt without measure.
talanta 100 za fedha, ngano kori 100, divai bathi 100, mafuta ya zeituni bathi 100, na chumvi kiasi chochote.
23 All that pertains to the rite of the God of heaven, let it be distributed scrupulously to the house of the God of heaven, lest perhaps he may become angry against the kingdom of the king and his sons.
Chochote ambacho Mungu wa mbinguni ameagiza, kifanyike kwa ukamilifu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wa mbinguni. Kwa nini pawepo ghadhabu dhidi ya utawala wa mfalme na wanawe?
24 Likewise, we would make known to you, about all the priests, and the Levites, and the singers, and the gatekeepers, and the temple servants, and the ministers of the house of this God, that you have no authority to impose tax, or tribute, or duty upon them.
Pia ninyi fahamuni kuwa hamna mamlaka ya kuwatoza kodi, ushuru au ada makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, watumishi wa Hekalu au wafanyakazi wengine kwenye nyumba ya Mungu.
25 But as for you, Ezra, in accord with the wisdom of your God, which is in your hand, appoint judges and magistrates, so that they may judge the entire people, which is beyond the river, especially so that they may know the law of your God, but also so as to teach the ignorant freely.
Nawe Ezra, kufuatana na hekima ya Mungu wenu uliyo nayo, weka mahakimu na waamuzi wote wanaozifahamu sheria za Mungu wenu ili watoe haki kwa watu wote wa Ngʼambo ya Mto Frati. Nawe inakupasa umfundishe yeyote ambaye hazifahamu.
26 And anyone who will not diligently keep the law of your God, and the law of the king, judgment shall be upon him, either to death, or to exile, or to the confiscation of his goods, or certainly to prison.”
Yeyote ambaye hataitii sheria ya Mungu wenu pia sheria ya mfalme, hakika lazima aadhibiwe kwa kuuawa, kuhamishwa, kunyangʼanywa mali au kufungwa gerezani.
27 Blessed be the Lord, the God of our fathers, who has put this into the heart of the king, so that he may glorify the house of the Lord, which is in Jerusalem.
Sifa ziwe kwa Bwana, Mungu wa baba zetu, Mungu ambaye kwa njia hii ameweka ndani ya moyo wa mfalme kuipa heshima nyumba ya Bwana iliyoko Yerusalemu, kwa namna hii
28 For he has turned his mercy toward me in the sight of the king, and his counselors, and all the powerful leaders of the king. And so, having been strengthened by the hand of the Lord, my God, which was upon me, I gathered together some of the leaders of Israel, those who were to go up with me.
ambaye ameniongezea kibali chake mbele ya mfalme, washauri wake na maafisa wote wa mfalme wenye uwezo. Kwa kuwa mkono wa Bwana Mungu wangu ulikuwa pamoja nami, nilijipa moyo nikakusanya watu walio viongozi kutoka Israeli wakwee pamoja nami.